< 1 Corinthians 1 >

1 Paul by vocacion an Apostle of Iesus Christ thorow the will of God and brother Sostenes.
Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene,
2 Vnto the congregacion of God which is at Corinthum. To them that are sanctified in Christ Iesu sainctes by callynge with all that call on the name of oure lorde Iesus Christ in every place both of theirs and of oures
tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Ninyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia.
3 Grace be with you and peace fro God oure father and from the lorde Iesus Christ.
Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
4 I thanke my God all wayes on youre behalfe for ye grace of God which is geuen you by Iesus Christ
Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia ninyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu.
5 that in all thinges ve are made riche by him in all lerninge and in all knowledge
Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri,
6 even as the testimony of Iesus Christ was confermed in you)
kwani, ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
7 so that ye are behynde in no gyft and wayte for the apperynge of oure lorde Iesus Christ
hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
8 which shall streght you vnto ye ende that ye maye be blamelesse in ye daye of oure lorde Iesus Christ.
Yeye atawaimarisha ninyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia Siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9 ffor god is faythfull by whom ye are called vnto ye fellishyppe of his sonne Iesus Christe oure lorde
Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita ninyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
10 I beseche you brethre in ye name of oure lorde Iesus Christ that ye all speake one thynge and that there be no dissencion amoge you: but be ye knyt together in one mynde and in one meaynge.
Ndugu, ninawasihi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja.
11 It is shewed vnto me (my brethren) of you by them that are of the housse of Cloe that ther is stryfe amonge you. And this is it that I meane:
Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonyesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.
12 how that comelie amonge you one sayeth: I holde of Paul: another I holde of Apollo: ye thyrde I holde of Cephas: ye four ye I holde of Christ.
Nataka kusema hivi: kila mmoja anasema chake: mmoja husema, “Mimi ni wa Paulo,” mwingine: “Mimi ni wa Apolo,” mwingine: “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine: “Mimi ni wa Kristo,”.
13 Ys Christ devided? was Paul crucified for you? ether were ye baptised in ye name of Paul?
Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14 I thanke God that I christened none of you but Crispus and Gayus
Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.
15 lest eny shulde saye that I had baptised in myne awne name.
Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu.
16 I baptised also the housse of Stephana. Forthermore knowe I not whether I baptised eny man or no.
(Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
17 For Christ sent me not to baptyse but to preache ye gospell not with wysdome of wordes lest the crosse of Christ shuld have bene made of none effecte.
Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
18 For ye preachinge of the crosse is to them yt perisshe folishnes: but vnto vs which are saved it is ye power of God.
Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu ujumbe huo ni nguvu ya Mungu.
19 For it is written: I will destroye the wysdome of the wyse and will cast awaye the vnderstondinge of the prudet.
Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali.”
20 Where is the wyse? Where is the scrybe? Where is the searcher of this worlde? Hath not God made the wysdome of this worlde folisshnes? (aiōn g165)
Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu. (aiōn g165)
21 For when the worlde thorow wysdome knew not God in ye wysdome of God: it pleased God thorow folisshnes of preachinge to save them yt beleve.
Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
22 For ye Iewes requyre a signe and the Grekes seke after wysdome.
Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
23 But we preache Christ crucified vnto the Iewes an occasion of fallinge and vnto the Grekes folisshnes:
lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu;
24 but vnto the which are called both of Iewes and Grekes we preache Christ ye power of God and the wysdome of God.
lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.
25 For the folishnes of God is wyser then me: and the weakenes of God is stronger then men.
Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.
26 Brethren loke on youre callinge how that not many wyse men after the flesshe not many myghty not many of hye degre are called:
Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka ya juu.
27 but God hath chosen the folysshe thinges of the worlde to confounde the wyse. And God hath chosyn the weake thinges of the worlde to confounde thinges which are mighty.
Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu.
28 And vile thinges of the worlde and thinges which are despysed hath God chosen yee and thinges of no reputacion for to brynge to nought thinges of reputacion
Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.
29 that no flesshe shulde reioyce in his presence.
Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.
30 And vnto him partayne ye in Christ Iesu which of God is made vnto vs wysdome and also rightewesnes and saunctifyinge and redempcion.
Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha ninyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.
31 That accordinge as it is written: he which reioyseth shulde reioyce in the Lorde.
Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mwenye kutaka kujivuna, basi, na ajivunie kazi ya Bwana.”

< 1 Corinthians 1 >