< Proverbios 15 >

1 LA blanda respuesta quita la ira: mas la palabra áspera hace subir el furor.
Jawabu la upole huondoa ghadhabu, bali neno la ukatili huchochea hasira.
2 La lengua de los sabios adornará la sabiduría: mas la boca de los necios hablará sandeces.
Ulimi wa watu mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha wapumbavu humwaga upuuzi.
3 Los ojos de Jehová están en todo lugar, mirando á los malos y á los buenos.
Macho ya Yehova yapo kila mahali, yakiwatazama juu ya waovu na wema.
4 La sana lengua es árbol de vida: mas la perversidad en ella es quebrantamiento de espíritu.
Ulimi unaoponya ni mti wa uzima, bali ulimi wa udanganyifu huvunja moyo.
5 El necio menosprecia el consejo de su padre: mas el que guarda la corrección, vendrá á ser cuerdo.
Mpumbavu hudharau marudi ya baba yake, bali yeye anayejifunza kutokana na masahihisho ni mwenye hekima.
6 En la casa del justo hay gran provisión; empero turbación en las ganancias del impío.
Katika nyumba ya wale watendao haki kuna hazina kubwa, bali mapato ya watu waovu huwapa taabu.
7 Los labios de los sabios esparcen sabiduría: mas no así el corazón de los necios.
Midomo ya wenye hekima husambaza maarifa, bali mioyo ya wapumbavu haifanyi hivyo.
8 El sacrificio de los impíos es abominación á Jehová: mas la oración de los rectos es su gozo.
Yehova anachukia sadaka za watu waovu, bali maombi ya watu waadilifu ndiyo furaha yake.
9 Abominación es á Jehová el camino del impío: mas él ama al que sigue justicia.
Yehova anachukia njia ya watu waovu, bali anampenda yule ambaye huandama haki.
10 La reconvención es molesta al que deja el camino: y el que aborreciere la corrección, morirá.
Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
11 El infierno y la perdición están delante de Jehová: ¡cuánto más los corazones de los hombres! (Sheol h7585)
Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu? (Sheol h7585)
12 El escarnecedor no ama al que le reprende; ni se allega á los sabios.
Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.
13 El corazón alegre hermosea el rostro: mas por el dolor de corazón el espíritu se abate.
Moyo wenye furaha husababisha uchangamfu wa uso, bali huzuni huvunja moyo.
14 El corazón entendido busca la sabiduría: mas la boca de los necios pace necedad.
Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha wapumbavu hujilisha kwenye upuuzi.
15 Todos los días del afligido son trabajosos: mas el de corazón contento [tiene] un convite continuo.
Siku zote za watu waliokandamizwa ni taabu, bali moyo wenye furaha unakaramu daima.
16 Mejor es lo poco con el temor de Jehová, que el gran tesoro donde hay turbación.
Bora kitu kidogo pamoja na kumcha Mungu kuliko hazina kubwa pamoja na ghasia.
17 Mejor es la comida de legumbres donde hay amor, que de buey engordado donde hay odio.
Bora mlo wenye mboga kukiwa na upendo kuliko kuandaliwa ndama aliyenona kwa chuki.
18 El hombre iracundo mueve contiendas: mas el que tarde se enoja, apaciguará la rencilla.
Mtu mwenye hasira huchochea mabishano, bali mtu ambaye hukawia kukasirika hutuliza ugomvi.
19 El camino del perezoso es como seto de espinos: mas la vereda de los rectos [como] una calzada.
Mapito ya mtu goigoi ni kama sehemu yenye uwa wa miiba, bali mapito ya mtu mwadilifu ni njia kuu iliyojengwa imara.
20 El hijo sabio alegra al padre: mas el hombre necio menosprecia á su madre.
Mwana mwenye busara huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
21 La necedad es alegría al falto de entendimiento: mas el hombre entendido enderezará su proceder.
Upuuzi humfurahia mtu ambaye amepungukiwa akili, bali mwenye ufahamu hutembea katika njia nyofu.
22 Los pensamientos son frustrados donde no hay consejo; mas en la multitud de consejeros se afirman.
Mipango huharibika ambapo hakuna ushauri, bali washauri wengi wanafanikiwa.
23 Alégrase el hombre con la respuesta de su boca: y la palabra á su tiempo, ¡cuán buena es!
Mtu anapata furaha wakati anapotoa jibu la kufaa; je ni zuri kiasi gani neno kwa wakati muafaka!
24 El camino de la vida [es] hacia arriba al entendido, para apartarse del infierno abajo. (Sheol h7585)
Njia ya uzima huwapeleka juu watu wenye hekima, ili waondoke kutoka chini kuzimu. (Sheol h7585)
25 Jehová asolará la casa de los soberbios: mas él afirmará el término de la viuda.
Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.
26 Abominación son á Jehová los pensamientos del malo: mas las expresiones de los limpios [son] limpias.
Yehova huyachukia mawazo ya watu waovu, bali maneno ya upole ni safi.
27 Alborota su casa el codicioso: mas el que aborrece las dádivas vivirá.
Mporaji huleta shida kwenye familia yake, bali yeye ambaye huchukia rushwa ataishi.
28 El corazón del justo piensa para responder: mas la boca de los impíos derrama malas cosas.
Moyo wa yule atendaye haki hutafakari kabla ya kujibu, bali kinywa cha watu waovu humwanga ubaya wake wote.
29 Lejos está Jehová de los impíos: mas él oye la oración de los justos.
Yehova yupo mbali na watu waovu, bali husikia maombi ya wale watendao haki.
30 La luz de los ojos alegra el corazón; y la buena fama engorda los huesos.
Nuru ya macho huleta furaha moyoni na habari njema ni afya kwenye mwili.
31 La oreja que escucha la corrección de vida, entre los sabios morará.
Kama utazingatia wakati mtu anapokurekebisha jinsi ya kuishi, utabaki miongoni mwa watu wenye busara.
32 El que tiene en poco la disciplina, menosprecia su alma: mas el que escucha la corrección, tiene entendimiento.
Yeye anayekataa karipio hujidharau mwenyewe, bali yule asikilizaye masahihisho hujipatia ufahamu.
33 El temor de Jehová es enseñanza de sabiduría: y delante de la honra [está] la humildad.
Kumcha Yehova hufundisha hekima na unyenyekevu huja kabla ya heshima.

< Proverbios 15 >