< Romans 9 >

1 I saye the trueth in Christ and lye not in that wherof my conscience beareth me witnes in the holy gost
Nasema ukweli mtupu; nimeungana na Kristo nami sisemi uongo. Dhamiri yangu ikiongozwa na Roho Mtakatifu inanithibitishia jambo hili pia.
2 that I have gret hevynes and continuall sorowe in my hert.
Nataka kusema hivi: nina huzuni kubwa na maumivu yasiyopimika moyoni mwangu
3 For I have wysshed my selfe to be cursed from Christ for my brethren and my kynsmen as pertayninge to the flesshe
kwa ajili ya watu wangu, walio damu moja nami! Kama ingekuwa kwa faida yao, ningekuwa radhi kulaaniwa na kutengwa na Kristo.
4 which are the Israelites. To whom pertayneth the adopcion and the glorie and the covenauntes and the law that was geven and the service of God and the promyses:
Hao ndio watu wa Israeli ambao Mungu aliwateua wawe watoto wake, akawashirikisha utukufu wake; aliagana nao, akawapa Sheria yake, imani ya kweli na ahadi zake.
5 whose also are the fathers and they of whome (as concernynge the flesshe) Christ came which is God over all thinges blessed for ever Amen. (aiōn g165)
Wao ni wajukuu wa mababu, naye Kristo, kadiri ya ubinadamu wake, ametoka katika ukoo wao. Mungu atawalaye juu ya yote, na atukuzwe milele! Amina. (aiōn g165)
6 I speake not these thinges as though the wordes of god had take none effecte. For they are not all Israelites which came of Israel:
Sisemi kwamba ahadi ya Mungu imebatilika; maana si watu wote wa Israeli ni wateule wa Mungu.
7 nether are they all chyldren strayght waye because they are the seed of Abraham. But in Isaac shall thy seede be called:
Wala, si wazawa wote wa Abrahamu ni watoto wake wa kweli. Ila, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Wazao wake watatokana na Isaka.”
8 that is to saye they which are the chyldren of the flesshe are not the chyldren of god. But the chyldren of promes are counted the seede.
Nido kusema, wale waliozaliwa kimaumbile ndio watoto wa Mungu, bali wale waliozaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ndio watakaoitwa watoto wake.
9 For this is a worde of promes aboute this tyme will I come and Sara shall have a sonne.
Maana ahadi yenyewe ni hii: “Nitakujia wakati maalum, naye Sara atapata mtoto.”
10 Nether was it so wt her only: but also when Rebecca was with chylde by one I meane by oure father Isaac
Tena si hayo tu ila pia Rebeka naye alipata mapacha kwa baba mmoja, yaani Isaka, babu yetu.
11 yeer the chyldren were borne when they had nether done good nether bad: that the purpose of God which is by election myght stonde
Lakini, ili Mungu aonekane kwamba anao uhuru wa kuchagua, hata kabla wale ndugu hawajazaliwa na kabla hawajaweza kupambanua jema na baya,
12 it was sayde vnto her not by the reason of workes but by grace of ye caller: the elder shall serve the yonger.
Rebeka aliambiwa kwamba yule mtoto wa kwanza atamtumikia yule wa nyuma. Hivyo uchaguzi wa Mungu unategemea jinsi anavyoita mwenyewe, na si matendo ya binadamu.
13 As it is written: Iacob he loved but Esau he hated.
Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia.”
14 What shall we saye then? is there eny vnrightewesses with God? God forbyd.
Basi, tuseme nini? Je, Mungu amekosa haki? Hata kidogo!
15 For he sayth to Moses: I will shewe mercye to who I shewe mercy: and will have compassion on whom I have copassion.
Maana alimwambia Mose: “Nitamhurumia mtu yeyote ninayetaka kumhurumia; nitamwonea huruma mtu yeyote ninayetaka.”
16 So lieth it not then in a mans will or cunnynge but in ye mercye of god.
Kwa hiyo, yote hutegemea huruma ya Mungu, na si bidii au mapenzi ya mtu.
17 For the scripture sayth vnto Pharao: Even for this same purpose have I stered ye vp to shewe my power on ye and that my name myght be declared thorow out all the worlde.
Maana Maandiko Matakatifu yasema hivi kwa Farao: “Nilikufanya mfalme ili kwa njia yako, uwezo wangu ujulikane, na jina langu litangazwe popote duniani.”
