< 1 Samuel 28 >

1 O sırada Filistliler İsrail'le savaşmak için askeri birliklerini topladılar. Akiş Davut'a, “Adamlarınla birlikte benim yanımda savaşacağını bilmelisin” dedi.
Siku zile Wafilisti wakakusanya majeshi yao ili kupigana vita dhidi ya Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Lazima ujue kuwa wewe pamoja na watu wako mtafuatana nami kwenda vitani.”
2 Davut, “O zaman sen de kulunun neler yapabileceğini göreceksin!” diye karşılık verdi. Akiş, “İyi!” dedi, “Yaşadığın sürece seni kendime koruma görevlisi atayacağım.”
Daudi akasema, “Ndipo wewe mwenyewe utakapojionea jambo ambalo mtumishi wako anaweza kufanya.” Akishi akamjibu Daudi, “Vyema sana, mimi nitakufanya uwe mlinzi wangu daima.”
3 Samuel ölmüş, bütün İsrail halkı onun için yas tutmuştu. Onu kendi kenti Rama'da gömmüşlerdi. Saul da cincilerle ruhlara danışanları ülkeden kovmuştu.
Wakati huo Samweli alikuwa amekufa, nao Israeli wote walikuwa wamemwombolezea na kumzika kwenye mji wake mwenyewe huko Rama. Sauli alikuwa amewafukuza waaguzi na wachawi.
4 Filistliler toplanıp Şunem'e gittiler ve orada ordugah kurdular. Saul da bütün İsrailliler'i toplayıp Gilboa Dağı'nda ordugah kurdu.
Wafilisti wakakusanyika na kupiga kambi yao huko Shunemu, naye Sauli akawakusanya Waisraeli wote na kupiga kambi yao huko Gilboa.
5 Saul Filist ordusunu görünce korkup büyük dehşete kapıldı.
Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, akaogopa; moyo wake ukajawa na hofu kuu.
6 RAB'be danıştıysa da, RAB ona ne düşlerle, ne Urim, ne de peygamberler aracılığıyla yanıt verdi.
Ndipo Sauli akauliza ushauri kwa Bwana, lakini Bwana hakumjibu kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala kwa njia ya manabii.
7 Bunun üzerine Saul görevlilerine, “Bana bir cinci kadın bulun da varıp ona danışayım” diye buyruk verdi. Görevliler, “Eyn-Dor'da bir cinci kadın var” dediler.
Basi Sauli akawaambia watumishi wake, “Nitafutieni mwanamke mwaguzi ili nimwendee, nipate kuuliza kwake.” Watumishi wake wakamwambia, “Yuko mwanamke mmoja huko Endori.”
8 Böylece Saul başka giysilere bürünüp kılığını değiştirdi. Geceleyin yanına iki kişi alıp kadının yaşadığı yere gitti. Kadına, “Lütfen benim için ruhlara danış ve sana söyleyeceğim kişiyi çağır” dedi.
Hivyo Sauli akajigeuza kwa kuvaa mavazi mengine, naye usiku akiwa amefuatana na watu wawili wakaenda kwa huyo mwanamke. Akamwambia, “Nibashirie kwa uaguzi, unipandishie yule nitakayekutajia.”
9 Ama kadın ona şu karşılığı verdi: “Saul'un neler yaptığını, cincilerle ruhlara danışanları ülkeden kovduğunu biliyorsun. Öyleyse neden beni öldürmek için tuzak kuruyorsun?”
Huyo mwanamke akamwambia, “Wewe unajua lile alilofanya Mfalme Sauli. Amewakatilia mbali waaguzi, wapiga ramli wote na wachawi katika nchi. Mbona umenitegea maisha yangu ili wapate kuniua?”
10 Saul, “Yaşayan RAB'bin adıyla derim ki, bundan sana bir kötülük gelmeyecek” diye ant içti.
Sauli akamwapia huyo mwanamke kwa Jina la Bwana, akasema, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo, hutaadhibiwa kwa ajili ya jambo hili.”
11 Bunun üzerine kadın, “Sana kimi çağırayım?” diye sordu. Saul, “Bana Samuel'i çağır” dedi.
Ndipo yule mwanamke akauliza, “Je unataka nikupandishie nani?” Sauli akasema, “Nipandishie Samweli.”
12 Kadın, Samuel'i görünce çığlık atarak, “Sen Saul'sun! Neden beni kandırdın?” dedi.
Yule mwanamke alipomwona Samweli, alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamuuliza Sauli, “Mbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.”
13 Kral ona, “Korkma!” dedi, “Ne görüyorsun?” Kadın, “Yerin altından çıkan bir ilah görüyorum” diye karşılık verdi.
Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona nini?” Yule mwanamke akasema, “Naona mungu unapanda kutoka ardhini.”
