< Proverbios 3 >

1 Hijo mío, no te olvides de mi ley; y tu corazón guarde mis mandamientos:
Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
2 Porque longura de días, y años de vida, y paz te aumentarán.
kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
3 Misericordia, y verdad no te desamparen: átalas a tu cuello, escríbelas en la tabla de tu corazón;
Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
4 Y hallarás gracia y buena opinión en los ojos de Dios, y de los hombres.
Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
5 Fíate de Jehová de todo tu corazón; y no estribes en tu prudencia.
Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
6 Reconócele en todos tus caminos; y él enderezará tus veredas.
katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
7 No seas sabio en tu opinión: teme a Jehová, y apártate del mal:
Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
8 Porque será medicina a tu ombligo, y tuétano a tus huesos.
Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
9 Honra a Jehová de tu sustancia; y de las primicias de todos tus frutos:
Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
10 Y serán llenos tus alfolíes de hartura; y tus lagares reventarán de mosto.
ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
11 No deseches, hijo mío, el castigo de Jehová: ni te fatigues de su corrección:
Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
12 Porque Jehová al que ama, y quiere, como el padre al hijo, a ese castiga.
kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
13 Bienaventurado el hombre que halló la sabiduría; y que saca a luz la inteligencia.
Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
14 Porque su mercadería es mejor que la mercadería de la plata; y sus frutos, más que el oro fino.
kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
15 Más preciosa es que las piedras preciosas; y todo lo que puedes desear, no se puede comparar a ella.
Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
16 Longura de días trae en su mano derecha: en su izquierda, riquezas y honra.
Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
17 Sus caminos son caminos deleitosos; y todas sus veredas, paz.
Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
18 Esta es el árbol de vida a los que asen de ella; y los que la sustentan, son bienaventurados.
Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
19 Jehová con sabiduría fundó la tierra: afirmó los cielos con inteligencia.
Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
20 Con su ciencia se partieron los abismos; y los cielos destilan el rocío.
kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
21 Hijo mío, no se aparten estas cosas de tus ojos: guarda la ley, y el consejo;
Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
22 Y serán vida a tu alma, y gracia a tu cuello.
ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
23 Entonces caminarás por tu camino confiadamente; y tu pie no tropezará.
Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
24 Cuando te acostares, no habrás temor; y acostarte has, y tu sueño será suave.
ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
25 No habrás temor del pavor repentino, ni de la ruina de los impíos, cuando viniere.
Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
26 Porque Jehová será tu confianza; y el guardará tu pie, porque no seas tomado.
kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
27 No detengas el bien de sus dueños, cuando tuvieres poder para hacerlo.
Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
28 No digas a tu prójimo: Vé, y vuelve, y mañana te daré, cuando tienes contigo.
Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
29 No pienses mal contra tu prójimo, estando él confiado de ti.
Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
30 No pleitées con alguno sin razón, si él no te ha malgalardonado.
Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
31 No tengas envidia al hombre injusto: ni escojas alguno de sus caminos:
Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
32 Porque el perverso es abominado de Jehová; y con los rectos es su secreto.
kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
33 Maldición de Jehová está en la casa del impío; mas a la morada de los justos bendecirá.
Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
34 Ciertamente él escarnecerá a los escarnecedores; y a los humildes dará gracia.
Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
35 Los sabios heredarán la honra; y los insensatos sostendrán deshonra.
Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.

< Proverbios 3 >