< Yohana 2 >

1 Siku ya tatu kulikuwa na arusi katika mji wa Kana ya Galilaya, naye mama yake Yesu alikuwepo pale.
Two days later there was a wedding at Cana in Galilee, and the mother of Jesus was there,
2 Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa arusini pia.
and Jesus also was invited and His disciples.
3 Divai ilipokwisha, mama yake Yesu akamwambia, “Wameishiwa na divai.”
Now the wine ran short; whereupon the mother of Jesus said to Him, "They have no wine."
4 Yesu akamwambia, “Mwanamke, nina nini nawe? Saa yangu haijawadia.”
"Leave the matter in my hands," He replied; "the time for me to act has not yet come."
5 Mama yake akawaambia wale watumishi, “Lolote atakalowaambia, fanyeni.”
His mother said to the attendants, "Whatever he tells you to do, do it."
6 Basi ilikuwepo mitungi sita ya kuhifadhia maji iliyotengenezwa kwa mawe kwa ajili ya kujitakasa kwa desturi ya Kiyahudi; kila mtungi ungeweza kuchukua vipipa viwili au vitatu.
Now there were six stone jars standing there (in accordance with the Jewish regulations for purification), each large enough to hold twenty gallons or more.
7 Yesu akawaambia wale watumishi, “Ijazeni hiyo mitungi maji.” Nao wakaijaza ile mitungi mpaka juu.
Jesus said to the attendants, "Fill the jars with water." And they filled them to the brim.
8 Kisha akawaambia, “Sasa choteni hayo maji kidogo, mpelekeeni mkuu wa meza.” Hivyo wakachota, wakampelekea.
Then He said, "Now, take some out, and carry it to the President of the feast."
9 Yule mkuu wa meza akayaonja yale maji ambayo yalikuwa yamebadilika kuwa divai. Hakujua divai hiyo ilikotoka ingawa wale watumishi waliochota yale maji wao walifahamu. Basi akamwita bwana arusi kando
So they carried some to him. And no sooner had the President tasted the water now turned into wine, than--not knowing where it came from, though the attendants who had drawn the water knew--he called to the bridegroom
10 akamwambia, “Watu wote hutoa kwanza divai nzuri, kisha huleta ile divai hafifu wageni wakisha kunywa vya kutosha, lakini wewe umeiweka ile nzuri kupita zote mpaka sasa.”
and said to him, "It is usual to put on the good wine first, and when people have drunk freely, then that which is inferior. But you have kept the good wine till now."
11 Huu, ndio uliokuwa muujiza wa kwanza Yesu aliofanya Kana ya Galilaya. Hivyo Yesu alidhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini.
This, the first of His miracles, Jesus performed at Cana in Galilee, and thus displayed His glorious power; and His disciples believed in Him.
12 Baada ya hayo, Yesu pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, walishuka mpaka Kapernaumu, wakakaa huko siku chache.
Afterwards He went down to Capernaum--He, and His mother, and His brothers, and His disciples; and they made a short stay there.
13 Ilipokaribia wakati wa Pasaka ya Wayahudi, Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
But the Jewish Passover was approaching, and for this Jesus went up to Jerusalem.
14 Huko Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ngʼombe, kondoo na njiwa, nao wengine walikuwa wameketi mezani wakibadili fedha.
And He found in the Temple the dealers in cattle and sheep and in pigeons, and the money-changers sitting there.
15 Akatengeneza mjeledi kutokana na kamba, akawafukuza wote kutoka kwenye eneo la Hekalu, pamoja na kondoo na ngʼombe. Akazipindua meza za wale wabadili fedha na kuzimwaga fedha zao.
So He plaited a whip of rushes, and drove all--both sheep and bullocks--out of the Temple. The small coin of the brokers He upset on the ground and overturned their tables.
16 Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, “Waondoeni hapa! Mnathubutuje kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa biashara?”
And to the pigeon-dealers He said, "Take these things away. Do not turn my Father's house into a market."
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa imeandikwa: “Wivu wa nyumba yako utanila.”
This recalled to His disciples the words of Scripture, "My zeal for Thy House will consume me."
18 Ndipo Wayahudi wakamuuliza, “Unaweza kutuonyesha ishara gani ili kuthibitisha mamlaka uliyo nayo ya kufanya mambo haya?”
So the Jews asked Him, "What proof of your authority do you exhibit to us, seeing that you do these things?"
19 Yesu akawajibu, “Libomoeni hili Hekalu, nami nitalijenga tena kwa siku tatu!”
"Demolish this Sanctuary," said Jesus, "and in three days I will rebuild it."
20 Wale Wayahudi wakamjibu, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita, nawe wasema utalijenga kwa siku tatu?”
"It has taken forty-six years," replied the Jews, "to build this Sanctuary, and will you rebuild it in three days?"
21 Lakini yeye Hekalu alilozungumzia ni mwili wake.
But He was speaking of the Sanctuary of His body.
22 Baada ya kufufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka yale aliyokuwa amesema. Ndipo wakayaamini Maandiko na yale maneno Yesu aliyokuwa amesema.
When however He had risen from among the dead, His disciples recollected that He had said this; and they believed the Scripture and the teaching which Jesus had given them.
23 Ikawa Yesu alipokuwa Yerusalemu kwenye Sikukuu ya Pasaka, watu wengi waliona ishara na miujiza aliyokuwa akifanya, wakaamini katika jina lake.
Now when He was in Jerusalem, at the Festival of the Passover, many became believers in Him through watching the miracles He performed.
24 Lakini Yesu hakujiaminisha kwao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
But for His part, Jesus did not trust Himself to them, because He knew them all,
25 Hakuhitaji ushuhuda wa mtu yeyote kuhusu mtu, kwa kuwa alijua yote yaliyokuwa moyoni mwa mtu.
and did not need any one's testimony concerning a man, for He of Himself knew what was in the man.

< Yohana 2 >