< 箴言 知恵の泉 24 >

1 悪を行う人をうらやんではならない、また彼らと共におることを願ってはならない。
Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
2 彼らはその心に強奪を計り、そのくちびるに人をそこなうことを語るからである。
kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
3 家は知恵によって建てられ、悟りによって堅くせられ、
Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
4 また、へやは知識によってさまざまの尊く、麗しい宝で満たされる。
Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
5 知恵ある者は強い人よりも強く、知識ある人は力ある人よりも強い。
Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
6 良い指揮によって戦いをすることができ、勝利は多くの議する者がいるからである。
maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
7 知恵は高くて愚かな者の及ぶところではない、愚かな者は門で口を開くことができない。
Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
8 悪を行うことを計る者を人はいたずら者ととなえる。
Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
9 愚かな者の計るところは罪であり、あざける者は人に憎まれる。
Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
10 もしあなたが悩みの日に気をくじくならば、あなたの力は弱い。
Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
11 死地にひかれゆく者を助け出せ、滅びによろめきゆく者を救え。
Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
12 あなたが、われわれはこれを知らなかったといっても、心をはかる者はそれを悟らないであろうか。あなたの魂を守る者はそれを知らないであろうか。彼はおのおのの行いにより、人に報いないであろうか。
Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
13 わが子よ、蜜を食べよ、これは良いものである、また、蜂の巣のしたたりはあなたの口に甘い。
Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
14 知恵もあなたの魂にはそのようであることを知れ。それを得るならば、かならず報いがあって、あなたの望みは、すたらない。
Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
15 悪しき者がするように、正しい者の家をうかがってはならない、その住む所に乱暴をしてはならない。
Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
16 正しい者は七たび倒れても、また起きあがる、しかし、悪しき者は災によって滅びる。
Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
17 あなたのあだが倒れるとき楽しんではならない、彼のつまずくとき心に喜んではならない。
Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
18 主はそれを見て悪いこととし、その怒りを彼から転じられる。
au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
19 悪を行う者のゆえに心を悩ましてはならない、よこしまな者をうらやんではならない。
Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
20 悪しき者には後の良い報いはない、よこしまな者のともしびは消される。
maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
21 わが子よ、主と王とを恐れよ、そのいずれにも不従順であってはならない。
Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
22 その災はたちまち起るからである。この二つの者からくる滅びをだれが知り得ようか。
maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
23 これらもまた知恵ある者の箴言である。片寄ったさばきをするのは、よくない。
Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
24 悪しき者に向かって、「あなたは正しい」という者を、人々はのろい、諸民は憎む。
Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
25 悪しき者をせめる者は恵みを得る、また幸福が与えられる。
Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
26 正しい答をする者は、くちびるに、口づけするのである。
Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
27 外で、あなたの仕事を整え、畑で、すべての物をおのれのために備え、その後あなたの家を建てるがよい。
Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
28 ゆえなく隣り人に敵して、証言をしてはならない、くちびるをもって欺いてはならない。
Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
29 「彼がわたしにしたように、わたしも彼にしよう、わたしは人がしたところにしたがって、その人に報いよう」と言ってはならない。
Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
30 わたしはなまけ者の畑のそばと、知恵のない人のぶどう畑のそばを通ってみたが、
Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
31 いばらが一面に生え、あざみがその地面をおおい、その石がきはくずれていた。
Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
32 わたしはこれをみて心をとどめ、これを見て教訓を得た。
Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
33 「しばらく眠り、しばらくまどろみ、手をこまぬいて、またしばらく休む」。
Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
34 それゆえ、貧しさは盗びとのように、あなたに来、乏しさは、つわもののように、あなたに来る。
na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.

< 箴言 知恵の泉 24 >