< 箴言 知恵の泉 22 >

1 令名は大いなる富にまさり、恩恵は銀や金よりも良い。
Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
2 富める者と貧しい者とは共に世におる、すべてこれを造られたのは主である。
Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
3 賢い者は災を見て自ら避け、思慮のない者は進んでいって、罰をうける。
Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
4 謙遜と主を恐れることとの報いは、富と誉と命とである。
Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
5 よこしまな者の道にはいばらとわながあり、たましいを守る者は遠くこれを離れる。
Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
6 子をその行くべき道に従って教えよ、そうすれば年老いても、それを離れることがない。
Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
7 富める者は貧しき者を治め、借りる者は貸す人の奴隷となる。
Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
8 悪をまく者は災を刈り、その怒りのつえはすたれる。
Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
9 人を見て恵む者はめぐまれる、自分のパンを貧しい人に与えるからである。
Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
10 あざける者を追放すれば争いもまた去り、かつ、いさかいも、はずかしめもなくなる。
Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
11 心の潔白を愛する者、その言葉の上品な者は、王がその友となる。
Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
12 主の目は知識ある者を守る、しかし主は不信実な者の言葉を敗られる。
Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
13 なまけ者は言う、「ししがそとにいる、わたしは、ちまたで殺される」と。
Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
14 遊女の口は深い落し穴である、主に憎まれる者はその中に陥る。
Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
15 愚かなことが子供の心の中につながれている、懲しめのむちは、これを遠く追いだす。
Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
16 貧しい者をしえたげて自分の富を増そうとする者と、富める者に与える者とは、ついに必ず貧しくなる。
Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
17 あなたの耳を傾けて知恵ある者の言葉を聞き、かつ、わたしの知識にあなたの心を用いよ。
Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
18 これをあなたのうちに保ち、ことごとく、あなたのくちびるに備えておくなら、楽しいことである。
maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
19 あなたが主に、寄り頼むことのできるように、わたしはきょう、これをあなたにも教える。
Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
20 わたしは、勧めと知識との三十の言葉をあなたのためにしるしたではないか。
Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
21 それは正しいこと、真実なことをあなたに示し、あなたをつかわした者に真実の答をさせるためであった。
kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
22 貧しい者を、貧しいゆえに、かすめてはならない、悩む者を、町の門でおさえつけてはならない。
Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
23 それは主が彼らの訴えをただし、かつ彼らをそこなう者の命を、そこなわれるからである。
maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
24 怒る者と交わるな、憤る人と共に行くな。
Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
25 それはあなたがその道にならって、みずから、わなに陥ることのないためである。
au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
26 あなたは人と手を打つ者となってはならない、人の負債の保証をしてはならない。
Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
27 あなたが償うものがないとき、あなたの寝ている寝床までも、人が奪い取ってよかろうか。
Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
28 あなたの先祖が立てた古い地境を移してはならない。
Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
29 あなたはそのわざに巧みな人を見るか、そのような人は王の前に立つが、卑しい人々の前には立たない。
Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.

< 箴言 知恵の泉 22 >