< Yohana 4 >

1 Basi Yesu alipofahamu kuwa Mafarisayo wamesikia kuwa Yesu alikuwa anafuasa na kuwabatiza zaidi ya Yohana,
Le Seigneur, sachant que les pharisiens avaient appris que Jésus faisait et baptisait plus de disciples que Jean
2 (ingawa Yesu mwenyewe alikuwa habatizi ila wanafunzi wake),
(bien que Jésus lui-même ne baptisât pas, mais ses disciples),
3 alitoka Judea na akaenda Galilaya.
quitta la Judée et se rendit en Galilée.
4 Hivyo ilikuwa muhimu kupitia Samaria.
Il lui fallait passer par la Samarie.
5 Na akafika kwenye mji wa Samaria, unaoitwa Sikari, karibu na eneo ambalo Yakobo alimpa mwanae Yusufu.
Il arriva donc dans une ville de Samarie appelée Sychar, près de la parcelle de terre que Jacob avait donnée à son fils Joseph.
6 Na kisima cha Yakobo kilikuwa hapo. Yesu alikuwa amechoka kwa ajili ya safari na akakaa karibu na kisima. Ilikuwa muda wa mchana.
Le puits de Jacob était là. Jésus, fatigué de son voyage, s'assit donc près du puits. C'était environ la sixième heure.
7 Mwanamke Msamaria alikuja kuteka maji, na Yesu akamwambia, “Nipe maji ninywe.”
Une femme de Samarie vint puiser de l'eau. Jésus lui dit: « Donne-moi à boire. »
8 Kwa sababu wanafunzi wake walikuwa wameenda zao mjini kununua chakula.
Car ses disciples étaient partis à la ville pour acheter des vivres.
9 Yule mwanamke akamwambia, “Inakuaje wewe Myahudi, kuniomba mimi mwanamke Msamaria, kitu cha kunywa?” Kwa sababu Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.
La Samaritaine lui dit donc: « Comment se fait-il que toi, qui es Juif, tu demandes à boire à moi, une Samaritaine? ». (Car les Juifs n'ont pas affaire aux Samaritains).
10 Yesu akamjibu, “Kama ungelijua karama ya Mungu, na yule anayekuambia 'Nipe maji, ' ungelimwomba, na angelikupa maji ya uzima.”
Jésus lui répondit: « Si tu savais quel est le don de Dieu, et qui est celui qui te dit: « Donne-moi à boire », tu lui aurais demandé, et il t'aurait donné de l'eau vive. »
11 Mwanamke akajibu, “Bwana hauna ndoo ya kuchotea, na kisima ni kirefu. Utayapata wapi Maji ya Uzima?
La femme lui dit: « Monsieur, vous n'avez rien pour puiser, et le puits est profond. Où vas-tu puiser cette eau vive?
12 Je wewe ni mkuu, kuliko baba yetu Yakobo, ambaye alitupa kisima hiki, na yeye mwenyewe na watoto wake pamoja na mifugo yake wakanywa maji ya kisima hiki?”
Es-tu plus grand que notre père Jacob, qui nous a donné le puits et y a bu lui-même, ainsi que ses enfants et son bétail? »
13 Yesu akajibu, “Yeyote anywae maji haya atapata kiu tena,
Jésus lui répondit: « Quiconque boit de cette eau aura encore soif,
14 lakini yeye atakaye kunywa maji nitakayompa hatapata kiu tena. Badala yake maji nitakayompa yatakuwa chemchemi inayobubujika hata milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
mais celui qui boira de l'eau que je lui donnerai n'aura plus jamais soif; l'eau que je lui donnerai deviendra en lui une source d'eau jaillissant en vie éternelle. » (aiōn g165, aiōnios g166)
15 Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, nayaomba maji hayo ili nisipate kiu, na nisihangaike kuja hapa kuchota maji.”
La femme lui dit: « Seigneur, donne-moi cette eau, afin que je n'aie pas soif et que je ne vienne pas jusqu'ici pour puiser. »
16 Yesu akamwambia, “Nenda kamwite mumeo, kisha urudi.”
Jésus lui dit: « Va, appelle ton mari, et viens ici. »
17 Mwanamke akamwambia, “Sina mume.” Yesu akajibu, “Umesema vyema, 'Sina mume;'
La femme répondit: « Je n'ai pas de mari. » Jésus lui dit: « Tu as bien dit: « Je n'ai pas de mari »,
18 kwa maana umekuwa na wanaume watano, na mmoja ambaye unaye sasa sio mume wako. Katika hili umesema kweli!”
car tu as eu cinq maris, et celui que tu as maintenant n'est pas ton mari. Tu l'as dit en vérité. »
19 Mwanamke akamwambia, “Bwana naona yakuwa wewe ni nabii.
La femme lui dit: « Monsieur, je vois que vous êtes un prophète.
