< 1 Samuel 30 >

1 Davut'la adamları üçüncü gün Ziklak Kenti'ne vardılar. Bu arada Amalekliler Negev bölgesiyle Ziklak'a baskın yapmış, Ziklak Kenti'ni yakıp yıkmışlardı.
Daudi na watu wake wakafika Siklagi siku ya tatu. Basi Waamaleki walikuwa wamevamia Negebu na Siklagi. Wakawa wameshambulia mji wa Siklagi na kuuteketeza kwa moto,
2 Kimseyi öldürmemişlerdi, ama kadınlarla orada yaşayan genç, yaşlı herkesi tutsak etmişlerdi. Sonra onları da yanlarına alıp yollarına gitmişlerdi.
nao wakawa wamewachukua mateka wanawake pamoja na wote waliokuwamo humo, vijana na wazee. Hawakuua yeyote, bali waliwachukua wakaenda zao.
3 Davut'la adamları oraya varınca kentin ateşe verildiğini, karılarının, oğullarının, kızlarının tutsak alındığını anladılar.
Daudi na watu wake walipofika Siklagi, wakakuta mji umeangamizwa kwa moto na wake zao pamoja na wana wao na binti zao wamechukuliwa mateka.
4 Güçleri tükeninceye dek hıçkıra hıçkıra ağladılar.
Hivyo Daudi na watu wake wakapiga yowe mpaka wakaishiwa na nguvu za kulia.
5 Davut'un iki karısı, Yizreelli Ahinoam ile Karmelli Naval'ın dulu Avigayil de tutsak edilmişti.
Wake wawili wa Daudi walikuwa wametekwa: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
6 Davut büyük sıkıntı içindeydi. Çünkü herkes oğulları, kızları için acı çekiyor ve, “Davut'u taşlayalım” diyordu. Ama Davut, Tanrısı RAB'de güç bularak,
Daudi alihuzunika sana kwa sababu watu walikuwa wakisemezana juu ya kumpiga kwa mawe. Kila mmoja alikuwa na uchungu rohoni kwa sababu ya wanawe na binti zake. Lakini Daudi akajitia nguvu katika Bwana, Mungu wake.
7 Ahimelek oğlu Kâhin Aviyatar'a, “Bana efodu getir” dedi. Aviyatar efodu getirdi.
Kisha Daudi akamwambia kuhani Abiathari mwana wa Ahimeleki, “Niletee kisibau.” Abiathari akamletea,
8 Davut RAB'be danışarak, “Bu akıncıların ardına düşersem, onlara yetişir miyim?” diye sordu. RAB, “Artlarına düş, kesinlikle onlara yetişip tutsakları kurtaracaksın” diye yanıtladı.
naye Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nifuatie kundi hili la wavamizi? Je, nitawapata?” Bwana akajibu, “Wafuatie. Hakika utawapata na utafanikiwa kuwaokoa.”
9 Bunun üzerine Davut yanındaki altı yüz kişiyle yola çıktı. Besor Vadisi'ne geldiler. Vadiyi geçemeyecek kadar bitkin düşen iki yüz kişi orada kaldı. Davut dört yüz kişiyle akıncıları kovalamayı sürdürdü.
Daudi pamoja na watu wake 600 wakafika kwenye Bonde la Besori, mahali ambapo wengine waliachwa nyuma,
kwa kuwa watu 200 walikuwa wamechoka sana kuweza kuvuka hilo bonde. Lakini Daudi pamoja na watu 400 wakaendelea kufuatia.
11 Kırda bir Mısırlı bulup Davut'a getirdiler. Yiyip içmesi için ona yiyecek, içecek verdiler.
Wakamkuta Mmisri katika shamba fulani, nao wakamleta kwa Daudi. Wakampa huyo Mmisri maji ya kunywa na chakula;
12 Bir parça incir pestili ile iki salkım kuru üzüm de verdiler. Adam yiyince canlandı. Üç gün üç gecedir yiyip içmemişti.
kipande cha andazi la tini na andazi la zabibu zilizokaushwa. Akala naye akapata nguvu, kwa kuwa hakuwa amekula chakula chochote wala kunywa maji kwa siku tatu usiku na mchana.
13 Davut ona, “Kime bağlısın? Nerelisin?” diye sordu. Genç adam, “Mısırlı'yım, bir Amalekli'nin kölesiyim” diye yanıtladı, “Üç gün önce hastalanınca, efendim beni bıraktı.
Daudi akamuuliza, “Wewe ni wa nani, na umetoka wapi?” Akajibu, “Mimi ni Mmisri, mtumwa wa Mwamaleki. Bwana wangu alinitelekeza nilipougua siku tatu zilizopita.
14 Keretliler'in güney sınırlarına, Yahuda topraklarına, Kalev'in güneyine baskınlar düzenlemiş, Ziklak Kenti'ni de ateşe vermiştik.”
Tulivamia Negebu ya Wakerethi, na nchi ya Yuda, na Negebu ya Kalebu. Nasi tulichoma moto Siklagi.”
15 Davut, “Beni bu akıncılara götürebilir misin?” diye sordu. Mısırlı genç, “Beni öldürmeyeceğine ya da efendimin eline teslim etmeyeceğine dair Tanrı'nın önünde ant içersen, seni akıncıların olduğu yere götürürüm” diye karşılık verdi.
Daudi akamuuliza, “Je, unaweza kuniongoza kufikia kundi hili la uvamizi?” Akajibu, “Niapie mbele ya Mungu kwamba hutaniua wala kunikabidhi mikononi mwa bwana wangu, nami nitakupeleka hadi waliko.”
