< Yohana 3 >

1 Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi lililotawala.
Now there was one of the Pharisees whose name was Nicodemus--a ruler among the Jews.
2 Huyu alimjia Yesu usiku akamwambia, “Rabi, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”
He came to Jesus by night and said, "Rabbi, we know that you are a teacher from God; for no one can do these miracles which you are doing, unless God is with him.
3 Yesu akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”
"In most solemn truth I tell you," answered Jesus, "that unless a man is born anew he cannot see the Kingdom of God."
4 Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa wakati akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”
"How is it possible," Nicodemus asked, "for a man to be born when he is old? Can he a second time enter his mother's womb and be born?"
5 Yesu akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho.
"In most solemn truth I tell you," replied Jesus, "that unless a man is born of water and the Spirit, he cannot enter the Kingdom of God.
6 Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho.
Whatever has been born of the flesh is flesh, and whatever has been born of the Spirit is spirit.
7 Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budi ‘kuzaliwa mara ya pili.’
Do not be astonished at my telling you, 'You must all be born anew.'
8 Upepo huvuma popote upendapo. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”
The wind blows where it chooses, and you hear its sound, but you do not know where it comes from or where it is going. So is it with every one who has been born of the Spirit."
9 Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”
"How is all this possible?" asked Nicodemus.
10 Yesu akamwambia, “Wewe ni mwalimu mashuhuri wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya?
"Are you," replied Jesus, "'the Teacher of Israel,' and yet do you not understand these things?
11 Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu.
In most solemn truth I tell you that we speak what we know, and give testimony of that of which we were eye-witnesses, and yet you all reject our testimony.
12 Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni?
If I have told you earthly things and none of you believe me, how will you believe me if I tell you of things in Heaven?
13 Hakuna mtu yeyote aliyekwenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu.
There is no one who has gone up to Heaven, but there is One who has come down from Heaven, namely the Son of Man whose home is in Heaven.
14 Kama vile Mose alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu.
And just as Moses lifted high the serpent in the Desert, so must the Son of Man be lifted up,
15 Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
in order that every one who trusts in Him may have the Life of the Ages." (aiōnios g166)
16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
For so greatly did God love the world that He gave His only Son, that every one who trusts in Him may not perish but may have the Life of Ages. (aiōnios g166)
17 Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa.
For God did not send His Son into the world to judge the world, but that the world might be saved through Him.
18 Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
He who trusts in Him does not come up for judgement. He who does not trust has already received sentence, because he has not his trust resting on the name of God's only Son.
19 Hii ndiyo hukumu kwamba: Nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru kwa sababu matendo yao ni maovu.
And this is the test by which men are judged--the Light has come into the world, and men loved the darkness more than they loved the Light, because their deeds were wicked.
20 Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe.
For every wrongdoer hates the light, and does not come to the light, for fear his actions should be exposed and condemned.
21 Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”
But he who does what is honest and right comes to the light, in order that his actions may be plainly shown to have been done in God.
22 Baada ya haya, Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika nchi ya Uyahudi, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza.
After this Jesus and His disciples went into Judaea; and there He made a stay in company with them and baptized.
23 Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. Watu wazima wakamjia huko ili kubatizwa.
And John too was baptizing at Aenon, near Salim, because there were many pools of water there; and people came and received baptism.
24 (Hii ilikuwa kabla Yohana hajatiwa gerezani).
(For John was not yet in prison.)
25 Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa kwa utakaso.
As the result, a discussion having arisen on the part of John's disciples with a Jew about purification,
26 Wakamwendea Yohana wakamwambia, “Rabi, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ngʼambo ya Mto Yordani, yule uliyeshuhudia habari zake, sasa anabatiza na kila mtu anamwendea!”
they came to John and reported to him, "Rabbi, he who was with you on the other side of the Jordan and to whom you bore testimony is now baptizing, and great numbers of people are resorting to him."
27 Yohana akawajibu, “Hakuna mtu yeyote awezaye kupata kitu chochote isipokuwa kile tu alichopewa kutoka mbinguni.
"A man cannot obtain anything," replied John, "unless it has been granted to him from Heaven.
28 Ninyi wenyewe ni mashahidi wangu kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo, ila nimetumwa nimtangulie.’
You yourselves can bear witness to my having said, 'I am not the Christ,' but 'I am His appointed forerunner.'
29 Bibi arusi ni wa bwana arusi. Lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama karibu naye na kusikiliza kutoka kwake, hufurahi sana aisikiapo sauti ya bwana arusi. Kwa sababu hii furaha yangu imekamilika.
He who has the bride is the bridegroom; and the bridegroom's friend who stands by his side and listens to him, rejoices heartily on account of the bridegroom's happiness. Therefore this joy of mine is now complete.
30 Yeye hana budi kuwa mkuu zaidi na mimi nizidi kuwa mdogo.”
He must grow greater, but I must grow less.
31 “Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote, yeye aliye wa duniani ni wa dunia, naye huzungumza mambo ya duniani. Yeye aliyekuja kutoka mbinguni, yu juu ya yote.
He who comes from above is above all. He whose origin is from the earth is not only himself from the earth, his teaching also is from the earth. He who comes from Heaven is above all.
32 Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake.
What He has seen and heard, to that He bears witness; but His testimony no one receives.
33 Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli.
Any man who has received His testimony has solemnly declared that God is true.
34 Yeye aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, kwa kuwa Mungu humtoa Roho pasipo kipimo.
For He whom God has sent speaks God's words; for God does not give the Spirit with limitations."
35 Baba anampenda Mwana, naye ametia vitu vyote mikononi mwake.
The Father loves the Son and has entrusted everything to His hands.
36 Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.” (aiōnios g166)
He who believes in the Son has the Life of the Ages; he who disobeys the Son will not enter into Life, but God's anger remains upon him. (aiōnios g166)

< Yohana 3 >