< Yohana 10 >

1 “Amin, amin nawaambia, yeye asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia kwenye lango, lakini akwea kuingia ndani kwa njia nyingine, ni mwizi na mnyangʼanyi.
"In most solemn truth I tell you that the man who does not enter the sheepfold by the door, but climbs over some other way, is a thief and a robber.
2 Yeye anayeingia kwa kupitia kwenye lango ndiye mchungaji wa kondoo.
But he who enters by the door is the shepherd of the sheep.
3 Mlinzi humfungulia lango na kondoo huisikia sauti yake. Huwaita kondoo wake kwa majina yao na kuwatoa nje ya zizi.
To him the porter opens the door, and the sheep hear his voice; and he calls his own sheep by their names and leads them out.
4 Akiisha kuwatoa wote nje, hutangulia mbele yao na kondoo humfuata kwa kuwa wanaijua sauti yake.
When he has brought out his own sheep--all of them--he walks at the head of them; and the sheep follow him, because they know his voice.
5 Lakini kondoo hawatamfuata mgeni bali watamkimbia, kwa sababu hawaijui sauti ya mgeni.”
But a stranger they will by no means follow, but will run away from him, because they do not know the voice of strangers."
6 Yesu alitumia mfano huu, lakini wao hawakuelewa hayo aliyokuwa akiwaambia.
Jesus spoke to them in this figurative language, but they did not understand what He meant.
7 Kwa hiyo Yesu akasema nao tena akawaambia, “Amin, amin nawaambia, mimi ndimi lango la kondoo.
Again therefore Jesus said to them, "In most solemn truth I tell you that I am the Door of the sheep.
8 Wote walionitangulia ni wevi na wanyangʼanyi, lakini kondoo hawakuwasikia.
All who have come before me are thieves and robbers; but the sheep would not listen to them.
9 Mimi ndimi lango, yeyote anayeingia zizini kwa kupitia kwangu ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
I am the Door. If any one enters by me, he will find safety, and will go in and out and find pasture.
10 Mwizi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi nimekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele.
The thief comes only to steal and kill and destroy: I have come that they may have Life, and may have it in abundance.
11 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
"I am the Good Shepherd. A good shepherd lays down his very life for the sheep.
12 Mtu wa kuajiriwa sio mchungaji mwenye kondoo. Amwonapo mbwa mwitu akija, yeye hukimbia na kuwaacha kondoo. Naye mbwa mwitu hulishambulia kundi na kulitawanya.
The hired servant--one who is not a shepherd and does not own the sheep--no sooner sees the wolf coming than he leaves the sheep and runs away; and the wolf worries and scatters them.
13 Yeye hukimbia kwa sababu ameajiriwa wala hawajali kondoo.
For he is only a hired servant and cares nothing for the sheep.
14 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Ninawajua kondoo wangu nao kondoo wangu wananijua.
"I am the Good Shepherd. And I know my sheep and my sheep know me,
15 Kama vile Baba anavyonijua mimi, nami ninavyomjua Baba, nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.
just as the Father knows me and I know the Father; and I am laying down my life for the sheep.
16 Ninao kondoo wengine ambao si wa zizi hili, inanipasa kuwaleta, nao wataisikia sauti yangu, hivyo patakuwa na kundi moja na mchungaji mmoja.
I have also other sheep--which do not belong to this fold. Those also I must bring, and they will listen to my voice; and they shall become one flock under one Shepherd.
17 Baba yangu ananipenda kwa kuwa ninautoa uhai wangu ili niupate tena.
For this reason my Father loves me, because I am laying down my life in order to receive it back again.
18 Hakuna mtu aniondoleaye uhai wangu, bali ninautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa uhai wangu na pia ninao uwezo wa kuutwaa tena. Amri hii nimepewa na Baba yangu.”
No one is taking it away from me, but I myself am laying it down. I am authorized to lay it down, and I am authorized to receive it back again. This is the command I received from my Father."
19 Kwa maneno haya Wayahudi waligawanyika.
Again there arose a division among the Jews because of these words.
20 Wengi wao wakasema, “Huyu amepagawa na pepo mchafu, naye amechanganyikiwa.”
Many of them said, "He is possessed by a demon and is mad. Why do you listen to him?"
21 Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mtu aliyepagawa na pepo mchafu. Je, pepo mchafu aweza kufungua macho ya kipofu?”
Others argued, "That is not the language of a demoniac: and can a demon open blind men's eyes?"
