< Proverbios 13 >

1 EL hijo sabio [toma] el consejo del padre: mas el burlador no escucha las reprensiones.
Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
2 Del fruto de su boca el hombre comerá bien: mas el alma de los prevaricadores [hallará] mal.
Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
3 El que guarda su boca guarda su alma: mas el que mucho abre sus labios tendrá calamidad.
Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
4 Desea, y nada [alcanza] el alma del perezoso: mas el alma de los diligentes será engordada.
Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
5 El justo aborrece la palabra de mentira: mas el impío se hace odioso é infame.
Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
6 La justicia guarda al de perfecto camino: mas la impiedad trastornará al pecador.
Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
7 Hay quienes se hacen ricos, y no tienen nada: y hay quienes se hacen pobres, y tienen muchas riquezas.
Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
8 La redención de la vida del hombre son sus riquezas: pero el pobre no oye censuras.
Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
9 La luz de los justos se alegrará: mas apagaráse la lámpara de los impíos.
Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
10 Ciertamente la soberbia parirá contienda: mas con los avisados es la sabiduría.
Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
11 Disminuiránse las riquezas de vanidad: empero multiplicará el que allega con su mano.
Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
12 La esperanza que se prolonga, es tormento del corazón: mas árbol de vida es el deseo cumplido.
Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
13 El que menosprecia la palabra, perecerá por ello: mas el que teme el mandamiento, será recompensado.
Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
14 La ley del sabio es manantial de vida, para apartarse de los lazos de la muerte.
Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
15 El buen entendimiento conciliará gracia: mas el camino de los prevaricadores es duro.
Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
16 Todo hombre cuerdo obra con sabiduría: mas el necio manifestará necedad.
Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
17 El mal mensajero caerá en mal: mas el mensajero fiel es medicina.
Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
18 Pobreza y vergüenza tendrá el que menosprecia el consejo: mas el que guarda la corrección, será honrado.
Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
19 El deseo cumplido deleita el alma: pero apartarse del mal es abominación á los necios.
Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
20 El que anda con los sabios, sabio será; mas el que se allega á los necios, será quebrantado.
Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
21 Mal perseguirá á los pecadores: mas á los justos les será bien retribuído.
Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
22 El bueno dejará herederos á los hijos de los hijos; y el haber del pecador, para el justo está guardado.
Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
23 En el barbecho de los pobres [hay] mucho pan: mas piérdese por falta de juicio.
Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
24 El que detiene el castigo, á su hijo aborrece: mas el que lo ama, madruga á castigarlo.
Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
25 El justo come hasta saciar su alma: mas el vientre de los impíos tendrá necesidad.
Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.

< Proverbios 13 >