< 箴言 知恵の泉 23 >

1 治める人と共に座して食事するとき、あなたの前にあるものを、よくわきまえ、
Unapoketi kula pamoja na mtawala, angalia kwa uangalifu kilichopo mbele yako,
2 あなたがもし食をたしなむ者であるならば、あなたののどに刀をあてよ。
na kama ni mtu unayependa kula chakula sana weka kisu kooni.
3 そのごちそうをむさぼり食べてはならない、これは人を欺く食物だからである。
Usitamani vinono vyake maana ni chakula cha uongo.
4 富を得ようと苦労してはならない、かしこく思いとどまるがよい。
Usifanye kazi sana ili kupata mali; uwe na busara ya kutosha ili ujue wakati wa kuacha.
5 あなたの目をそれにとめると、それはない、富はたちまち自ら翼を生じて、わしのように天に飛び去るからだ。
Je utaruhusu macho yako yaangaze juu yake? Itaondoka, maana itawaa mabawa kama tai na kuruka angani.
6 物惜しみする人のパンを食べてはならない、そのごちそうをむさぼり願ってはならない。
Usile chakula cha yule mwenye jicho baya- na usiwe na shauku ya vinono vyake,
7 彼は心のうちで勘定する人のように、「食え、飲め」とあなたに言うけれども、その心はあなたに真実ではない。
maana ni mtu mwenye kuhesabu gharama ya chakula. “Kula na kunywa!” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.
8 あなたはついにその食べた物を吐き出すようになり、あなたのねんごろな言葉もむだになる。
Utatapika kiasi kidogo ulichokula na utakuwa umepoteza sifa zako njema.
9 愚かな者の耳に語ってはならない、彼はあなたの言葉が示す知恵をいやしめるからだ。
Usiongee katika usikivu wa mpumbavu, maana atadharau hekima ya maneno yako.
10 古い地境を移してはならない、みなしごの畑を侵してはならない。
Usihamishe jiwe la mpaka wa kale au kunyang'anya mashamba ya yatima,
11 彼らのあがない主は強くいらせられ、あなたに逆らって彼らの訴えを弁護されるからだ。
maana Mkombozi wao ni imara na atatetea kesi yao dhidi yako.
12 あなたの心を教訓に用い、あなたの耳を知識の言葉に傾けよ。
Elekeza moyo wako katika mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
13 子を懲らすことを、さし控えてはならない、むちで彼を打っても死ぬことはない。
Usizuie kuadilisha mtoto, maana ukimchapa kwa fimbo, hatakufa.
14 もし、むちで彼を打つならば、その命を陰府から救うことができる。 (Sheol h7585)
Ni wewe unayepaswa kumchapa kwa fimbo na kuikoa nafsi yake kuzimu. (Sheol h7585)
15 わが子よ、もしあなたの心が賢くあれば、わたしの心もまた喜び、
Mwanangu, kama moyo wako una busara, basi moyo wangu utafurahi pia;
16 もしあなたのくちびるが正しい事を言うならば、わたしの心も喜ぶ。
sehemu zangu ndani kabisa zitafurahi sana midomo yako inaponena haki.
17 心に罪びとをうらやんではならない、ただ、ひねもす主を恐れよ。
Usiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi, lakini endelea kumcha Yehova siku zote.
18 かならず後のよい報いがあって、あなたの望みは、すたらない。
Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
19 わが子よ、よく聞いて、知恵を得よ、かつ、あなたの心を道に向けよ。
Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
20 酒にふけり、肉をたしなむ者と交わってはならない。
Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
21 酒にふける者と、肉をたしなむ者とは貧しくなり、眠りをむさぼる者は、ぼろを身にまとうようになる。
maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
22 あなたを生んだ父のいうことを聞き、年老いた母を軽んじてはならない。
Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
23 真理を買え、これを売ってはならない、知恵と教訓と悟りをも買え。
Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
24 正しい人の父は大いによろこび、知恵ある子を生む者は子のために楽しむ。
Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.
25 あなたの父母を楽しませ、あなたを産んだ母を喜ばせよ。
Mfurahishe baba yako na mama yako na yule aliyekuzaa afurahie.
26 わが子よ、あなたの心をわたしに与え、あなたの目をわたしの道に注げ。
Mwanangu, nipe moyo wako na macho yako yachunguze njia zangu.
27 遊女は深い穴のごとく、みだらな女は狭い井戸のようだ。
Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.
28 彼女は盗びとのように人をうかがい、かつ世の人のうちに、不信実な者を多くする。
Anavizia kama mnyang'anyi na huongeza idadi ya wadanganyifu miongoni mwa wanadamu.
29 災ある者はだれか、憂いある者はだれか、争いをする者はだれか、煩いある者はだれか、ゆえなく傷をうける者はだれか、赤い目をしている者はだれか。
Nani mwenye taabu? Nani mwenye huzuni? Nani mwenye mapigano? Nani mwenye malalamiko? Nani mwenye majeraha bila sababu? Nani mwenye macho mekundu?
30 酒に夜をふかす者、行って、混ぜ合わせた酒を味わう者である。
Ni wale ambao huzengea kwenye mvinyo, wale wanaojaribu kuchanganya mvinyo.
31 酒はあかく、杯の中にあわだち、なめらかにくだる、あなたはこれを見てはならない。
Usiutazame mvinyo ukiwa mwekundu, wakati unametameta kwenye kikombe na kutelemka kwa uraini.
32 これはついに、へびのようにかみ、まむしのように刺す。
Mwisho wake unauma kama nyoka na sumu yake kama kifutu.
33 あなたの目は怪しいものを見、あなたの心は偽りを言う。
Macho yako yataona vitu vigeni na moyo wako utatamka vitu vya ukaidi.
34 あなたは海の中に寝ている人のように、帆柱の上に寝ている人のようになる。
Utakuwa kama anayelala kwenye bahari au anayelala juu ya mlingoti. “
35 あなたは言う、「人がわたしを撃ったが、わたしは痛くはなかった。わたしを、たたいたが、わたしは何も覚えはない。いつわたしはさめるのか、また酒を求めよう」と。
Wamenipiga,” utasema, “lakini sikuumia. Wamenichapa, lakini sikuwa na hisia. Nitaamka lini? Nitatafuta kinywaji kingine.”

< 箴言 知恵の泉 23 >