< Zaburi 36 >

1 Dhambi hunena kama unabii katika moyo wa mwovu; machoni mwake hamna hofu ya Mungu.
For the Leader. A Psalm of David the servant of the LORD. Transgression speaketh to the wicked, methinks — there is no fear of God before his eyes.
2 Kwa maana yeye hujifariji mwenyewe, akifikiria kuwa dhambi zake hazitagundulika na kuchukiwa.
For it flattereth him in his eyes, until his iniquity be found, and he be hated.
3 Maneno yake ni yenye dhambi na udanganyifu; hataki kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
The words of his mouth are iniquity and deceit; he hath left off to be wise, to do good.
4 Alalapo kitandani, hupanga namna ya kutenda dhambi; yeye hukaa nje kwenye nja ya uovu; yeye hakatai uovu.
He deviseth iniquity upon his bed; he setteth himself in a way that is not good; he abhorreth not evil.
5 Uaminifu wa agano lako, Yahwe, unafika mbinguni; uaminifu wako unafika mawinguni.
Thy lovingkindness, O LORD, is in the heavens; Thy faithfulness reacheth unto the skies.
6 Haki yako ni kama milima ya Mungu; hukumu yako ni kama kina kirefu. Yahwe, wewe huwahifadhi wote wanadamu na wanyama.
Thy righteousness is like the mighty mountains; Thy judgments are like the great deep; man and beast Thou preservest, O LORD.
7 Ni jinsi gani uaminifu wa aganao lako ni wa thamani, Mungu! Watu hukimbilia usalama chini ya uvuli wa mbawa zako.
How precious is Thy lovingkindness, O God! and the children of men take refuge in the shadow of Thy wings.
8 Nao watatoshelezwa tele na utajiri wa chakula nyumbani mwako; utawafanya wanywe kutoka katika mto wa baraka zako za thamani.
They are abundantly satisfied with the fatness of Thy house; and Thou makest them drink of the river of Thy pleasures.
9 Kwa kuwa mna chemichemi ya uzima; na katika mwanga wako tutaiona nuru.
For with Thee is the fountain of life; in Thy light do we see light.
10 Uupanue uaminifu wa agano lako kikamilifu kwa wale wanao kujua wewe, ulinzi wako uwe juu ya wanyoofu wa moyo.
O continue Thy lovingkindness unto them that know Thee; and Thy righteousness to the upright in heart.
11 Usiuache mguu wa mwenye kiburi unisogelee. Usiiache mkono wa mwovu unitoweshe.
Let not the foot of pride overtake me, and let not the hand of the wicked drive me away.
12 Kule wafanyao maovu wameanguka; wameharibiwa hawawezi kuinuka.
There are the workers of iniquity fallen; they are thrust down, and are not able to rise.

< Zaburi 36 >