< Luka 23 >

1 Kisha umati wote wa watu ukainuka na kumpeleka Yesu kwa Pilato.
Then the whole assembly rose and brought Him to Pilate, and began to accuse Him.
2 Nao wakaanza kumshtaki wakisema: “Tumemwona huyu mtu akipotosha taifa letu, akiwazuia watu wasilipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Kristo, mfalme.”
"We have found this man," they said, "an agitator among our nation, forbidding the payment of tribute to Caesar, and claiming to be himself an anointed king."
3 Basi Pilato akamuuliza Yesu, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe wasema.”
Then Pilate asked Him, "You, then, are the King of the Jews?" "It is as you say," He replied.
4 Pilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”
Pilate said to the High Priests and to the crowd, "I can find no crime in this man."
5 Lakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”
But they violently insisted. "He stirs up the people," they said, "throughout all Judaea with His teaching--even from Galilee (where He first started) to this city."
6 Pilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?”
On hearing this, Pilate inquired, "Is this man a Galilaean?"
7 Alipofahamu kwamba Yesu alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu.
And learning that He belonged to Herod's jurisdiction he sent Him to Herod, for he too was in Jerusalem at that time.
8 Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha.
To Herod the sight of Jesus was a great gratification, for, for a long time, he had been wanting to see Him, because he had heard so much about Him. He hoped also to see some miracle performed by Him.
9 Herode akamuuliza maswali mengi, lakini Yesu hakumjibu lolote.
So he put a number of questions to Him, but Jesus gave him no reply.
10 Wakati huo viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwepo wakitoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
Meanwhile the High Priests and the Scribes were standing there and vehemently accusing Him.
11 Herode na askari wake wakamdhihaki Yesu na kumfanyia mzaha. Wakamvika vazi zuri sana, wakamrudisha kwa Pilato.
Then, laughing to scorn the claims of Jesus, Herod (and his soldiers with him) made sport of Him, dressed Him in a gorgeous costume, and sent Him back to Pilate.
12 Siku hiyo, Herode na Pilato wakawa marafiki; kabla ya jambo hili walikuwa na uadui kati yao.
And on that very day Herod and Pilate became friends again, for they had been for some time at enmity.
13 Basi Pilato akawaita pamoja viongozi wa makuhani, viongozi wengine na watu,
Then calling together the High Priests and the Rulers and the people, Pilate said,
14 akawaambia, “Ninyi mlimleta huyu mtu kwangu kana kwamba ni mtu anayewachochea watu ili waasi. Nimemhoji mbele yenu nami nimeona hakuna msingi wowote wa mashtaka yenu dhidi yake.
"You have brought this man to me on a charge of corrupting the loyalty of the people. But, you see, I have examined him in your presence and have discovered in the man no ground for the accusations which you bring against him.
15 Wala Herode hakumwona na kosa lolote, ndiyo sababu amemrudisha kwetu. Kama mnavyoona, mtu huyu hakufanya jambo lolote linalostahili kifo.
No, nor does Herod; for he has sent him back to us; and, you see, there is nothing he has done that deserves death.
16 Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi na kumwachia.” [
I will therefore give him a light punishment and release him."
17 Kwa kuwa ilikuwa lazima kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa Sikukuu.]
18 Ndipo watu wote wakapiga kelele kwa pamoja, “Mwondoe mtu huyo! Tufungulie Baraba!”
Then the whole multitude burst out into a shout. "Away with this man," they said, "and release Barabbas to us"
19 (Baraba alikuwa amefungwa gerezani kwa sababu ya maasi yaliyokuwa yametokea mjini, na kwa ajili ya uuaji.)
--Barabbas! who had been lodged in jail for some time in connexion with a riot which had occurred in the city, and for murder.
20 Pilato, akitaka kumwachia Yesu, akasema nao tena.
But Pilate once more addressed them, wishing to set Jesus free.
21 Lakini wao wakaendelea kupiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!”
They, however, persistently shouted, "Crucify, crucify him!"
22 Kwa mara ya tatu, Pilato akawauliza, “Kwani amefanya kosa gani huyu mtu? Sikuona kwake sababu yoyote inayostahili adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi, na kisha nitamwachia.”
A third time he appealed to them: "Why, what crime has the man committed? I have discovered in him nothing that deserves death. I will therefore give him a light punishment and release him."
23 Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu zaidi, wakidai kwamba Yesu asulubiwe. Hivyo, kelele zao zikashinda.
But they urgently insisted, demanding with frantic outcries that He should be crucified; and their clamour prevailed.
24 Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu kwamba madai yao yatimizwe.
So Pilate gave judgement, yielding to their demand.
25 Akamfungua yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika uasi dhidi ya serikali na mauaji. Akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfanyie watakavyo.
The man who was lying in prison charged with riot and murder and for whom they clamoured he set free, but Jesus he gave up to be dealt with as they desired.
26 Walipokuwa wakienda naye, wakamkamata mtu mmoja aitwaye Simoni mwenyeji wa Kirene, aliyekuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shambani. Wakambebesha msalaba, wakamlazimisha auchukue nyuma ya Yesu.
As soon as they led Him away, they laid hold on one Simon, a Cyrenaean, who was coming in from the country, and on his shoulders they put the cross, for him to carry it behind Jesus.
27 Idadi kubwa ya watu wakamfuata Yesu, wakiwamo wanawake waliokuwa wakimlilia na kumwombolezea.
A vast crowd of the people also followed Him, and of women who were beating their breasts and wailing for Him.
