< Zaburi 22 >

1 Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
For the Leader; upon Aijeleth ha-Shahar. A Psalm of David. My God, my God, why hast Thou forsaken me, and art far from my help at the words of my cry?
2 Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
O my God, I call by day, but Thou answerest not; and at night, and there is no surcease for me.
3 Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
Yet Thou art holy, O Thou that art enthroned upon the praises of Israel.
4 Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
In Thee did our fathers trust; they trusted, and Thou didst deliver them.
5 Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
Unto Thee they cried, and escaped; in Thee did they trust, and were not ashamed.
6 Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
But I am a worm, and no man; a reproach of men, and despised of the people.
7 Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
All they that see me laugh me to scorn; they shoot out the lip, they shake the head:
8 Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
'Let him commit himself unto the LORD! let Him rescue him; let Him deliver him, seeing He delighteth in him.'
9 Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
For Thou art He that took me out of the womb; Thou madest me trust when I was upon my mother's breasts.
10 Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
Upon Thee I have been cast from my birth; Thou art my God from my mother's womb.
11 Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
Be not far from me; for trouble is near; for there is none to help.
12 Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
Many bulls have encompassed me; strong bulls of Bashan have beset me round.
13 Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
They open wide their mouth against me, as a ravening and a roaring lion.
14 Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
I am poured out like water, and all my bones are out of joint; my heart is become like wax; it is melted in mine inmost parts.
15 Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
My strength is dried up like a potsherd; and my tongue cleaveth to my throat; and Thou layest me in the dust of death.
16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
For dogs have encompassed me; a company of evil-doers have inclosed me; like a lion, they are at my hands and my feet.
17 Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
I may count all my bones; they look and gloat over me.
18 Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
They part my garments among them, and for my vesture do they cast lots.
19 Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
But Thou, O LORD, be not far off; O Thou my strength, hasten to help me.
20 Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
Deliver my soul from the sword; mine only one from the power of the dog.
21 Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
Save me from the lion's mouth; yea, from the horns of the wild-oxen do Thou answer me.
22 Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
I will declare Thy name unto my brethren; in the midst of the congregation will I praise Thee.
23 Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
'Ye that fear the LORD, praise Him; all ye the seed of Jacob, glorify Him; and stand in awe of Him, all ye the seed of Israel.
24 Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
For He hath not despised nor abhorred the lowliness of the poor; neither hath He hid His face from him; but when he cried unto Him, He heard.'
25 Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
From Thee cometh my praise in the great congregation; I will pay my vows before them that fear Him.
26 Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
Let the humble eat and be satisfied; let them praise the LORD that seek after Him; may your heart be quickened for ever!
27 Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
All the ends of the earth shall remember and turn unto the LORD; and all the kindreds of the nations shall worship before Thee.
28 Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
For the kingdom is the LORD'S; and He is the ruler over the nations.
29 Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
All the fat ones of the earth shall eat and worship; all they that go down to the dust shall kneel before Him, even he that cannot keep his soul alive.
30 Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
A seed shall serve him; it shall be told of the Lord unto the next generation.
31 Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!
They shall come and shall declare His righteousness unto a people that shall be born, that He hath done it.

< Zaburi 22 >