< Luka 1 >

1 Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
Puisque plusieurs ont entrepris de mettre en ordre le récit des événements qui se sont accomplis parmi nous,
2 kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
comme nous l'ont transmis ceux qui, dès le début, ont été témoins oculaires et serviteurs de la parole,
3 Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
il m'a semblé bon, ayant dès le début suivi exactement le cours de toutes choses, de t'écrire avec ordre, très excellent Théophile,
4 Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
afin que tu saches avec certitude les choses dans lesquelles tu as été instruit.
5 Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
Il y avait, du temps d'Hérode, roi de Judée, un prêtre nommé Zacharie, de la division sacerdotale d'Abija. Il avait une femme parmi les filles d'Aaron, et son nom était Élisabeth.
6 Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
Ils étaient tous deux justes devant Dieu, marchant sans reproche dans tous les commandements et ordonnances du Seigneur.
7 Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
Mais ils n'eurent pas d'enfant, car Élisabeth était stérile, et ils étaient tous deux avancés en âge.
8 Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
Or, tandis qu'il exerçait la fonction de prêtre devant Dieu selon l'ordre de sa division,
9 Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
selon la coutume de la fonction de prêtre, son lot était d'entrer dans le temple du Seigneur et d'y brûler des parfums.
10 Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
Toute la multitude du peuple priait dehors à l'heure de l'encens.
11 Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
Un ange du Seigneur lui apparut, se tenant à droite de l'autel des parfums.
12 Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
Zacharie fut troublé en le voyant, et la peur le saisit.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
Mais l'ange lui dit: « Ne crains pas, Zacharie, car ta demande a été exaucée. Ta femme, Élisabeth, t'enfantera un fils, et tu lui donneras le nom de Jean.
14 Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
Tu auras de la joie et de l'allégresse, et beaucoup se réjouiront de sa naissance.
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
Car il sera grand aux yeux du Seigneur, et il ne boira ni vin ni boisson forte. Il sera rempli de l'Esprit Saint, dès le sein de sa mère.
16 Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
Il ramènera beaucoup de fils d'Israël à l'Éternel, leur Dieu.
17 Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
Il le précédera avec l'esprit et la puissance d'Élie, pour ramener le cœur des pères vers les enfants, et les désobéissants à la sagesse des justes, afin de préparer un peuple à l'Éternel. »
18 Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
Zacharie dit à l'ange: « Comment puis-je en être sûr? Car je suis un vieil homme, et ma femme est bien avancée en âge. »
19 Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
L'ange lui répondit: « Je suis Gabriel, qui se tient dans la présence de Dieu. J'ai été envoyé pour te parler et t'annoncer cette bonne nouvelle.
20 Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
Voici, tu te tairas et tu ne pourras pas parler jusqu'au jour où ces choses arriveront, parce que tu n'as pas cru à mes paroles, qui s'accompliront en leur temps. »
21 Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
Le peuple attendait Zacharie et s'étonnait qu'il tarde à entrer dans le temple.
22 Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
Lorsqu'il sortit, il ne put leur parler. Ils comprirent qu'il avait eu une vision dans le temple. Il continua à leur faire des signes, et il resta muet.
23 Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
Lorsque les jours de son service furent accomplis, il s'en alla dans sa maison.
24 Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
Après ces jours-là, Élisabeth, sa femme, devint enceinte, et elle se cacha pendant cinq mois, en disant:
25 “Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
« C'est ainsi que le Seigneur m'a fait pendant les jours où il m'a regardée, pour ôter mon opprobre parmi les hommes. »
26 Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
Au sixième mois, l'ange Gabriel fut envoyé par Dieu dans une ville de Galilée, nommée Nazareth,
27 kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
auprès d'une vierge promise en mariage à un homme du nom de Joseph, de la maison de David. Le nom de la vierge était Marie.
28 Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
Après être entré, l'ange lui dit: « Réjouis-toi, toi qui es si favorisée! Le Seigneur est avec toi. Tu es bénie entre toutes les femmes! »
29 Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
Mais quand elle le vit, elle fut très troublée par cette parole, et elle réfléchit à la manière dont elle pouvait être saluée.
30 Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
L'ange lui dit: « Ne crains pas, Marie, car tu as trouvé grâce devant Dieu.
31 Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
Voici que tu concevras dans ton sein et tu donneras naissance à un fils, et tu lui donneras le nom de Jésus.
32 Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
Il sera grand et on l'appellera le Fils du Très-Haut. Le Seigneur Dieu lui donnera le trône de son père David,
33 Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn g165)
et il régnera sur la maison de Jacob pour toujours. Il n'y aura pas de fin à son règne. » (aiōn g165)
34 Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
Marie dit à l'ange: « Comment cela se peut-il, puisque je suis vierge? »
35 Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
L'ange lui répondit: « L'Esprit Saint viendra sur toi, et la puissance du Très-Haut te couvrira de son ombre. C'est pourquoi aussi le saint qui naîtra de toi sera appelé Fils de Dieu.
