< Zaburi 48 >

1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
A Song; a Psalm of the sons of Korah. Great is the LORD, and highly to be praised, in the city of our God, His holy mountain,
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
Fair in situation, the joy of the whole earth; even mount Zion, the uttermost parts of the north, the city of the great King.
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
God in her palaces hath made Himself known for a stronghold.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
For, lo, the kings assembled themselves, they came onward together.
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
They saw, straightway they were amazed; they were affrighted, they hasted away.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
Trembling took hold of them there, pangs, as of a woman in travail.
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
With the east wind Thou breakest the ships of Tarshish.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
As we have heard, so have we seen in the city of the LORD of hosts, in the city of our God — God establish it for ever. (Selah)
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
We have thought on Thy lovingkindness, O God, in the midst of Thy temple.
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
As is Thy name, O God, so is Thy praise unto the ends of the earth; Thy right hand is full of righteousness.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
Let mount Zion be glad, let the daughters of Judah rejoice, because of Thy judgments.
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
Walk about Zion, and go round about her; count the towers thereof.
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
Mark ye well her ramparts, traverse her palaces; that ye may tell it to the generation following.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
For such is God, our God, for ever and ever; He will guide us eternally.

< Zaburi 48 >