< Acts 28 >

1 And when they were scaped then they knewe that the yle was called Milete.
Tulipokwisha fika salama kwenye nchi kavu, tuligundua kwamba kile kisiwa kinaitwa Malta.
2 And the people of the countre shewed vs no lytell kyndnes: for they kyndled a fyre and receaved vs every one because of the present rayne and because of colde.
Wenyeji wa hapo walikuwa wema sana kwetu. Mvua ilikuwa inaanza kunyesha na kulikuwa na baridi, hivyo waliwasha moto, wakatukaribisha.
3 And when Paul had gaddered a boundle of stickes and put them into the fyre ther came a viper out of the heet and lept on his honde.
Paulo aliokota mzigo mdogo wa kuni akawa anazitia motoni. Hapo, kwa sababu ya lile joto la moto, nyoka akatoka katika kuni akamnasa Paulo mkononi na kujishikilia hapo.
4 When the men of the contre sawe the worme hange on his honde they sayde amonge the selves: this man must nedes be a mortherer. Whome (though he have escaped the see) yet vengeaunce suffreth not to lyve.
Wenyeji wa pale walipokiona kile kiumbe kinaning'inia kwenye mkono wake waliambiana, “Bila shaka mtu huyu amekwisha ua mtu, na ingawa ameokoka kuangamia baharini, Haki haitamwacha aendelee kuishi!”
5 But he shouke of the vermen into the fyre and felt no harme.
Lakini Paulo alikikung'utia kile kiumbe motoni na hakuumizwa hata kidogo.
6 Howbeit they wayted when he shuld have swolne or fallen doune deed sodenly. But after they had loked a greate whyle and sawe no harme come to him they chaunged their myndes and sayde that he was a God.
Wale watu walikuwa wakitazamia kwamba angevimba au hapohapo angeanguka chini na kufa. Baada ya kungojea kwa muda mrefu bila kuona kwamba Paulo amepatwa na jambo lolote lisilo la kawaida, walibadilisha fikira zao juu yake, wakasema kuwa ni mungu.
7 In the same quarters the chefe man of the yle whose name was Publius had a lordshippe: the same receaved vs and lodged vs thre dayes courteously.
Karibu na mahali pale palikuwa na mashamba ya Publio, mkuu wa kile kisiwa. Publio alitukaribisha kirafiki, tukawa wageni wake kwa siku tatu.
8 And it fortuned that the father of Publius laye sicke of a fiever and of a bluddy flixe. To who Paul entred in and prayde and layde his hondes on him and healed him.
Basi, ikawa kwamba baba yake Publio alikuwa amelala kitandani, mgonjwa, ana homa na kuhara. Paulo alikwenda kumwona na baada ya kusali, akaweka mikono yake juu ya mgonjwa, akamponya.
9 When this was done other also which had diseases in the yle came and were healed.
Kutokana na tukio hilo, wagonjwa wote katika kile kisiwa walikuja wakaponywa.
10 And they dyd vs gret honoure. And when we departed they laded vs with thinges necessary.
Watu walitupatia zawadi mbalimbali na wakati tulipoanza tena safari, walitia ndani ya meli masurufu tuliyohitaji.
11 After thre monethes we departed in a ship of Alexandry which had wyntred in the yle whose badge was Castor and Pollux.
Baada ya miezi mitatu tulianza tena safari yetu kwa meli moja ya Aleksandria iitwayo “Miungu Pacha”. Meli hiyo ilikuwa imetia nanga kisiwani wakati wote wa baridi.
12 And whe we came to Cyracusa we taryed there. iii. dayes.
Tulifika katika mji wa Sirakusa, tukakaa hapo kwa siku tatu.
13 And from thence we set a compasse and came to Regium. And after one daye the south wynde blewe and we came the next daye to Putiolus:
Toka huko tuling'oa nanga, tukazunguka na kufika Regio. Baada ya siku moja, upepo ulianza kuvuma kutoka kusini, na baada ya siku mbili tulifika bandari ya Potioli.
14 where we founde brethren and were desyred to tary with them seven dayes and so came to Rome.
Huko tuliwakuta ndugu kadhaa ambao walituomba tukae nao kwa juma moja. Hivi ndivyo tulivyopata kufika Roma.
15 And from thence when ye brethren hearde of vs they came agaynst vs to Apiphorum and to ye thre taverns. When Paul sawe the he thanked God and wexed bolde.
Ndugu wa kule Roma walipopata habari zetu, wakaja kutulaki kwenye soko la Apio na Mikahawa Mitatu. Paulo alipowaona alimshukuru Mungu, akapata moyo.
16 And when he came to Rome ye vnder captayne delyvered ye presoners to ye chefe captayne of ye host: but Paul was suffered to dwell by him selfe with one soudier that kept him.
Tulipofika Roma, Paulo aliruhusiwa kukaa peke yake pamoja na askari mmoja wa kumlinda.