16 Böylece Mısırlı Davut'u götürdü. Akıncılar dört bir yana dağılmışlardı. Filist ve Yahuda topraklarından topladıkları büyük yağmadan yiyip içiyor, eğlenip oynuyorlardı.
Akamwongoza Daudi mpaka mahali walipokuwa, nao walikuwa wametawanyika eneo lote, wakila, wakinywa na wakifanya karamu kwa sababu ya nyara nyingi walizochukua kutoka nchi ya Wafilisti na kutoka Yuda.
17 Davut ertesi gün tan vaktinden akşama dek onları öldürdü. Develere binip kaçan dört yüz genç dışında içlerinden kurtulan olmadı.
Daudi akapigana nao kuanzia machweo ya jua hadi kesho yake jioni, na hakuna yeyote miongoni mwao aliyetoroka, isipokuwa vijana wanaume 400 waliopanda ngamia na kutoroka.
18 Davut Amalekliler'in ele geçirdiği her şeyi, bu arada da iki karısını kurtardı.
Daudi akarudisha kila kitu Waamaleki walikuwa wamechukua, pamoja na wake zake wawili.
19 Gençler, yaşlılar, oğullar, kızlar, yağmalanan mallar, kısacası Amalekliler'in aldıklarından hiçbir şey eksik kalmadı. Davut tümünü geri aldı.
Hakuna chochote kilichopotea: kijana au mzee, mvulana au msichana, nyara au kitu kingine chochote walichokuwa wamechukua. Daudi akarudisha kila kitu.
20 Bütün koyunlarla sığırları da aldı. Adamları, bunları öbür hayvanların önünden sürerek, “Bunlar Davut'un yağmaladıkları” diyorlardı.
Akachukua makundi yote ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, nao watu wake wakawaswaga wanyama hao mbele ya wanyama wengine wa kufugwa, wakisema, “Hizi ni nyara za Daudi.”
21 Bundan sonra Davut, daha ileriye gidemeyecek kadar bitkin düşüp Besor Vadisi'nde kalan iki yüz kişinin bulunduğu yere vardı. Onlar da Davut'la yanındakileri karşılamaya çıktılar. Davut yaklaşınca onlara esenlik diledi.
Kisha Daudi akafika kwa wale watu 200 waliokuwa wamechoka sana kumfuata na ambao waliachwa nyuma kwenye Bonde la Besori. Wakatoka kwenda kumlaki Daudi na wale watu aliokuwa nao. Daudi na watu wake walipowakaribia, akawasalimu.
22 Ama Davut'la giden adamlardan kötü ve değersiz olanların tümü, “Madem bizimle birlikte gitmediler, geri aldığımız yağmadan onlara hiçbir pay vermeyeceğiz” dediler, “Her biri yalnız karısıyla çocuklarını alıp gitsin.”
Lakini watu wote waovu na wakorofi miongoni mwa wafuasi wa Daudi wakasema, “Kwa sababu hawakwenda pamoja nasi, hatutagawana nao nyara tulizorudisha. Lakini, kila mtu aweza kuchukua mkewe na watoto wake na kuondoka.”
23 Ama Davut, “Hayır, kardeşlerim!” dedi, “RAB'bin bize verdikleri konusunda böyle davranamayız! O bizi korudu ve bize saldıran akıncıları elimize teslim etti.
Daudi akajibu, “La hasha, ndugu zangu, kamwe hamwezi kufanya hivyo kwa kile ambacho Bwana ametupatia. Yeye ametulinda na kuweka mikononi mwetu majeshi yale yaliyokuja kupigana dhidi yetu.
24 Sizin bu söylediklerinizi kim kabul eder? Savaşa gidenle eşyanın yanında kalanın payı aynıdır. Her şey eşit paylaşılacak!”
Ni nani atasikiliza yale mnayosema? Fungu la mtu aliyekaa na vyombo litakuwa sawa na la yule aliyekwenda vitani. Wote watashiriki sawa.”
25 O günden sonra Davut bunu İsrail için bugüne dek geçerli bir kural ve ilke haline getirdi.
Daudi akafanya hili liwe amri na agizo kwa Israeli kutoka siku ile hata leo.
26 Davut Ziklak'a dönünce, dostları olan Yahuda ileri gelenlerine yağma mallardan göndererek, “İşte RAB'bin düşmanlarından yağmalanan mallardan size bir armağan” dedi.
Daudi alipofika Siklagi, akatuma baadhi ya nyara kwa wazee wa Yuda, waliokuwa rafiki zake, akasema, “Tazama, hapa kuna zawadi kwa ajili yenu kutoka nyara za adui za Bwana.”
27 Sonra Beytel, Negev'deki Ramot, Yattir,
Akazituma kwa wale waliokuwa Betheli, Ramoth-Negebu na Yatiri;
28 Aroer, Sifmot, Eştemoa,
kwa wale walioko Aroeri, Sifmothi, Eshtemoa
29 Rakal, Yerahmeelliler'in, Kenliler'in kentlerinde,
na Rakali; kwa wale waliokuwa katika miji ya Wayerameeli na ya Wakeni;
30 Horma, Bor-Aşan, Atak,
na kwa wale walioko Horma, Bori-Ashani, Athaki,
31 Hevron'da oturanlara ve adamlarıyla birlikte sık sık uğradığı yerlerin tümüne yağmalanan mallardan gönderdi.
na kwa wakazi wa Hebroni; na kwa wale waliokuwa mahali pengine pote ambako Daudi na watu wake walitembelea.

< 1 Samuel 30 >