< Acts 1 >

1 In the former treatise (Deare frende Theophilus) I have written of all that Iesus beganne to do and teache
Ndugu Theofilo, Katika kitabu cha kwanza niliandika juu ya mambo yote Yesu aliyotenda na kufundisha tangu mwanzo wa kazi yake
2 vntyll the daye in the which he was taken vp after that he thorowe the holy goost had geven commaundementes vnto the Apostles which he had chosen:
mpaka siku ile alipochukuliwa mbinguni. Kabla ya kuchukuliwa mbinguni aliwapa maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
3 to whom also he shewed him selfe alyve after his passion by many tokens apperynge vnto them fourty dayes and speakynge of the kyngdome of god
Kwa muda wa siku arobaini baada ya kifo chake aliwatokea mara nyingi kwa namna ambazo zilithibitisha kabisa kwamba alikuwa hai. Walimwona, naye aliongea nao juu ya ufalme wa Mungu.
4 and gaddered them togeder and commaunded the that they shuld not departe from Ierusalem: but to wayte for ye promys of the father whereof ye have herde of me.
Wakati walipokutana pamoja aliwaamuru hivi: “Msiondoke Yerusalemu, bali ngojeeni ile zawadi aliyoahidi Baba, zawadi ambayo mlikwisha nisikia nikiongea juu yake.
5 For Iohn baptised wt water: but ye shalbe baptised with the holy goost and that with in this feawe dayes.
Kwani Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
6 When they were come togeder they axed of him sayinge: Lorde wilt thou at this tyme restore agayne ye kyngdome to Israel?
Basi, mitume walipokutana pamoja na Yesu, walimwuliza, “Je Bwana, wakati huu ndipo utakaporudisha ule ufalme kwa Israeli?”
7 And he sayde vnto them: It is not for you to knowe the tymes or the seasons which ye father hath put in his awne power:
Lakini Yesu akawaambia, “Nyakati na majira ya mambo hayo viko chini ya mamlaka ya Baba yangu, wala si shauri lenu kujua yatakuwa lini.
8 but ye shall receave power of the holy goost which shall come on you. And ye shall be witnesses vnto me in Ierusalem and in all Iewrye and in Samary and even vnto the worldes ende.
Lakini wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na hata miisho ya dunia.”
9 And when he had spoken these thinges whyll they behelde he was take vp and a cloude receaved him vp out of their sight.
Baada ya kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni; wingu likamficha wasimwone tena.
10 And while they looked stedfastly vp to heaven as he went beholde two men stode by them in white apparell
Walipokuwa bado wanatazama juu angani, akiwa anakwenda zake, mara watu wawili waliokuwa wamevaa nguo nyeupe walisimama karibu nao,
11 which also sayde: ye men of Galile why stonde ye gasinge vp into heave? This same Iesus which is taken vp fro you in to heaven shall so come even as ye haue sene him goo into heaven.
wakasema, “Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna hiyohiyo mliivyomwona akienda mbinguni.”
12 Then returned they vnto Ierusalem from mount olivete which is nye to Ierusalem coteyninge a Saboth dayes iorney.
Kisha mitume wakarudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko karibu kilomita moja kutoka mjini.
13 And when they were come in they went vp into a parler where abode both Peter and Iames Iohn and Andrew Philip and Thomas Bartlemew and Mathew Iames the sonne of Alpheus and Simo Zelotes and Iudas Iames sonne.
Walipofika mjini waliingia katika chumba ghorofani ambamo walikuwa wanakaa; nao walikuwa Petro, Yohane, Yakobo, Andrea, Filipo na Thoma, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
14 These all cotinued with one acorde in prayer and supplicacion with the wemen and Mary the mother of Iesu and with his brethren.
Hawa wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria mama yake Yesu, na ndugu zake.
15 And in those dayes Peter stode vp in the myddes of the disciples and sayde (the noumbre of names that were to gether were aboute an hondred and twenty)
Siku chache baadaye, kulikuwa na mkutano wa waumini, karibu watu mia moja na ishirini. Petro alisimama mbele yao,
16 Ye men and brethren this scripture must have nedes ben fulfilled which the holy goost thorow ye mouth of David spake before of Iudas which was gyde to them that tooke Iesus.
akasema, “Ndugu zangu, ilikuwa lazima ile sehemu ya Maandiko Matakatifu itimie, sehemu ambayo Roho Mtakatifu, kwa maneno ya Daudi, alibashiri habari za Yuda ambaye aliwaongoza wale waliomtia Yesu nguvuni.
17 For he was noubred with vs and had obtayned fellouship in this ministracion.
Yuda alikuwa mmoja wa kikundi chetu maana alichaguliwa ashiriki huduma yetu.
18 And the same hath now possessed a plot of grounde with the rewarde of iniquite and when he was hanged brast a sondre in ye myddes and all his bowels gusshed oute.
(“Mnajua kwamba yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na kitendo chake kiovu. Akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika nje.
19 And it is knowe vnto all the inhabiters of Ierusalem: in so moche that that felde is called in their mother tonge Acheldama that is to saye the bloud felde.
Kila mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao, wakaliita lile shamba Hekeli Dama, maana yake, Shamba la Damu.)
20 It is written in the boke of Psalmes: His habitacio be voyde and no man be dwellinge therin: and his bisshoprycke let another take.
Basi, imeandikwa katika kitabu cha Zaburi: Nyumba yake ibaki mahame; mtu yeyote asiishi ndani yake. Tena imeandikwa: Mtu mwingine achukue nafasi yake katika huduma hiyo.
21 Wherfore of these me which have copanyed with vs all ye tyme that the Lorde Iesus wet in and out amonge vs
Kwa hiyo, ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi kama shahidi wa ufufuo wake Bwana Yesu.
22 begynninge at the baptyme of Iohn vnto that same daye that he was taken vp from vs must one be ordeyned to be are witnes with vs of his resurreccion.
Anapaswa kuwa mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana alipokuwa anasafiri pamoja nasi, tangu wakati Yohane alipokuwa anabatiza mpaka siku ile Yesu alipochukuliwa kutoka kwetu kwenda mbinguni.”
23 And they appoynted two Ioseph called Barsabas (whose syr name was Iustus) and Mathias.
Basi, wakataja majina ya watu wawili; wa kwanza Yosefu aliyeitwa Barsaba (au pia Yusto), na wa pili Mathia.
24 And they prayed sayinge: thou Lorde which knowest the hertes of all me shewe whether of these two thou hast chosen
Kisha wakasali: “Bwana, wewe unajua mioyo ya watu wote. Hivyo, utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
25 that the one maye take the roume of this ministracion and apostleshippe from the which Iudas by transgression fell that he myght go to his awne place.
ili achukue nafasi hii ya huduma ya kitume aliyoacha Yuda akaenda mahali pake mwenyewe.”
26 And they gave forthe their lottes and the lot fell on Mathias and he was counted with the eleven Apostles.
Hapo, wakapiga kura; kura ikampata Mathia, naye akaongezwa katika idadi ya wale mitume wengine kumi na mmoja.

< Acts 1 >