20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu. Lakini ninyi mwasema ya kuwa Yerusalemu ndiyo sehemu ambayo watu wanapaswa kuabudu.”
Nos pères se sont prosternés sur cette montagne, et vous, les Juifs, vous dites que le lieu où l'on doit se prosterner est à Jérusalem. »
21 Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu au Yerusalemu.
Jésus lui dit: « Femme, crois-moi, l'heure vient où ce n'est ni sur cette montagne ni à Jérusalem que vous adorerez le Père.
22 Ninyi watu mwaabudu kile msichokijua, lakini sisi twaabudu tunachokijua, kwa sababu wokovu watoka kwa Wayahudi.”
Vous adorez ce que vous ne connaissez pas. Nous adorons ce que nous connaissons, car le salut vient des Juifs.
23 Hatahivyo, wakati unakuja, na sasa upo hapa, wakati waabuduo kweli watamwabudu Baba katika roho na kweli, kwa sababu Baba anawatafuta watu wa namna hiyo kuwa watu wake wanao mwabudu.
Mais l'heure vient, et c'est maintenant, où les vrais adorateurs adoreront le Père en esprit et en vérité, car le Père cherche de tels adorateurs.
24 Mungu ni Roho, na wale wanaomwabudu wanapaswa kumwabudu kwa roho na kweli.”
Dieu est esprit, et ceux qui l'adorent doivent adorer en esprit et en vérité. »
25 Mwanamke akamwambia, “Ninajua kuwa Masihi anakuja, (aitwaye Kristo). Huyo atakapokuja atatwambia yote.”
La femme lui dit: « Je sais que le Messie va venir, celui qu'on appelle Christ. Quand il sera venu, il nous annoncera toutes choses. »
26 Yesu akamwambia, “Mimi unayesema nami ndiye.”
Jésus lui dit: « C'est moi, celui qui te parle. »
27 Wakati huo huo wanafunzi wake wakarudi. Nao walishangaa kwa nini alikuwa akizungumza na mwanamke, lakini hakuna aliyethubutu kumuuliza, “Unataka nini?” au “Kwa nini unazungumza naye?”
A l'instant même, ses disciples arrivèrent. Ils s'étonnaient de ce qu'il parlait à une femme; pourtant, personne ne disait: « Que cherchez-vous? » ou « Pourquoi parlez-vous avec elle? »
28 Hivyo mwanamke akauacha mtungi wake na akaenda mjini na akawambia watu,
La femme laissa donc son pot à eau, s'en alla dans la ville et dit aux gens:
29 “Njooni mwone mtu aliyeniambia mambo yangu yote niliyoyatenda, je yawezekana akawa ndiye Kristo?”
« Venez voir un homme qui m'a raconté tout ce que j'ai fait. Est-ce là le Christ? »
30 Wakatoka mjini wakaja kwake.
Ils sortirent de la ville, et s'approchèrent de lui.
31 Wakati wa mchana wanafunzi wake walimsihi wakisema, “Rabi kula chakula.”
Pendant ce temps, les disciples le pressaient en disant: « Rabbi, mange. »
32 lakini yeye aliwambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
Mais il leur dit: « J'ai un repas à manger que vous ne connaissez pas. »
33 Wanafunzi wakaambizana, hakuna aliyemletea kitu chochotekula,”Je walileta?”
Les disciples se dirent donc les uns aux autres: « Quelqu'un lui a-t-il apporté quelque chose à manger? »
34 Yesu akawambia, “Chakula changu ni kufanya mapenzi yake yeye aliyenituma na kutimiza kazi yake.
Jésus leur dit: « Ma nourriture est de faire la volonté de celui qui m'a envoyé et d'accomplir son œuvre.
35 Je, hamsemi, 'Bado miezi mitano na mavuno yatakuwa tayari?' Ninawambieni tazameni mashamba yalivyo tayari kwa mavuno!
Ne dites-vous pas: « Il y a encore quatre mois avant la moisson? Voici, je vous le dis, levez les yeux et regardez les champs: ils sont déjà blancs pour la moisson.
36 Yeye avunaye hupokea mishahara na kukusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele, ili kwamba yeye apandaye naye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios g166)
Celui qui moissonne reçoit un salaire et recueille du fruit pour la vie éternelle, afin que celui qui sème et celui qui moissonne se réjouissent ensemble. (aiōnios g166)
37 Kwa kuwa msemo huu ni wa kweli, 'Mmoja apanda na mwingine avuna.'
Car cette parole est vraie: « L'un sème, l'autre moissonne ».
