< Yohana 1 >

1 Mwanzoni kulikuwako Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu.
Au commencement était la Parole, et la Parole était avec Dieu, et la Parole était Dieu.
2 Huyu, Neno, Mwanzoni alikuwa pamoja na Mungu.
Le même était au commencement avec Dieu.
3 Vitu vyote vilifanyika kupitia yeye, na pasipo yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuwa kimefanyika.
Toutes choses ont été faites par elle. Sans elle, rien n'a été fait de ce qui a été fait.
4 Ndani yake kulikuwa uzima, na huo uzima ulikuwa nuru ya wanadamu wote.
En lui était la vie, et la vie était la lumière des hommes.
5 Nuru yang'aa gizani, wala giza halikuizimisha.
La lumière brille dans les ténèbres, et les ténèbres ne l'ont pas vaincue.
6 Palikuwa na mtu aliyetumwa kutoka kwa Mungu, ambaye jina lake alikuwa Yohana.
Il vint un homme envoyé de Dieu, dont le nom était Jean.
7 Alikuja kama shahidi kushuhudia kuhusu ile nuru, ili kwamba wote waweze kuamini kupitia yeye.
Il est venu comme témoin, afin de rendre témoignage à la lumière, pour que tous croient par lui.
8 Yohana hakuwa ile nuru, bali alikuja ili ashuhudie kuhusu ile nuru
Il n'était pas la lumière, mais il a été envoyé pour rendre témoignage à la lumière.
9 Hiyo ilikuwa nuru ya kweli ambayo ilikuwa inakuja katika dunia nayo humtia nuru kila mmoja
La vraie lumière, qui éclaire tout le monde, venait dans le monde.
10 Alikuwa katika dunia, na dunia iliumbwa kupitia yeye, na dunia haikumjua.
Il était dans le monde, et le monde a été fait par lui, et le monde ne l'a pas reconnu.
11 Alikuja kwa vitu vyake, na watu wake hawakumpokea.
Il est venu vers les siens, et les siens ne l'ont pas reçu.
12 Bali kwa wale wengi waliompokea, ambao waliamini jina lake, kwa hao aliwapa haki ya kuwa wana wa Mungu,
Mais à tous ceux qui l'ont reçu, il a donné le droit de devenir enfants de Dieu, à ceux qui croient en son nom,
13 Ambao walizaliwa, sio kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu mwenyewe.
lesquels sont nés, non du sang, ni de la volonté de la chair, ni de la volonté de l'homme, mais de Dieu.
14 Naye Neno alifanyika mwili na akaishi miongoni mwetu, tumeuona utukufu wake, utukufu kama wa mtu pekee wa kipekee aliyekuja kutoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.
Le Verbe s'est fait chair et a vécu parmi nous. Nous avons vu sa gloire, une gloire comme celle du Fils unique du Père, plein de grâce et de vérité.
15 Yohana alishuhudia kuhusu yeye, na alipaza sauti akisema, “Huyu ndiye ambaye nilisema habari zake nikisema, “Yule ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu amekuwako kabla yangu.”
Jean rendit témoignage de lui. Il s'est écrié: « C'est celui dont j'ai dit: Celui qui vient après moi m'a surpassé, car il était avant moi. »
16 Kwa kuwa kutoka katika utimilifu wake, sisi sote tumepokea bure kipawa baada ya kipawa.
De sa plénitude, nous avons tous reçu grâce sur grâce.
17 Kwa kuwa sheria ililetwa kupitia Musa. Neema na kweli vilikuja kupitia Yesu Kristo.
Car la loi a été donnée par Moïse. La grâce et la vérité ont été réalisées par Jésus-Christ.
18 Hakuna mwanadamu aliyemwona Mungu wakati wowote. Mtu pekee ambaye ni Mungu, aliye katika kifua cha Baba, amemfanya yeye ajulikane.
En aucun temps, personne n'a vu Dieu. Le Fils unique, qui est dans le sein du Père, l'a déclaré.
19 Na huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati makuhani na walawi waliotumwa kwake na Wayahudi kumwuliza, “Wewe ni nani?”
Tel est le témoignage de Jean, lorsque les Juifs envoyèrent de Jérusalem des prêtres et des lévites pour lui demander: « Qui es-tu? »
20 Bila kusitasita na hakukana, bali alijibu, “Mimi sio Kristo.”
Il a déclaré, et n'a pas nié, mais il a déclaré: « Je ne suis pas le Christ. »
21 Hivyo wakamuuliza, “kwa hiyo wewe ni nani sasa?” Wewe ni Eliya? Akasema, “Mimi siye.” Wakasema, Wewe ni nabii? Akajibu,” Hapana.”
