< Proverbios 4 >

1 Oíd hijos la enseñanza del padre; y estád atentos, para que sepáis inteligencia.
Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu; sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.
2 Porque os doy buen enseñamiento: no desamparéis mi ley.
Ninawapa mafundisho ya maana, kwa hiyo msiyaache mafundisho yangu.
3 Porque yo fui hijo de mi padre, delicado y único delante de mi madre:
Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu, ningali mchanga na mtoto pekee kwa mama yangu,
4 Y enseñábame, y me decía: Sustente mis razones tu corazón: guarda mis mandamientos, y vivirás.
baba alinifundisha akisema, “Yashike maneno yangu yote kwa moyo wako wote; yashike maagizo yangu na wewe utaishi.
5 Adquiere sabiduría, adquiere inteligencia: no te olvides, ni te apartes de las razones de mi boca.
Pata hekima, pata ufahamu; usiyasahau maneno yangu wala usiyaache.
6 No la dejes, y ella te guardará; ámala, y conservarte ha.
Usimwache hekima naye atakuweka salama; mpende, naye atakulinda.
7 Primeramente sabiduría: adquiere sabiduría, y ante toda tu posesión adquiere inteligencia.
Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima. Hata ikikugharimu vyote ulivyo navyo, pata ufahamu.
8 Engrandécela, y ella te engrandecerá; ella te honrará, cuando tú la hubieres abrazado.
Mstahi, naye atakukweza; mkumbatie, naye atakuheshimu.
9 Dará a tu cabeza aumento de gracia: corona de hermosura te entregará.
Atakuvika shada la neema kichwani mwako na kukupa taji ya utukufu.”
10 Oye, hijo mío, y recibe mis razones; y multiplicársete han años de vida.
Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia, nayo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.
11 Por el camino de la sabiduría te he encaminado; y por veredas derechas te he hecho andar.
Ninakuongoza katika njia ya hekima na kukuongoza katika mapito yaliyonyooka.
12 Cuando por ellas anduvieres, no se estrecharán tus pasos; y si corrieres, no tropezarás.
Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa; ukimbiapo, hutajikwaa.
13 Ten asida la instrucción, no la dejes: guárdala, porque ella es tu vida.
Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; mshike, maana yeye ni uzima wako.
14 No entres por la vereda de los impíos: ni vayas por el camino de los malos:
Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu wala usitembee katika njia ya watu wabaya.
15 Desampárala; no pases por ella: apártate de ella, y pasa.
Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo; achana nayo, na uelekee njia yako.
16 Porque no duermen, si no hicieren mal; y pierden su sueño, si no han hecho caer.
Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu; wanashindwa hata kusinzia mpaka wamwangushe mtu.
17 Porque comen pan de maldad, y beben vino de robos.
Wanakula mkate wa uovu, na kunywa mvinyo wa jeuri.
18 Mas la vereda de los justos es como la luz del lucero: auméntase, y alumbra hasta que el día es perfecto.
Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko, ambayo hungʼaa zaidi na zaidi mpaka mchana mkamilifu.
19 El camino de los impíos es como la oscuridad: no saben en qué tropiezan.
Lakini njia ya waovu ni kama giza nene; hawajui kinachowafanya wajikwae.
20 Hijo mío, está atento a mis palabras; y a mis razones inclina tu oreja:
Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia; sikiliza kwa makini maneno yangu.
21 No se aparten de tus ojos: mas guárdalas en medio de tu corazón;
Usiruhusu yaondoke machoni pako, yahifadhi ndani ya moyo wako;
22 Porque son vida a los que las hallan; y medicina a toda su carne.
kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata na afya kwa mwili wote wa mwanadamu.
23 Sobre toda cosa guardada, guarda tu corazón; porque de él mana la vida.
Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo, maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
24 Aparta de ti la perversidad de la boca; y la iniquidad de labios aleja de ti.
Epusha kinywa chako na ukaidi; weka mazungumzo machafu mbali na midomo yako.
25 Tus ojos miren lo recto; y tus párpados enderecen tu camino delante de ti.
Macho yako na yatazame mbele, kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.
26 Pesa la vereda de tus pies; y todos tus caminos sean ordenados.
Sawazisha mapito ya miguu yako na njia zako zote ziwe zimethibitika.
27 No te apartes a diestra, ni a siniestra: aparta tu pie del mal.
Usigeuke kulia wala kushoto; epusha mguu wako na ubaya.

< Proverbios 4 >