< Proverbios 14 >

1 LA mujer sabia edifica su casa: mas la necia con sus manos la derriba.
Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 El que camina en su rectitud teme á Jehová: mas el pervertido en sus caminos lo menosprecia.
Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
3 En la boca del necio está la vara de la soberbia: mas los labios de los sabios los guardarán.
Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
4 Sin bueyes el granero está limpio: mas por la fuerza del buey hay abundancia de pan.
Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
5 El testigo verdadero no mentirá: mas el testigo falso hablará mentiras.
Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
6 Busca el escarnecedor la sabiduría, y no [la halla]: mas la sabiduría al hombre entendido es fácil.
Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
7 Vete de delante del hombre necio, porque [en él] no advertirás labios de ciencia.
Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
8 La ciencia del cuerdo es entender su camino: mas la indiscreción de los necios es engaño.
Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
9 Los necios se mofan del pecado: mas entre los rectos hay favor.
Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
10 El corazón conoce la amargura de su alma; y extraño no se entrometerá en su alegría.
Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
11 La casa de los impíos será asolada: mas florecerá la tienda de los rectos.
Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
12 Hay camino que al hombre parece derecho; empero su fin son caminos de muerte.
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
13 Aun en la risa tendrá dolor el corazón; y el término de la alegría es congoja.
Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
14 De sus caminos será harto el apartado de razón: y el hombre de bien [estará contento] del [suyo].
Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
15 El simple cree á toda palabra: mas el avisado entiende sus pasos.
Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
16 El sabio teme, y se aparta del mal: mas el necio se arrebata, y confía.
Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
17 El que presto se enoja, hará locura: y el hombre malicioso será aborrecido.
Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
18 Los simples heredarán necedad: mas los cuerdos se coronarán de sabiduría.
Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
19 Los malos se inclinarán delante de los buenos, y los impíos á las puertas del justo.
Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
20 El pobre es odioso aun á su amigo: pero muchos son los que aman al rico.
Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
21 Peca el que menosprecia á su prójimo: mas el que tiene misericordia de los pobres, es bienaventurado.
Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
22 ¿No yerran los que piensan mal? Misericordia empero y verdad [alcanzarán] los que piensan bien.
Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
23 En toda labor hay fruto: mas la palabra de los labios solamente empobrece.
Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
24 Las riquezas de los sabios son su corona: [mas] es infatuación la insensatez de los necios.
Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
25 El testigo verdadero libra las almas: mas el engañoso hablará mentiras.
Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
26 En el temor de Jehová está la fuerte confianza; y esperanza tendrán sus hijos.
Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
27 El temor de Jehová es manantial de vida, para apartarse de los lazos de la muerte.
Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
28 En la multitud de pueblo está la gloria del rey: y en la falta de pueblo la flaqueza del príncipe.
Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
29 El que tarde se aira, es grande de entendimiento: mas el corto de espíritu engrandece el desatino.
Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
30 El corazón apacible es vida de las carnes: mas la envidia, pudrimiento de huesos.
Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
31 El que oprime al pobre, afrenta á su Hacedor: mas el que tiene misericordia del pobre, lo honra.
Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
32 Por su maldad será lanzado el impío: mas el justo en su muerte tiene esperanza.
Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
33 En el corazón del cuerdo reposa la sabiduría; y es conocida en medio de los necios.
Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
34 La justicia engrandece la nación: mas el pecado es afrenta de las naciones.
Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
35 La benevolencia del rey es para con el ministro entendido: mas su enojo [contra] el que [lo] avergüenza.
Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.

< Proverbios 14 >