28 Yesu akawageukia, akawaambia, “Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi bali jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu.
But Jesus turned towards them and said, "Daughters of Jerusalem, weep not for me, but weep for yourselves and for your children.
29 Kwa maana wakati utafika mtakaposema, ‘Wamebarikiwa wanawake tasa, ambao matumbo yao hayakuzaa, wala matiti yao hayakunyonyesha!’
For a time is coming when they will say, 'Blessed are the women who never bore children, and the breasts which have never given nourishment.'
30 Ndipo “‘wataiambia milima, “Tuangukieni!” na vilima, “Tufunikeni!”’
Then will they begin to say to the mountains, 'Fall on us;' and to the hills, 'Cover us.'
31 Kwa maana kama wamefanya hivi kwa mti mbichi, kwa mti mkavu itakuwaje?”
For if they are doing these things in the case of the green tree, what will be done in that of the dry?"
32 Watu wengine wawili wahalifu, walipelekwa pamoja na Yesu ili wakasulubiwe.
They brought also two others, criminals, to put them to death with Him.
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, hapo ndipo walipomsulubisha Yesu pamoja na hao wahalifu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.
When they reached the place called 'The Skull,' there they nailed Him to the cross, and the criminals also, one at His right hand and one at His left.
34 Yesu akasema, “Baba, wasamehe, kwa maana hawajui walitendalo!” Wakagawana nguo zake kwa kupiga kura.
Jesus prayed, "Father, forgive them, for they know not what they are doing." And they divided His garments among them, drawing lots for them;
35 Watu wakasimama hapo wakimwangalia, nao viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.”
and the people stood looking on. The Rulers, too, repeatedly uttered their bitter taunts. "This fellow," they said, "saved others: let him save himself, if he is God's Anointed, the Chosen One."
36 Askari nao wakaja, wakamdhihaki. Wakamletea siki ili anywe,
And the soldiers also made sport of Him, coming and offering Him sour wine and saying,
37 na wakamwambia, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
"Are you the King of the Jews? Save yourself, then!"
38 Kwenye msalaba juu ya kichwa chake, kulikuwa na maandishi haya: Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi. Maandishi haya yalikuwa yameandikwa kwa lugha za Kiyunani, Kilatini na Kiebrania.
There was moreover a writing over His head: THIS IS THE KING OF THE JEWS.
39 Mmoja wa wale wahalifu waliosulubiwa pamoja naye akamtukana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe mwenyewe na utuokoe na sisi.”
Now one of the criminals who had been crucified insulted Him, saying, "Are not you the Christ? Save yourself and us."
40 Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akasema, “Je, wewe humwogopi Mungu, wakati uko kwenye adhabu iyo hiyo?
But the other, answering, reproved him. "Do you also not fear God," he said, "when you are actually suffering the same punishment?
41 Sisi tumehukumiwa kwa haki kwa kuwa tunapata tunayostahili kwa ajili ya matendo yetu. Lakini huyu mtu hajafanya kosa lolote.”
And we indeed are suffering justly, for we are receiving due requital for what we have done. But He has done nothing amiss."
42 Kisha akasema, “Yesu, unikumbuke utakapokuja katika Ufalme wako.”
And he said, "Jesus, remember me when you come in your Kingdom."
43 Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
"I tell you in solemn truth," replied Jesus, "that this very day you shall be with me in Paradise."
44 Ilikuwa kama saa sita mchana, nalo giza likafunika nchi yote hadi saa tisa,
It was now about noon, and a darkness came over the whole country till three o'clock in the afternoon.
45 kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili.
The sun was darkened, and the curtain of the Sanctuary was torn down the middle,
46 Yesu akapaza sauti yake akasema, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.
and Jesus cried out in a loud voice, and said, "Father, to Thy hands I entrust my spirit." And after uttering these words He yielded up His spirit.
47 Yule jemadari alipoona yaliyotukia, akamsifu Mungu, akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.”
The Captain, seeing what had happened, gave glory to God, saying, "Beyond question this man was innocent."
48 Watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hili walipoyaona hayo, wakapigapiga vifua vyao kwa huzuni na kwenda zao.
And all the crowds that had come together to this sight, after seeing all that had occurred, returned to the city beating their breasts.
49 Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wale wanawake waliokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyatazama mambo haya.
But all His acquaintances, and the women who had been His followers after leaving Galilee, continued standing at a distance and looking on.
50 Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,
There was a member of the Council of the name of Joseph, a kind-hearted and upright man,
51 lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa.
who came from the Jewish town of Arimathaea and was awaiting the coming of the Kingdom of God. He had not concurred in the design or action of the Council,
52 Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
and now he went to Pilate and asked for the body of Jesus.
53 Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado.
Then, taking it down, he wrapped it in a linen sheet and laid it in a tomb in the rock, where no one else had yet been put.
54 Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.
It was the Preparation Day, and the Sabbath was near at hand.
55 Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yosefu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa.
The women--those who had come with Jesus from Galilee--followed close behind, and saw the tomb and how His body was placed.
56 Kisha wakarudi nyumbani, wakaandaa manukato na marhamu ya kuupaka huo mwili. Lakini wakapumzika siku ya Sabato kama ilivyoamriwa.
Then they returned, and prepared spices and perfumes. On the Sabbath they rested in obedience to the Commandment.

< Luka 23 >