Ils lui demandèrent: « Qui donc? Es-tu Elijah? » Il a dit: « Je ne le suis pas. » « Vous êtes le prophète? » Il a répondu: « Non. »
22 Kisha wakamwambia, “Wewe ni nani, ili kwamba tuwape jibu waliotutuma”? Wajishuhudiaje wewe mwenyewe?”
Ils lui dirent donc: « Qui es-tu? Donne-nous une réponse à rapporter à ceux qui nous ont envoyés. Que dis-tu de toi-même? »
23 Akasema, “Mimi ni sauti yake aliaye nyikani: 'Inyosheni njia ya Bwana,' kama nabii Isaya alivyosema.”
Il dit: « Je suis la voix de celui qui crie dans le désert: « Aplanissez le chemin du Seigneur », comme l'a dit le prophète Ésaïe. »
24 Basi kulikuwa na watu wametumwa pale kutoka kwa Mafarisayo. Wakamuuliza na kusema,
Ceux qui avaient été envoyés étaient des pharisiens.
25 “Kwa nini unabatiza basi kama wewe sio Kristo wala Eliya wala nabii?”
Ils lui demandèrent: « Pourquoi donc baptises-tu, si tu n'es ni le Christ, ni Élie, ni le prophète? »
26 Yohana aliwajibu akisema, “Ninabatiza kwa maji. Hata hivyo, miongoni mwenu anasimama mtu msiyemtambua.
Jean leur répondit: « Moi, je baptise dans l'eau, mais il y a parmi vous quelqu'un que vous ne connaissez pas.
27 Huyu ndiye ajaye baada yangu. Mimi sisitahili kulegeza kamba za viatu vyake.”
C'est lui qui vient après moi, qui est préféré à moi, et dont je ne suis pas digne de délier la courroie de la sandale. »
28 Mambo haya yalitendeka huko Bethania, ng'ambo ya Yordani, mahali ambapo Yohana alikuwa akibatiza.
Ces choses se passaient à Béthanie, de l'autre côté du Jourdain, où Jean baptisait.
29 Siku iliyofuata Yohana alimwona Yesu akija kwake akasema, “Tazama mwanakondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu!
Le lendemain, il vit Jésus venir à lui, et il dit: « Voici l'Agneau de Dieu, qui enlève le péché du monde!
30 huyu ndiye niliyesema habari zake nikisema, “Yeye ajaye nyuma yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa kuwa alikuwa kabla yangu.'
C'est lui dont j'ai dit: « Après moi vient un homme qui est préféré à moi, car il était avant moi.
31 Sikumtambua yeye, lakini ilifanyika hivyo ili kwamba afunuliwe katika Israeli, kwamba nilikuja nikibatiza kwa maji.”
Je ne l'ai pas connu, mais c'est pour cela que je suis venu baptiser dans l'eau, afin qu'il soit révélé à Israël. »
32 Yohana alishuhudia, “Niliona Roho akishuka kutoka mbinguni mfano wa hua, na ilibaki juu yake.
Jean rendit ce témoignage: « J'ai vu l'Esprit descendre du ciel comme une colombe, et il est resté sur lui.
33 Mimi sikumtambua lakini yeye aliyenituma ili nibatize kwa maji aliniambia, 'yule ambaye utaona Roho akishuka na kukaa juu yake, Huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.'
Je ne l'ai pas reconnu, mais celui qui m'a envoyé baptiser dans l'eau m'a dit: « Celui sur qui tu verras l'Esprit descendre et rester, c'est celui qui baptise dans l'Esprit Saint.
34 Nimeona na nimeshuhudia kwamba huyu ni Mwana wa Mungu.”
J'ai vu et j'ai témoigné que c'est le Fils de Dieu. »
35 Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama pamoja na wanafunzi wake wawili,
Le lendemain, Jean se tenait encore debout avec deux de ses disciples,
36 walimwona Yesu akitembea na Yohana akasema, “Tazama, Mwana kondoo wa Mungu!”
et, regardant Jésus qui marchait, il dit: « Voici l'Agneau de Dieu. »
37 Wanafunzi wawili walimsikia Yohana akisema haya wakamfuata Yesu.
Les deux disciples l'entendirent parler, et ils suivirent Jésus.