14 Saul, “Neye benziyor?” diye sordu. Kadın, “Cüppe giymiş yaşlı bir adam yukarıya çıkıyor” dedi. O zaman Saul onun Samuel olduğunu anladı; eğilip yüzüstü yere kapandı.
Sauli akamuuliza, “Ni mfano wa nini?” Yule mwanamke akasema, “Ni mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.” Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi, uso wake hadi ardhini.
15 Samuel Saul'a, “Neden beni çağırtıp rahatsız ettin?” dedi. Saul, “Büyük sıkıntı içindeyim” diye yanıtladı, “Filistliler bana karşı savaşıyor ve Tanrı da beni terk etti. Artık bana ne peygamberler aracılığıyla, ne de düşlerle yanıt veriyor. Bu yüzden, ne yapmam gerektiğini bana bildirmen için seni çağırttım.”
Samweli akamuuliza Sauli, “Kwa nini unanitaabisha kwa kunipandisha juu?” Sauli akasema, “Mimi ninasumbuka sana, kwa maana Wafilisti wanapigana vita dhidi yangu, naye Mungu ameniacha. Hanijibu tena wala kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita wewe ili unijulishe la kufanya.”
16 Samuel, “RAB seni terk edip sana düşman olduğuna göre, neden bana danışıyorsun?” dedi,
Samweli akamuuliza, “Kwa nini uniulize mimi, maadamu Bwana amekuacha na kuwa adui yako?
17 “RAB benim aracılığımla söylediğini yaptı, krallığı senden alıp soydaşın Davut'a verdi.
Bwana ametenda lile alilotangulia kusema kupitia kwangu. Bwana ameurarua ufalme kutoka mikononi mwako, naye amempa mmoja wa jirani zako, yaani Daudi.
18 Çünkü sen RAB'bin buyruğuna uymadın, O'nun alevlenen öfkesini Amalekliler'e uygulamadın. RAB bugün bunları bu yüzden başına getirdi.
Kwa sababu wewe hukumtii Bwana, wala hukumtimizia ghadhabu yake kali juu ya Waamaleki, Bwana amekutendea mambo haya leo.
19 RAB seni de, İsrail halkını da Filistliler'in eline teslim edecek. Yarın sen ve oğulların bana katılacaksınız. RAB İsrail ordusunu da Filistliler'in eline teslim edecek.”
Zaidi ya hayo, Bwana atawatia Israeli pamoja na wewe mikononi mwa Wafilisti, na kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. Bwana pia atalitia jeshi la Israeli mikononi mwa Wafilisti.”
20 Saul birden boylu boyunca yere düştü. Samuel'in sözlerinden ötürü büyük korkuya kapıldı. Gücü de kalmamıştı; çünkü bütün gün, bütün gece yemek yememişti.
Papo hapo Sauli akaanguka chini, akajinyoosha, akiwa amejawa na hofu kwa ajili ya maneno ya Samweli. Nguvu zake zikamwishia kwa maana alikuwa hajala chochote mchana ule wote na usiku.
21 Kadın Saul'a yaklaştı. Onun büyük şaşkınlık içinde olduğunu görünce, “Bak, kölen sözünü dinledi” dedi, “Canımı tehlikeye atarak benden istediğini yaptım.
Yule mwanamke alipomwendea Sauli na kumwona amepatwa na hofu, akamwambia, “Tazama, mimi mtumishi wako mwanamke nimekutii. Nimeweka maisha yangu hatarini kwa kufanya kile ulichoniagiza nifanye.
22 Şimdi lütfen kölenin söyleyeceğini dinle. İzin ver de, önüne biraz yemek koyayım. Yoluna devam edecek gücün olması için yemek yemelisin.”
Sasa tafadhali isikilize sauti ya mtumishi wako, uniruhusu nikupatie chakula kidogo ule ili uwe na nguvu za kurejea ulikotoka.”
23 Ama Saul, “Yemem” diyerek reddetti. Ancak hizmetkârlarıyla kadın zorlayınca, onların dediğini yaptı. Yerden kalkıp yatağın üzerine oturdu.
Akakataa, akisema, “Mimi sitaki kula.” Lakini watumishi wake wakaungana na yule mwanamke wakamsihi ale, naye akakubali. Basi akainuka hapo chini, akaketi juu ya kitanda.
24 Kadının evinde besili bir dana vardı. Kadın onu hemen kesti. Un alıp yoğurdu ve mayasız ekmek pişirdi.
Yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona hapo nyumbani, akamchinja mara moja. Akachukua unga, akaukanda, akatengeneza mkate usio chachu.
25 Sonra Saul'la görevlilerinin önüne koydu. Onlar da yediler. Sonra o gece kalkıp gittiler.
Ndipo akamwandalia meza Sauli pamoja na watu wake, nao wakala. Usiku ule ule wakainuka na kwenda zao.

< 1 Samuel 28 >