< 2 Samuel 1 >

1 Saul'un ölümünden sonra Amalekliler'e karşı kazandığı zaferden dönen Davut Ziklak'ta iki gün kaldı.
Baada ya kifo cha Sauli, Daudi alipokuwa amerudi kutoka kuwashinda Waamaleki, Daudi alikaa siku mbili huko Siklagi.
2 Üçüncü gün, Saul'un ordugahından giysileri yırtılmış, başı toz toprak içinde bir adam geldi. Adam Davut'a yaklaşınca önünde yere kapandı.
Siku ya tatu akaja mtu mwenye nguo zilizoraruka na mavumbi kichwani mwake kutoka kwenye kambi ya Sauli. Alipomjia Daudi, akajitupa chini ili kumpa heshima.
3 Davut, “Nereden geliyorsun?” diye sordu. Adam, “İsrail ordugahından kaçıp kurtuldum” dedi.
Daudi akamuuliza, “Wewe umetoka wapi?” Akamjibu, “Nimetoroka kutoka kambi ya Waisraeli.”
4 Davut, “Ne oldu? Bana anlat” dedi. Adam askerlerin savaş alanından kaçtığını, birçoğunun düşüp öldüğünü, Saul'la oğlu Yonatan'ın da ölüler arasında olduğunu anlattı.
Daudi akamuuliza, “Ni nini kilichotokea? Niambie.” Akasema, “Watu walikimbia kutoka vitani. Wengi wao walianguka na kufa. Naye Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa.”
5 Davut, kendisine haberi veren genç adama, “Saul'la oğlu Yonatan'ın öldüğünü nereden biliyorsun?” diye sordu.
Ndipo Daudi akamwambia huyo kijana aliyemletea taarifa, “Je, umefahamuje kwamba Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa?”
6 Genç adam şöyle yanıtladı: “Bir rastlantı sonucu Gilboa Dağı'ndaydım. Saul mızrağına dayanmıştı. Atlılarla savaş arabaları ona doğru yaklaşıyordu.
Yule kijana akasema, “Nilijipata huko Mlima Gilboa, naye Sauli alikuwa huko akiegemea mkuki wake, na magari ya vita na wapanda farasi wa upande wa adui wakawa wamemkaribia sana.
7 Saul arkasına dönüp beni görünce seslendi. Ben de, ‘Buyrun, buradayım’ dedim.
Alipogeuka na kuniona, akaniita, nami nikasema, ‘Je, nifanye nini?’
8 “Saul, ‘Sen kimsin?’ diye sordu. “‘Ben bir Amalekli'yim’ diye yanıtladım.
“Akaniuliza, ‘Wewe ni nani?’ “Nikamjibu, ‘Mimi ni Mwamaleki.’
9 “Saul, ‘Ne olur üstüme var ve beni öldür!’ dedi, ‘Çünkü çektiğim acılardan kurtulmak istiyorum.’
“Kisha akaniambia, ‘Nikaribie mimi na uniue! Niko katika maumivu makali ya kifo, lakini bado ningali hai.’
10 Bu yüzden varıp onu öldürdüm. Çünkü yere düştükten sonra yaşayamayacağını biliyordum. Başındaki taçla kolundaki bileziği aldım ve onları buraya, efendime getirdim.”
“Kwa hiyo nikamkaribia nikamuua, kwa sababu nilijua kwamba baada ya kuanguka hangeweza kupona. Nami nikachukua lile taji lililokuwa kichwani mwake na utepe uliokuwa mkononi mwake nami nimevileta hapa kwa bwana wangu.”
11 Bunun üzerine Davut'la yanındakiler giysilerini yırttılar.
Ndipo Daudi pamoja na watu wote waliokuwa pamoja naye wakazishika nguo zao na kuzirarua.
12 Kılıçtan geçirilen Saul, oğlu Yonatan ve RAB'bin halkı olan İsrailliler için akşama dek yas tutup ağladılar, oruç tuttular.
Wakaomboleza, wakalia pia na kufunga mpaka jioni kwa ajili ya Sauli na Yonathani mwanawe, kwa ajili ya jeshi la Bwana na nyumba ya Israeli, kwa sababu wameanguka kwa upanga.
13 Davut, kendisine haber getiren genç adama, “Nerelisin?” diye sordu. Adam, “Ben yabancıyım, bir Amalekli'nin oğluyum” dedi.
Daudi akamwambia yule kijana aliyemletea taarifa, “Wewe ni mwenyeji wa wapi?” Akamjibu, “Mimi ni mwana wa mgeni, Mwamaleki.”