17 And it fortuned after thre dayes that Paul called ye chefe of ye Iewes together. And whe they were come he sayde vnto the: Men and brethren though I have comitted nothinge agaynst the people or lawes of oure fathers: yet was I delyvered presoner from Ierusalem in to the hondes of ye Romayns.
Baada ya siku tatu, Paulo aliwaita pamoja viongozi wa Kiyahudi wa mahali hapo. Walipokusanyika, Paulo aliwaambia, “Wananchi wenzangu, mimi, ingawa sikufanya chochote kibaya wala kupinga desturi za wazee wetu, nilitiwa nguvuni kule Yerusalemu na kutiwa mikononi mwa Waroma.
18 Which when they had examined me wolde have let me goo because they founde no cause of deeth in me.
Waliponihoji na kuona kwamba sikuwa na hatia yeyote, walitaka kuniacha.
19 But when ye Iewes cryed cotrary I was constrayned to appeale vnto Cesar: not because I had ought to accuse my people of.
Lakini Wayahudi wengine walipinga jambo hilo, nami nikalazimika kukata rufani kwa Kaisari, ingawa sikuwa na chochote cha kuwashtaki wananchi wenzangu.
20 For this cause have I called for you eve to se you and to speake with you: because that for the hope of Israel I am bounde with this chayne.
Ni kwa sababu hiyo nimeomba kuonana na kuongea nanyi, maana nimefungwa minyororo hii kwa sababu ya tumaini lile la Israeli.”
21 And they sayde vnto him: We nether receaved letters out of Iewry pertayninge vnto ye nether came eny of the brethren that shewed or spake eny harme of the.
Wao wakamwambia, “Sisi hatujapokea barua yoyote kutoka Yudea, wala hakuna ndugu yeyote aliyefika hapa na kutoa habari rasmi au kusema chochote kibaya juu yako.
22 But we will heare of the what thou thynkest. For we have hearde of this secte that every wheare it is spoken agaynst.
Lakini tunafikiri inafaa tusikie kutoka kwako mwenyewe mambo yaliyo kichwani mwako. Kwa maana tujualo sisi kuhusu hicho kikundi ni kwamba kinapingwa kila mahali.”
23 And when they had apoynted him a daye ther came many vnto him into his lodgynge. To whom he expounded and testifyed the kyngdome of God and preached vnto the of Iesu: both out of the lawe of Moses and also out of the prophetes even from mornynge to nyght.
Basi, walipanga naye siku kamili ya kukutana, na wengi wakafika huko alikokuwa anakaa. Tangu asubuhi mpaka jioni Paulo aliwaeleza na kuwafafanulia juu ya Ufalme wa Mungu akijaribu kuwafanya wakubali habari juu ya Yesu kwa kutumia Sheria ya Mose na maandiko ya manabii.
24 And some beleved ye thinges which were spoken and some beleved not.
Baadhi yao walikubali maneno yake, lakini wengine hawakuamini.
25 When they agreed not amonge the selves they departed after that Paul had spoken one worde. Well spake the holy goost by Esay ye prophet vnto oure fathers
Basi, kukawa na mtengano wa fikira kati yao. Walipokuwa wanakwenda zao, Paulo alisema jambo hili, “Kweli ni sawa yale aliyoyanena Roho Mtakatifu kwa wazee wenu kwa njia ya nabii Isaya
26 sayinge: Goo vnto this people and saye: with youre eares shall ye heare and shall not vnderstonde: and with youre eyes shall ye se and shall not perceave.
akisema: Nenda kwa watu hawa ukawaambie: kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa; kutazama mtatazama, lakini hamtaona.
27 For the hert of this people is wexed grosse and their eares were thycke of hearynge and their eyes have they closed: lest they shuld se with their eyes and heare with their eares and vnderstonde with their hertes and shuld be converted and I shulde heale them.
Maana akili za watu hawa zimepumbaa, wameziba masikio yao, wamefumba macho yao. La sivyo, wangeona kwa macho yao, wangesikia kwa masikio yao. Wangeelewa kwa akili zao, na kunigeukia, asema Bwana, nami ningewaponya.”
28 Be it knowen therfore vnto you that this salvacion of God is sent to the gentyls and they shall heare it.
Halafu Paulo akamaliza na kusema, “Jueni basi, kwamba ujumbe wa Mungu juu ya wokovu umepelekwa kwa watu wa mataifa. Wao watasikiliza!”
29 And when he had sayde that the Iewes departed and had grete despicios amonge them selves.
Paulo alipokwisha sema hayo, Wayahudi walijiondokea huku wakiwa wanabishana vikali wao kwa wao.
30 And Paul dwelt two yeares full in his lodgynge and receaved all that came to him
Kwa muda wa miaka miwili mizima Paulo aliishi katika nyumba aliyoipanga yeye mwenyewe; akawa anawakaribisha wote waliofika kumsalimu.
31 preachyng the kyngdome of God and teachynge those thinges which concerned the lorde Iesus with all confidence vnforboden.
Alikuwa akihubiri Ufalme wa Mungu na kufundisha juu ya Bwana Yesu Kristo kwa uhodari, bila kizuizi.

< Acts 28 >