18 So hath he mercye on whom he will and whom he will he maketh hearde herted.
Ni wazi, basi, kwamba Mungu humhurumia yeyote anayetaka kumhurumia, na akipenda kumfanya mtu awe mkaidi, hufanya hivyo.
19 Thou wilt saye then vnto me: why then blameth he vs yet? For who can resist his will?
Labda utaniuliza: “Ikiwa mambo yako hivyo, Mungu anawezaje kumlaumu mtu? Nani awezaye kuyapinga mapenzi yake?”
20 But o man what arte thou which disputest with God? Shall the worke saye to the workeman: why hast thou made me on this fassion?
Lakini, ewe binadamu, u nani hata uthubutu kumhoji Mungu? Je, chungu chaweza kumwuliza mfinyanzi wake: “Kwa nini umenitengeneza namna hii?”
21 Hath not the potter power over the claye even of the same lompe to make one vessell vnto honoure and a nother vnto dishonoure?
Mfinyanzi anaweza kuutumia udongo apendavyo na kufinyanga vyungu viwili kwa udongo uleule; kimoja kwa matumizi ya heshima, na kingine kwa matumizi ya kawaida.
22 Even so God willynge to shewe his wrath and to make his power knowen suffered with longe pacience the vessels of wrath ordeyned to damnacion
Hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu. Alitaka kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha uwezo wake, Basi, alikuwa na saburi sana, akiwavumilia wale ambao walikuwa lengo la ghadhabu yake, ambao walistahili kuangamizwa.
23 that he myght declare ye ryches of his glory on the vessels of mercye which he had prepayred vnto glorie:
Alitaka pia kudhihirisha wingi wa utukufu wake ambao alitumiminia sisi tulio lengo la huruma yake; sisi ambao alikwisha kututayarisha kuupokea utukufu wake.
24 that is to saye vs which he called not of the Iewes only but also of ye gentyls.
Maana sisi ndio hao aliowaita, si tu kutoka miongoni mwa Wayahudi bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.
25 As he sayth in Osee: I will call them my people which were not my people: and her beloved which was not beloved.
Maana ndivyo asemavyo katika kitabu cha Hosea: “Wale waliokuwa Si watu wangu nitawaita: Watu wangu! Naye Sikupendi ataitwa: Mpenzi wangu!
26 And it shall come to passe in the place where it was sayd vnto them ye are not my people: that there shalbe called the chyldren of the lyvynge God.
Na pale walipoambiwa: Ninyi si wangu hapo wataitwa: Watoto wa Mungu hai.”
27 But Esaias cryeth concernynge Israel though the nomber of the chyldren of Israel be as the sonde of the see yet shall a remnaut be saved.
Naye nabii Isaya, kuhusu Israeli anapaaza sauti: “Hata kama watoto wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaookolewa;
28 He finyssheth the worde verely and maketh it short in ryghtwesses. For a short worde will god make on erth.
maana, Bwana ataitekeleza upesi hukumu yake kamili juu ya ulimwengu wote.”
29 And as Esaias sayd before: Except the Lorde of sabaoth had left us seede we had bene made as Zodoma and had bene lykened to Gomorra.
Ni kama Isaya alivyosema hapo awali: “Kama Bwana Mwenye Nguvu asingalituachia baadhi ya watoto wa Israeli, tungalikwisha kuwa kama Sodoma, tungalikwisha kuwa ma Gomora.”
30 What shall we saye then? We saye that the gentyls which followed not rightewesnes have overtaken rightewesnes: I meane the rightewesnes which cometh of fayth.
Basi, tuseme nini? Ni hivi: watu wa mataifa ambao hawakutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu, wamekubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani,
31 But Israel which folowed the lawe of rightewesnes coulde not attayne vnto ye lawe of rightewesnes.
hali watu wa Israeli waliokuwa wakitafuta Sheria iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu, hawakuipata.
32 And wherfore? Because they sought it not by fath: but as it were by the workes of the lawe. For they have stombled at the stomblynge stone.
Kwa nini? Kwa sababu walitegemea matendo yao badala ya kutegemea imani. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa
33 As it is written: Beholde I put in Syon a stomblynge stone and a rocke which shall make men faule. And none yt beleve on him shalbe a shamed.
kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Tazama! Naweka huko Sioni jiwe likwazalo, mwamba utakaowafanya watu waanguke. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa!”

< Romans 9 >