22 Wakati huo ilikuwa Sikukuu ya Kuwekwa wakfu kwa Hekalu huko Yerusalemu, nao ulikuwa wakati wa majira ya baridi.
The Dedication Festival came on in Jerusalem. It was winter,
23 Naye Yesu alikuwa akitembea ndani ya Hekalu katika ukumbi wa Solomoni.
and Jesus was walking in the Temple in Solomon's Portico,
24 Wayahudi wakamkusanyikia wakamuuliza, “Utatuweka katika hali ya mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo tuambie waziwazi.”
when the Jews gathered round Him and kept asking Him, "How long do you mean to keep us in suspense? If you are the Christ, tell us so plainly."
25 Yesu akawajibu, “Nimewaambia, lakini hamwamini. Mambo ninayoyatenda kwa jina la Baba yangu yananishuhudia.
"I have told you," answered Jesus, "and you do not believe. The deeds that I do in my Father's name--they give testimony about me.
26 Lakini hamwamini, kwa sababu ninyi si wa kundi la kondoo wangu.
But you do not believe, because you are not my sheep.
27 Kondoo wangu huisikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata,
My sheep listen to my voice, and I know them, and they follow me.
28 nami ninawapa uzima wa milele, hawataangamia kamwe wala hakuna mtu atakayewapokonya kutoka mikono yangu. (aiōn g165, aiōnios g166)
I give them the Life of the Ages, and they shall never, never perish, nor shall any one wrest them from my hand. (aiōn g165, aiōnios g166)
29 Baba yangu aliyenipa hawa ni mkuu kuliko wote na hakuna awezaye kuwapokonya kutoka mikononi mwake.
What my Father has given me is more precious than all besides; and no one is able to wrest anything from my Father's hand.
30 Mimi na Baba yangu tu umoja.”
I and the Father are one."
31 Kwa mara nyingine Wayahudi wakainua mawe ili wampige nayo,
Again the Jews brought stones with which to stone Him.
32 lakini Yesu akawaambia, “Nimewaonyesha miujiza mingi mikubwa kutoka kwa Baba yangu. Ni ipi katika hiyo mnataka kunipiga mawe?”
Jesus remonstrated with them. "Many good deeds," He said, "have I shown you as coming from the Father; for which of them are you going to stone me?"
33 Wayahudi wakamjibu, “Hatukupigi mawe kwa sababu ya mambo mema uliyotenda, bali ni kwa kuwa umekufuru. Wewe ingawa ni mwanadamu unajifanya kuwa Mungu.”
"For no good deed," the Jews replied, "are we going to stone you, but for blasphemy, and because you, who are only a man, are making yourself out to be God."
34 Yesu akawajibu, “Je, haikuandikwa katika Sheria ya kwamba, ‘Nimesema kuwa, ninyi ni miungu?’
"Does it not stand written in your Law," replied Jesus, "'I said, you are gods'?
35 Kama aliwaita ‘miungu,’ wale ambao neno la Mungu liliwafikia, nayo Maandiko hayawezi kutanguka,
If those to whom God's word was addressed are called gods (and the Scripture cannot be annulled),
36 je, mwawezaje kusema kwamba yule ambaye Baba amemweka wakfu na kumtuma ulimwenguni anakufuru, kwa sababu nilisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu?’
how is it that you say to one whom the Father consecrated and sent into the world, 'You are blaspheming,' because I said, 'I am God's Son'?
37 Ikiwa sifanyi kazi za Baba yangu, basi msiniamini,
If the deeds I do are not my Father's deeds, do not believe me.
38 lakini ikiwa nazifanya kazi za Mungu, hata kama hamniamini mimi ziaminini hizo kazi, ili mpate kujua na kuelewa kwamba Baba yu ndani yangu, nami ndani yake.”
But if they are, then even if you do not believe me, at least believe the deeds, that you may know and see clearly that the Father is in me, and that I am in the Father."
39 Ndipo wakajaribu kumkamata kwa mara nyingine, lakini akaponyoka kutoka mikononi mwao.
This made them once more try to arrest Him, but He withdrew out of their power.
40 Akaenda tena ngʼambo ya Mto Yordani mpaka mahali pale ambapo Yohana alikuwa akibatiza hapo awali, naye akakaa huko.
Then He went away again to the other side of the Jordan, to the place where John had been baptizing at first; and there He stayed.
41 Watu wengi wakamjia, nao wakawa wakisema, “Yohana hakufanya muujiza wowote, lakini kila jambo alilosema kumhusu huyu mtu ni kweli.”
Large numbers of people also came to Him. Their report was, "John did not work any miracle, but all that John said about this Teacher was true."
42 Nao wengi wakamwamini Yesu huko.
And many became believers in Him there.

< Yohana 10 >