36 Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
Voici qu'Élisabeth, ta parente, a conçu un fils dans sa vieillesse, et c'est le sixième mois de celle qu'on appelait stérile.
37 Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
Car rien de ce qui est dit par Dieu n'est impossible. »
38 Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
Marie dit: « Voici la servante du Seigneur; qu'il me soit fait selon ta parole. » Puis l'ange s'éloigna d'elle.
39 Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
En ces jours-là, Marie se leva et se rendit en hâte dans la montagne, dans une ville de Juda,
40 Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
elle entra dans la maison de Zacharie et salua Elisabeth.
41 Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
Lorsqu'Elisabeth entendit la salutation de Marie, l'enfant tressaillit dans son sein, et Elisabeth fut remplie du Saint-Esprit.
42 Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
Elle cria d'une voix forte et dit: « Tu es bénie entre toutes les femmes, et le fruit de tes entrailles est béni!
43 Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
Pourquoi suis-je si favorisée, pour que la mère de mon Seigneur vienne à moi?
44 Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
Car voici, quand la voix de ta salutation est parvenue à mes oreilles, le bébé a bondi de joie dans mon sein!
45 Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
Heureuse celle qui a cru, car les choses qui lui ont été dites de la part du Seigneur s'accompliront! »
46 Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
Marie a dit, « Mon âme magnifie le Seigneur.
47 na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
Mon esprit s'est réjoui en Dieu mon Sauveur,
48 Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
car il a regardé l'humble condition de son serviteur. Car voici qu'à partir de maintenant, toutes les générations me diront béni.
49 Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
Car celui qui est puissant a fait de grandes choses pour moi. Saint est son nom.
50 Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
Sa miséricorde s'étend de génération en génération sur ceux qui le craignent.
51 Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
Il a montré de la force avec son bras. Il a dispersé les orgueilleux dans l'imagination de leur cœur.
52 Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
Il a fait tomber les princes de leurs trônes, et a élevé les humbles.
53 Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
Il a rassasié de bonnes choses les affamés. Il a renvoyé les riches à vide.
54 Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
Il a secouru Israël, son serviteur, pour qu'il se souvienne de la miséricorde,
55 (kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn g165)
comme il a parlé à nos pères, à Abraham et à sa descendance pour toujours. » (aiōn g165)
56 Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
Marie resta avec elle environ trois mois, puis elle retourna dans sa maison.
57 Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
Le temps où Élisabeth devait accoucher s'accomplit, et elle donna naissance à un fils.
58 Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
Ses voisins et ses proches apprirent que le Seigneur avait magnifié sa miséricorde envers elle, et ils se réjouirent avec elle.
59 Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
Le huitième jour, on vint pour circoncire l'enfant, et l'on voulut l'appeler Zacharie, du nom de son père.
60 Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
Sa mère répondit: « Non, mais on l'appellera Jean. »
61 Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
Ils lui dirent: « Il n'y a personne parmi tes proches qui soit appelé de ce nom. »
62 Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
Ils firent des signes à son père, pour savoir comment il voulait qu'on l'appelle.
63 Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
Il demanda une tablette et écrivit: « Son nom est Jean. » Ils étaient tous émerveillés.
64 Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
Aussitôt sa bouche s'ouvrit et sa langue se délia, et il parla en bénissant Dieu.
65 Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
La crainte s'empara de tous les habitants des environs, et l'on parlait de toutes ces paroles dans toute la montagne de Judée.
66 Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
Tous ceux qui les entendaient les fixaient dans leur cœur, en disant: « Que sera donc cet enfant? » La main du Seigneur était avec lui.
67 Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
Son père Zacharie fut rempli du Saint-Esprit, et il prophétisa, disant,
68 “Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
« Béni soit le Seigneur, le Dieu d'Israël, car il a visité et racheté son peuple;
69 Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
et il nous a suscité une corne de salut dans la maison de son serviteur David.
70 kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn g165)
(comme il l'a dit par la bouche de ses saints prophètes qui existent depuis des temps immémoriaux), (aiōn g165)
71 Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
le salut de nos ennemis et de la main de tous ceux qui nous haïssent;
72 Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
pour faire preuve de clémence envers nos pères, pour se souvenir de sa sainte alliance,
73 kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
le serment qu'il a fait à Abraham, notre père,
74 Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
de nous accorder que, délivrés de la main de nos ennemis, doivent le servir sans crainte,
75 katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
dans la sainteté et la droiture devant lui tous les jours de notre vie.
76 Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
Et toi, mon enfant, tu seras appelé prophète du Très-Haut; car tu iras devant la face du Seigneur pour préparer ses voies,
77 kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
pour donner la connaissance du salut à son peuple par la rémission de ses péchés,
78 Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
à cause de la tendre miséricorde de notre Dieu, par lequel l'aube d'en haut nous visitera,
79 kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
pour éclairer ceux qui sont assis dans les ténèbres et l'ombre de la mort; pour guider nos pieds sur le chemin de la paix. »
80 Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.
L'enfant grandissait et devenait fort en esprit, et il était dans le désert jusqu'au jour de son apparition publique en Israël.

< Luka 1 >