< 1 Samuel 27 >

1 Davut, “Bir gün Saul'un eliyle yok olacağım” diye düşündü, “Benim için en iyisi hemen Filist topraklarına kaçmak. O zaman Saul İsrail'in her yanında beni aramaktan vazgeçer; ben de onun elinden kurtulmuş olurum.”
Daudi akasema moyoni mwake, “Katika mojawapo ya siku hizi nitaangamizwa kwa mkono wa Sauli. Jambo lililo bora ni kutorokea kwenye nchi ya Wafilisti. Hivyo Sauli atakata tamaa ya kunisaka popote katika Israeli, nami nitakuwa nimeponyoka mkononi mwake.”
2 Böylece Davut'la yanındaki altı yüz kişi kalkıp Gat Kralı Maok oğlu Akiş'in tarafına geçtiler.
Hivyo Daudi akaondoka na hao watu mia sita waliokuwa pamoja naye na kwenda kwa Akishi mwana wa Maoki mfalme wa Gathi.
3 Aileleriyle birlikte Gat'ta Akiş'in yanına yerleştiler. İki karısı Yizreelli Ahinoam'la Karmelli Naval'ın dul karısı Avigayil de Davut'un yanındaydı.
Daudi na watu wake wakakaa huko Gathi pamoja na Akishi. Kila mtu alikuwa pamoja na jamaa yake, naye Daudi pamoja na wakeze wawili: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
4 Saul Davut'un Gat'a kaçtığını duyunca, artık onu aramaktan vazgeçti.
Sauli alipokuwa ameambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbilia Gathi, hakuendelea kumsaka tena.
5 Davut Akiş'e, “Benden hoşnut kaldıysan, çevre kentlerden birinde bana bir yer versinler de orada oturayım” dedi, “Çünkü ben kulunun seninle birlikte kral kentinde yaşamasına gerek yok.”
Ndipo Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, unipe sehemu katika mojawapo ya miji katika nchi nikae huko. Kwa nini mtumwa wako akae pamoja nawe katika mji huu wa kifalme?”
6 Akiş o gün ona Ziklak Kenti'ni verdi. Bundan ötürü Ziklak bugün de Yahuda krallarına aittir.
Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi mji wa Siklagi, nao Siklagi umekuwa mali ya wafalme wa Yuda tangu wakati huo.
7 Davut Filist topraklarında bir yıl dört ay yaşadı.
Daudi akaishi katika nchi ya Wafilisti muda wa mwaka mmoja na miezi minne.
8 Bu süre içinde Davut'la adamları gidip Geşurlular'a, Girizliler'e ve Amalekliler'e baskınlar yaptılar. Bunlar uzun zamandan beri Şur'a, hatta Mısır'a dek uzanan topraklarda yaşıyorlardı.
Basi Daudi na watu wake wakapanda na kuwashambulia Wageshuri, Wagirizi na Waamaleki. (Tangu zamani haya mataifa yalikuwa yameishi kwenye eneo lililotanda kuanzia Telemu katika njia iteremkayo Shuri hadi kufikia nchi ya Misri.)
9 Davut bir bölgeye saldırdığında kadın erkek demez, kimseyi sağ bırakmazdı; yalnız davarları, sığırları, eşekleri, develeri ve giysileri alıp Akiş'e dönerdi.
Kila mara Daudi aliposhambulia eneo, hakubakiza hai mwanaume wala mwanamke, lakini alichukua kondoo na ngʼombe, punda na ngamia, na nguo. Kisha akarudi kwa Akishi.
10 Akiş, “Bugün nerelere baskın düzenlediniz?” diye sorardı. Davut da, “Yahuda'nın güneyine, Yerahmeelliler'in ve Kenliler'in güney bölgesine saldırdık” derdi.
Akishi alipomuuliza, “Je leo umeshambulia wapi?” Daudi humjibu, “Dhidi ya Negebu ya Yuda,” au wakati mwingine husema, “Dhidi ya Negebu ya Yerameeli,” au “Dhidi ya Negebu ya Wakeni.”
11 Davut, kendisiyle Gat'a kimseyi götürmemek için kadın erkek kimseyi sağ bırakmazdı. Çünkü, “Gat'a gidip, ‘Davut şöyle yaptı, böyle yaptı’ diyerek bize karşı bilgi aktarmasınlar” diye düşünürdü. Davut, Filist topraklarında yaşadığı sürece bu yöntemi uyguladı.
Daudi hakumwacha hai mwanaume au mwanamke ili apate kuletwa Gathi, kwa maana Daudi aliwaza, “Wanaweza kujulisha habari zetu na kusema, ‘Hivi ndivyo alivyofanya Daudi.’” Hii ndiyo ilikuwa desturi yake wakati wote aliishi katika nchi ya Wafilisti.
12 Akiş Davut'a güven duymaya başladı. “Davut kendi halkı olan İsrailliler'in nefretine uğradı. Bundan böyle benim hizmetimde kalacak” diye düşünüyordu.
Akishi akamsadiki Daudi na kuwaza moyoni mwake, akasema, “Daudi amekuwa kitu cha kuchukiza kabisa kwa watu wake, Waisraeli, hivi kwamba atakuwa mtumishi wangu milele.”

< 1 Samuel 27 >