14 Davut, “RAB'bin meshettiği kişiye el kaldırıp onu yok etmekten korkmadın mı?” diye sordu.
Daudi akamuuliza, “Kwa nini hukuogopa kuinua mkono wako ili kumwangamiza mpakwa mafuta wa Bwana?”
15 Sonra adamlarından birini çağırıp, “Git, öldür onu!” diye buyurdu. Böylece adam Amalekli'yi vurup öldürdü.
Kisha Daudi akamwita mmoja wa watu wake na kumwambia, “Nenda ukamuue!” Kwa hiyo akampiga, naye akafa.
16 Davut Amalekli'ye, “Kanından sen kendin sorumlusun” demişti, “Çünkü ‘RAB'bin meshettiği kişiyi ben öldürdüm’ demekle kendine karşı ağzınla tanıklıkta bulundun.”
Kwa maana Daudi alikuwa amemwambia, “Damu yako iwe juu ya kichwa chako mwenyewe. Kinywa chako mwenyewe kimeshuhudia dhidi yako uliposema, ‘Nilimuua mpakwa mafuta wa Bwana.’”
17 Davut Saul'la oğlu Yonatan için ağıt yaktı.
Daudi akafanya maombolezo haya kuhusu Sauli na Yonathani mwanawe,
18 Sonra Yaşar Kitabı'nda yazılan Yay adındaki ağıtın Yahuda halkına öğretilmesini buyurdu:
naye akaagiza kwamba watu wa Yuda wafundishwe ombolezo hili la upinde (ambalo limeandikwa katika Kitabu cha Yashari):
19 “Ey İsrail, senin yüceliğin yüksek tepelerinde yok oldu! Güçlüler nasıl da yere serildi!
“Walio fahari yako, ee Israeli, wameuawa juu ya mahali pako palipoinuka. Jinsi wenye nguvu walivyoanguka!
20 Haberi ne Gat'a duyurun, Ne de Aşkelon sokaklarında yayın. Öyle ki, ne Filistliler'in kızları sevinsin, Ne de sünnetsizlerin kızları coşsun.
“Msilisimulie hili katika Gathi, msilitangaze hili katika barabara za Ashkeloni, binti za Wafilisti wasije wakafurahia, binti za hao wasiotahiriwa wasije wakashangilia.
21 Ey Gilboa dağları, Üzerinize ne çiy ne de yağmur düşsün. Ürün veren tarlalarınız olmasın. Çünkü güçlünün kalkanı, Bir daha yağ sürülmeyecek olan Saul'un kalkanı Orada bir yana atıldı!
“Enyi milima ya Gilboa, msipate umande wala mvua, wala mashamba yazaayo sadaka ya nafaka. Kwa maana huko ndiko ngao ya mwenye nguvu iliponajisiwa, ngao ya Sauli haitapakwa tena mafuta.
22 Yonatan'ın yayı yere serilmişlerin kanından, Yiğitlerin bedenlerinden hiç geri çekilmedi. Saul'un kılıcı hiç boşa savrulmadı.
Kutokana na damu ya waliouawa, kutokana na miili ya wenye nguvu, ule upinde wa Yonathani haukugeuka nyuma. Upanga wa Sauli haukurudi bure.
23 Saul'la Yonatan tatlı ve sevimliydiler, Yaşamda da ölümde de ayrılmadılar. Kartallardan daha çevik, Aslanlardan daha güçlüydüler.
“Sauli na Yonathani, maishani walipendwa na kuneemeka, na katika kifo hawakutengana. Walikuwa wepesi kuliko tai, walikuwa na nguvu kuliko simba.
24 Ey İsrail kızları! Sizi al renkli, süslü giysilerle donatan, Giysinizi altın süslerle bezeyen Saul için ağlayın!
“Enyi binti za Israeli, lieni kwa ajili ya Sauli, ambaye aliwavika nguo nyekundu na maridadi, ambaye aliremba mavazi yenu kwa mapambo ya dhahabu.
25 Güçlüler nasıl da yere serildi savaşta! Yonatan senin yüksek tepelerinde ölü yatıyor.
“Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka vitani! Yonathani ameuawa mahali pako palipoinuka.
26 Senin için üzgünüm, kardeşim Yonatan. Benim için çok değerliydin. Sevgin kadın sevgisinden daha üstündü.
Nahuzunika kwa ajili yako, Yonathani ndugu yangu, kwangu ulikuwa mpendwa sana. Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, wa ajabu zaidi kuliko ule wa wanawake.
27 Güçlüler nasıl da yere serildi! Savaş silahları yok oldu!”
“Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka! Silaha za vita zimeangamia!”

< 2 Samuel 1 >