< Romans 16 >

1 I commede vnto you Phebe oure sister (which is a minister of the congregacion of Chenchrea)
Napenda kumjulisha kwenu dada yetu Foibe ambaye ni mtumishi katika kanisa la Kenkrea.
2 that ye receave her in the Lorde as it becommeth saynctes and that ye assist her in whatsoever busynes she neadeth of youre ayde. For she hath suckered many and myne awne selfe also.
Mpokeeni kwa ajili ya Bwana kama iwapasavyo watu wa Mungu. Mpeni msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, maana yeye amekuwa mwema sana kwa watu wengi na kwangu pia.
3 Grete Prisca and Aquila my helpers in Christ Iesu
Salamu zangu ziwafikie Priska na Akula, wafanyakazi wenzangu katika utumishi wa Kristo Yesu.
4 which have for my lyfe layde doune their awne neckes. Vnto which not I only geve thankes but also the congregacion of the getyls.
Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu. Wanastahili shukrani; si tu kutoka kwangu, bali pia kutoka kwa makanisa yote ya watu wa mataifa mengine.
5 Lyke wyse grete all the copany that is in thy housse. Salute my welbeloved Epenetos which is the fyrst frute amoge them of Achaia.
Salamu zangu pia kwa kanisa linalokutana nyumbani kwao. Salamu zangu zimfikie rafiki yangu Epaineto ambaye ni kwa kwanza katika mkoa wa Asia kumwamini Kristo.
6 Grete Mary which bestowed moche labour on vs.
Nisalimieni Maria ambaye amefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
7 Salute Andronicus and Iunia my cosyns which were presoners with me also which are wele taken amoge the Apostles and were in Christ before me.
Salamu zangu kwa Androniko na Yunia, wananchi wenzangu waliofungwa gerezani pamoja nami; wao wanajulikana sana kati ya mitume; tena walikuwa Wakristo kabla yangu mimi.
8 Grete Amplias my beloved in ye Lorde.
Salamu zangu kwa Ampliato, rafiki yangu katika kuungana na Bwana.
9 Salute Vrban oure helper in Christ and Stachys my beloved.
Salamu zangu zimfikie Urbano, mfanyakazi mwenzangu katika utumishi wa Kristo; salamu zangu pia kwa rafiki yangu Staku.
10 Salute Appelles approved in Christ. Salute them which are of Aristobolus housholde.
Nisalimieni Apele ambaye uaminifu wake kwa Kristo umethibitishwa. Salamu zangu kwa wote walio nyumbani mwa Aristobulo.
11 Salute Herodion my kynsma. Grete them of the housholde of Narcissus which are in the Lorde.
Salamu zangu kwa Herodiana, mwananchi mwenzangu; na kwa jamaa yote ya Narkisi iliyojiunga na Bwana.
12 Salute Triphena and Triphosa which wemen dyd labour in ye Lorde. Salute ye beloved Persis which laboured in the Lorde.
Nisalimieni Trufena na Trufosa wanaofanya kazi katika utumishi wa Bwana, na rafiki yangu Persi ambaye amefanya mengi kwa ajili ya Bwana.
13 Salute Rufus chosen tn the Lorde and his mother and myne.
Nisalimieni Rufo, mtu hodari sana katika kazi ya Bwana, na mama yake ambaye ni mama yangu pia.
14 Grete Asincritus Phlegon Herman Patrobas Hermen and the brethren which are wt them.
Nisalimieni Asunkrito, Flegoni, Herme Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.
15 Salute Philologus and Iulia Nereus and his sister and Olimpha and all the saynctes which are with them.
Nisalimieni Filologo na Yulia, Nerea na dada yake, na Olumpa, pamoja na watu wote wa Mungu walio pamoja nao.
16 Salute one another with an holy kysse. The congregacions of Christ salute you.
Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa ishara ya upendo. Salamu kwenu kutoka kwa makanisa yote ya Kristo.
17 I beseche you brethre marke them which cause division and geve occasions of evyll contrary to the doctrine which ye have learned: and avoyde them.
Ndugu zangu, nawasihi muwafichue wote wanaosababisha mafarakano na kuwafanya watu wengine waanguke, kinyume cha mafundisho mliyofundishwa. Jiepusheni na watu hao,
18 For they yt are suche serve not ye Lorde Iesus Christ: but their awne bellyes and with swete preachinges and flatteringe wordes deceave the hertes of the innocetes.
maana watu wa namna hiyo hawamtumikii Kristo Bwana wetu, bali wanayatumikia matumbo yao wenyewe. Kwa maneno yao matamu na hotuba za kubembeleza hupotosha mioyo ya watu wanyofu.
19 For youre obedience extendeth to all men. I am glad no dout of you. But yet I wolde have you wyse vnto yt which is good and to be innocetes concerninge evyll.
Kila mtu amesikia juu ya utii wenu na hivyo mmekuwa sababu ya furaha yangu. Nawatakeni muwe na hekima katika mambo mema, na bila hatia kuhusu mambo mabaya.
20 The God of peace treade Satan vnder youre fete shortly. The grace of oure Lorde Iesu Christ be with you.
Naye Mungu aliye chanzo cha amani hatakawia kumponda Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
21 Thimotheus my worke felow and Lucius and Iason and Sopater my kynsmen salute you.
Timotheo, mfanyakazi mwenzangu, anawasalimu. Hali kadhalika Lukio, Yasoni, na Sosipatro, wananchi wenzangu, wanawasalimu.
22 I Tertius salute you which wrote this epistle in the Lorde.
Nami Tertio, ninayeandika barua hii nawasalimuni katika Bwana.
23 Gaius myne hoste and the hoste of all the congregacions saluteth you. Erastus the chamberlayne of ye cite saluteth you. And Quartus a brother saluteth you.
Gayo, mwenyeji wangu, pamoja na kanisa lote linalokutana kwake, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto, wanawasalimu.
24 The grace of oure Lorde Iesu Christ be wt you all. Ame
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amina.
25 To him that is of power to stablisshe you accordinge to my gospell and preachinge of Iesus Christ in vtteringe of the mistery which was kept secret sence the worlde begane (aiōnios g166)
Basi, sasa na tumsifu Mungu! Yeye anaweza kuwaimarisheni katika ile Habari Njema niliyohubiri juu ya ujumbe wa Yesu Kristo, na katika ile siri iliyofunuliwa na ambayo ilikuwa imefichika kwa karne nyinyi zilizopita. (aiōnios g166)
26 but now is opened by ye scriptures of prophesie at the commaundement of the everlastinge god to stere vp obedience to the faith publisshed amonge all nacions: (aiōnios g166)
Lakini, sasa ukweli huo umefunuliwa kwa njia ya maandiko ya manabii; na kwa amri ya Mungu wa milele umedhihirisha kwa mataifa yote ili wote waweze kuamini na kutii. (aiōnios g166)
27 To the same God which alone is wyse be prayse thorowe Iesus Christ for ever. Amen. (aiōn g165)
Kwake Mungu aliye peke yake mwenye hekima, uwe utukufu kwa njia ya Yesu Kristo, milele na milele! Amina. (aiōn g165)

< Romans 16 >