< Acts 27 >

1 When it was cocluded that we shuld sayle into Italy they delivered Paul and certayne other presoners vnto one named Iulius an vnder captayne of Cesars soudiars.
Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho “Kikosi cha Augusto.”
2 And we entred into a ship of Adramicium and lowsed from lond apoynted to sayle by the costes of Asia one Aristarcus out of Macedonia of the contre of Thessalia beinge with vs.
Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonika, alikuwa pamoja nasi.
3 And the nexte daye we came to Sidon. And Iulius courteously entreated Paul and gave him liberte to goo vnto his frendes and to refresshe him selfe.
Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
4 And from thence lanched we and sayled harde by Cypers because the wyndes were contrarye.
Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi.
5 Then sayled we over the see of Cilicia and Pamphylia and came to Myra a cite in Lycia.
Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
6 And there ye vnder captayne founde a shippe of Alexander redy to sayle into Italy and put vs therin.
Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani.
7 And when we had sayled slowly many dayes and scace were come over agaynst Gnydon (because the wynde with stode vs) we sayled harde by the costes of Candy over agaynste Salmo
Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
8 and with moche worke sayled beyonde yt and came vnto a place called good porte. Nye whervnto was a citie called Lasea.
Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo “Bandari Nzuri”, karibu na mji wa Lasea.
9 When moche tyme was spent and saylinge was now ieoperdeous because also that we had overlonge fasted Paul put them in remembraunce
Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo:
10 and sayde vnto them Syrs I perceave that this vyage wilbe with hurte and moche domage not of the ladynge and ship only: but also of oure lyves.
“Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu.”
11 Neverthelather the vndercaptayne beleved the governer and the master better then tho thinges which were spoken of Paul.
Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
12 And because the haven was not comodius to wynter in many toke counsell to departe thence yf by eny meanes they myght attayne to Phenices and there to wynter which is an haven of Candy and servith to the southwest and northwest wynde.
Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
13 When the south wynde blewe they supposynge to obtayne their purpose lowsed vnto Asson and sayled paste all Candy.
Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakang'oa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete.
14 But anone after ther arose agaynste their purpose a flawe of wynde out of the northeeste.
Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao “Upepo wa Kaskazi” ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
15 And when the ship was caught and coulde not resist the wynde we let her goo and drave with the wether.
Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo.
16 And we came vnto an yle named Clauda and had moche worke to come by abote
Kisiwa kimoja kiitwacho Kanda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
17 which they toke vp and vsed helpe vndergerdynge the shippe fearynge lest we shuld have fallen into Syrtes and we let doune a vessell and so were caryed.
Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libya. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
18 The nexte daye when we were tossed wt an exceadynge tempest they lyghtened ye ship
Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli.
19 and the thyrde daye we cast out with oure awne hondes the tacklynge of the shippe.
Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
20 When at the last nether sunne nor starre in many dayes appered and no small tempest laye apon vs all hope that we shuld be saved was then taken awaye.
Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
21 Then after longe abstinence Paul stode forth in the myddes of them and sayde: Syrs ye shulde have harkened to me and not have lowsed from Candy nether to have brought vnto vs this harme and losse.
Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, “Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
22 And nowe I exhorte you to be of good chere. For ther shalbe no losse of eny mas lyfe amonge you save of the ship only.
Lakini sasa ninawaombeni muwe na moyo; hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake; meli tu ndiyo itakayopotea.
23 For ther stode by me this nyght the angell of God whose I am and whom I serve
Kwa maana jana usiku malaika wa yule Mungu ambaye mimi ni wake na ambaye mimi ninamwabudu alinitokea,
24 sayinge: feare not Paul for thou must be brought before Cesar. And lo God hath geven vnto the all that sayle with ye.
akaniambia: Paulo usiogope! Ni lazima utasimama mbele ya Kaisari; naye Mungu, kwa wema wake, amekufadhili kwa kuwaokoa wote wanaosafiri nawe wasiangamie.
25 Wherfore Syrs be of good chere: for I beleve God that so it shalbe even as it was tolde me.
Hivyo, waheshimiwa, jipeni moyo! Maana ninamwamini Mungu kwamba itakuwa sawa kama nilivyoambiwa.
26 How be it we must be cast into a certayne ylonde.
Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani.”
27 But when ye fourtethe nyght was come as we were caryed in Adria about mydnyght the shipmen demed that ther appered some countre vnto the:
Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huku katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
28 and sounded and founde it. xx. feddoms. And when they had gone a lytell further they sounded agayne and founde. xv. feddoms.