38 Niliwatuma kuvuna ambacho hamkukihangaikia, Wengine wamefanya kazi na ninyi mmeingia katika furaha ya kazi yao.”
Je vous ai envoyés pour moissonner ce que vous n'avez pas travaillé. D'autres ont travaillé, et vous avez participé à leur travail. »
39 Wasamaria wengi katika mji ule walimwani kwa sababu ya taarifa ya yule mwanamke aliyekuwa akishuhudia, “Aliyeniambia mambo yote niliyoyafanya.”
De cette ville, beaucoup de Samaritains crurent en lui, à cause de la parole de la femme, qui témoigna:" Il m'a dit tout ce que j'ai fait. »
40 Hivyo Wasamaria walipokuja walimsihi akae pamoja nao na akakaa kwao kwa siku mbili.
Les Samaritains vinrent donc le trouver et le prièrent de rester avec eux. Il resta là deux jours.
41 Na wengi zaidi wakamwamini kwa sababu ya neno lake.
Beaucoup d'autres crurent à cause de sa parole.
42 Wakamwambia yule mwanamke, “Tunaamini sio tu kwa maneno yako, kwa sababu sisi wenyewe tumesikia, na sasa twafahamu kuwa hakika yeye ni mwokozi wa ulimwengu.”
Ils dirent à la femme: « Maintenant, nous croyons, non pas à cause de ce que tu as dit, mais parce que nous l'avons entendu nous-mêmes, et nous savons que c'est vraiment le Christ, le Sauveur du monde. »
43 Baada ya siku hizo mbili, akaondoka na kuelekea Galilaya.
Après ces deux jours, il partit de là et se rendit en Galilée.
44 Kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa ametangaza kuwa nabii hana heshima katika nchi yake mwenyewe.
Car Jésus lui-même a témoigné qu'un prophète n'a pas d'honneur dans sa propre patrie.
45 Alipokuja kutoka Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha. Walikuwa wameona mambo yote aliyoyafanya Yerusalemu kwenye sikukuu, kwa sababu na wao pia walikuwa wamehudhuria kwenye sikukuu.
Lorsqu'il arriva en Galilée, les Galiléens le reçurent, après avoir vu tout ce qu'il faisait à Jérusalem pendant la fête, car eux aussi allaient à la fête.
46 Alikuja tena Kana ya Galilaya huko alikoyabadilisha maji kuwa divai. Palikuwa na ofisa ambaye mwana wake alikuwa ni mgonjwa huko Kapernaumu.
Jésus revint donc à Cana de Galilée, où il changea l'eau en vin. Il y avait à Capharnaüm un gentilhomme dont le fils était malade.
47 Aliposikia kuwa Yesu alitoka Judea na kwenda Galilaya, alienda kwa Yesu na kumsihi atelemke amponye mwanawe, ambaye alikuwa karibu kufa.
Ayant appris que Jésus était passé de la Judée à la Galilée, il alla le trouver et le pria de descendre et de guérir son fils, car il était à l'article de la mort.
48 Ndipo Yesu akamwambia, “Ninyi msipoona ishara na maajabu hamwezi kuamini.
Jésus lui dit alors: « Si vous ne voyez des signes et des prodiges, vous ne croirez en aucune façon. »
49 Kiongozi akasema, “Bwana shuka chini kabla mwanangu hajafa.”
Le noble lui dit: « Monsieur, descendez avant que mon enfant ne meure. »
50 Yesu akamwambia, “Nenda mwanao ni mzima.” Yule mtu akaamini neno alilolisema Yesu na akaenda zake.
Jésus lui dit: « Va-t'en. Ton fils est vivant. » L'homme crut à la parole que Jésus lui avait dite, et il s'en alla.
51 Alipokuwa akishuka, watumishi wake walimpokea na kumwambia mwana wake alikuwa mzima.
Comme il descendait, ses serviteurs vinrent à sa rencontre et lui rapportèrent: « Ton enfant vit! »
52 Hivyo akawauliza ni muda gani alipata nafuu. Wakajibu, “Jana muda wa saa saba homa ilipomwacha.”
Il s'enquit donc auprès d'eux de l'heure à laquelle il commença à aller mieux. Ils lui dirent donc: « Hier, à la septième heure, la fièvre l'a quitté. »
53 Ndipo baba yake akatambua kuwa ni muda ule ule Yesu aliosema, “Mwana wako ni mzima.” Hivyo yeye na familia yake wakaamini.
Le père sut donc que c'était à cette heure-là que Jésus lui avait dit: « Ton fils vit. » Il crut, ainsi que toute sa maison.
54 Hii ilikuwa ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipotoka Yudea kwenda Galilaya.
Voici encore le second signe que fit Jésus, après être passé de la Judée en Galilée.

< Yohana 4 >