38 Tena Yesu aligeuka na kuwaona wanafunzi wale wakimfuata, na akawambia, “Mnataka nini?” Wakajibu, “Rabbi, (maana yake 'mwalimu,' unaishi wapi?”
Jésus se retourna, les vit qui le suivaient, et leur dit: « Que cherchez-vous? » Ils lui dirent: « Rabbi » (ce qui veut dire, en étant interprété, Maître), « où demeures-tu? »
39 Akawambia, “Njooni na mwone.”Kisha walikwenda na kuona mahali alipokuwa akiishi; walikaa pamoja naye siku hiyo, kwa kuwa ilikuwa yapata kama saa kumi hivi.
Il leur dit: « Venez et voyez. » Ils sont venus et ont vu où il se trouvait, et ils sont restés avec lui ce jour-là. C'était environ la dixième heure.
40 Mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana akiongea na kisha kumfuata Yesu alikuwa ni Andrea, ndugu yake Simoni Petro.
L'un de ceux qui avaient entendu Jean et qui le suivirent était André, frère de Simon Pierre.
41 Akamwona ndugu yake Simoni na akamwambia, “Tumempata Masihi” (ambayo inatafsiriwa Kristo).
Il trouva d'abord son propre frère, Simon, et lui dit: « Nous avons trouvé le Messie! » (c'est-à-dire, selon l'interprétation, le Christ).
42 Akamleta kwa Yesu. Yesu akamtazama na akasema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana” utaitwa Kefa,” (maana yake 'Petro').
Il l'amena à Jésus. Jésus le regarda et dit: « Tu es Simon, fils de Jonas. On t'appellera Céphas » (ce qui est, par interprétation, Pierre).
43 Siku iliyofuata wakati Yesu alipotaka kuondoka kwenda Galilaya, alimpata Filipo na akamwambia, “Nifuate mimi.”
Le lendemain, décidé à aller en Galilée, il trouva Philippe. Jésus lui dit: « Suis-moi. »
44 Filipo alikuwa ni mwenyeji wa Bethsaida, mji wa Andrea na Petro.
Or, Philippe était de Bethsaïda, la ville d'André et de Pierre.
45 Filipo alimpata Nathanaeli na kumwambia, Tumempata yule ambaye Musa aliandika habari zake katika sheria na Manabii. Yesu mwana wa Yusufu, kutoka Nazareti.
Philippe, ayant trouvé Nathanaël, lui dit: « Nous avons trouvé celui dont Moïse, dans la loi, et aussi les prophètes, ont parlé: Jésus de Nazareth, fils de Joseph. »
46 Nathanaeli akamwambia, “Je kitu chema chaweza kutokea Nazareti?” Filipo akamwambia, Njoo na uone.”
Nathanaël lui dit: « Peut-il sortir quelque chose de bon de Nazareth? » Philippe lui dit: « Viens et vois. »
47 Yesu akamwona Nathanaeli akija kwake na akasema, “Tazama, Mwisraeli kweli kweli asiye na udanganyifu ndani yake!”
Jésus, voyant Nathanaël s'approcher de lui, dit à son sujet: « Voici vraiment un Israélite en qui il n'y a aucune tromperie! »
48 Nathanaeli akamwambia, “Umenifahamuje mimi?” Yesu akajibu na akamwambia, “Kabla Filipo hajakuita ulipokuwa chini ya mtini, nalikuona.”
Nathanaël lui dit: « Comment me connais-tu? » Jésus lui répondit: « Avant que Philippe ne t'appelle, quand tu étais sous le figuier, je t'ai vu. »
49 Nathanaeli akajibu, “Rabi wewe u Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli”!
Nathanaël lui répondit: « Rabbi, tu es le Fils de Dieu! Tu es le Roi d'Israël! »
50 Yesu akajibu akamwambia, Kwa sababu nilikuambia 'nilikuona chini ya mtini' je waamini? utaona matendo makubwa kuliko haya.”
Jésus lui répondit: « Parce que je t'ai dit: « Je t'ai vu sous le figuier », crois-tu? Tu verras des choses plus grandes que celles-ci! »
51 Yesu akasema, “Amini amini nawambieni mtaziona mbingu zikifunguka, na kuwaona malaika wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
Il lui dit: « Très certainement, je vous le dis à tous, vous verrez désormais le ciel ouvert, et les anges de Dieu monter et descendre sur le Fils de l'homme. »

< Yohana 1 >