Hivyo walitafuta kina cha bahari kwa kuteremsha kamba iliyokuwa imefungiwa kitu kizito, wakapata kina cha mita arobaini. Baadaye wakapima tena wakapata mita thelathini.
29 Then fearinge lest they shuld have fallen on some Rocke they cast. iiii. ancres out of the sterne and wysshed for ye daye.
Kwa sababu ya kuogopa kukwama kwenye miamba, waliteremsha nanga nne nyuma ya meli; wakaomba kuche upesi.
30 As the shipmen were about to fle out of the ship and had let doune the bote into the see vnder a coloure as though they wolde have cast ancres out of the forshippe:
Wanamaji walitaka kutoroka, na walikwisha kuteremsha ule mtumbwi majini, wakijisingizia kwamba wanakwenda kuteremsha nanga upande wa mbele wa meli.
31 Paul sayd vnto ye vnder captayne and the soudiers: excepte these abyde in the ship ye cannot be safe.
Lakini Paulo alimwambia yule ofisa wa jeshi na askari wake, “Kama wanamaji hawa hawabaki ndani ya meli, hamtaokoka.”
32 Then the soudiers cut of the rope of the bote and let it fall awaye.
Hapo wale askari walizikata kamba zilizokuwa zimeshikilia ule mtumbwi, wakauacha uchukuliwe na maji.
33 And in ye meane tyme betwixt that and daye Paul besought them all to take meate sayinge: this is ye fourtenthe daye that ye have taried and continued fastynge receavinge nothinge at all.
Karibu na alfajiri, Paulo aliwahimiza wote wale chakula: “Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika mashaka na bila kula; hamjala kitu chochote.
34 Wherfore I praye you to take meate: for this no dout is for youre helth: for ther shall not an heere fall fro the heed of eny of you.
Basi, ninawasihi mle chakula kwa maana mnakihitaji ili mweze kuendelea kuishi. Maana hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.”
35 And when he had thus spoke he toke breed and gave thankes to God in presence of the all and brake it and begane to eate.
Baada ya kusema hivyo, Paulo alichukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, akaanza kula.
36 Then were they all of good cheare and they also toke meate.
Hapo wote wakapata moyo, nao pia wakala chakula.
37 We were all together in ye ship two hundred thre score and sixtene soules.
Jumla tulikuwa watu mia mbili na sabini na sita katika meli.
38 And whe they had eate ynough they lightened ye ship and cast out the wheate into the see.
Baada ya kila mmoja kula chakula cha kutosha, walipunguza uzito wa meli kwa kutupa nafaka baharini.
39 Whe yt was daye they knew not ye lande but they spied a certayne haven with a banke into ye which they were mynded (yf yt were possible) to thrust in the ship.
Kulipokucha, wanamaji hawakuweza kuitambua nchi ile, ila waliona ghuba moja yenye ufuko; wakaamua kutia nanga huko kama ikiwezekana.
40 And when they had taken vp the ancres they comytted them selves vnto the see and lowsed the rudder bondes and hoysed vp ye mayne sayle to the wynde and drue to londe.
Hivyo walikata nanga na kuziacha baharini, na wakati huohuo wakazifungua kamba zilizokuwa zimeufunga usukani, kisha wakatweka tanga moja mbele kushika upepo, wakaelekea ufukoni.
41 But they chaunsed on a place which had the see on bothe the sydes and thrust in the ship. And the foore parte stucke fast and moved not but ye hynder brake with the violence of the waves.
Lakini walifika mahali ambapo mikondo miwili ya bahari hukutana, na meli ikakwama. Sehemu ya mbele ilikuwa imezama mchangani bila kutikisika. Sehemu ya nyuma ya meli ilianza kuvunjika vipandevipande kwa mapigo ya nguvu ya mawimbi.
42 The soudears counsell was to kyll ye presoners lest eny of them when he had swome out shulde fle awaye.
Askari walitaka kuwaua wafungwa wote kwa kuogopa kwamba wangeogelea hadi pwani na kutoroka.
43 But the vndercaptayne willinge to save Paul kept the from their purpose and commaunded that they yt could swyme shulde cast the selves first in to ye see and scape to londe.
Lakini kwa vile yule ofisajeshi alitaka kumwokoa Paulo, aliwazuia wasifanye hivyo. Aliamuru wale waliojua kuogelea waruke kutoka melini na kuogelea hadi pwani,
44 And the other he comaunded to goo some on bordes and some on broken peces of the ship. And so it came to passe that they came all safe to londe.
na wengine wafuate wakijishikilia kwenye mbao au kwenye vipande vya meli iliyovunjika. Ndivyo sisi sote tulivyofika salama pwani.

< Acts 27 >