< Acts 7 >

1 Then sayde ye chefe prest: is it even so?
Basi, Kuhani Mkuu akamwuliza, “Je, mambo haya ni kweli?”
2 And he sayde: ye men brethren and fathers harken to. The God of glory appered vnto oure father Abraha whyll he was yet in Mesopotamia before he dwelt in Charran
Naye Stefano akasema, “Ndugu zangu na akina baba, nisikilizeni! Mungu alimtokea baba yetu Abrahamu alipokuwa kule Mesopotamia kabla hajaenda kukaa kule Harani.
3 and sayd vnto him: come out of thy contre and from thy kynred and come into the londe which I shall shewe the.
Mungu alimwambia: Ondoka katika nchi yako; waache watu wa ukoo wako; nenda katika nchi nitakayokuonyesha!
4 Then came he out of the londe of Chaldey and dwelt in Charran. And after that assone as his father was deed he brought him into this lande in which ye now dwell
Kwa hivyo, Abrahamu alihama nchi ya Kaldayo, akaenda kukaa Harani. Baada ya kifo cha baba yake, Mungu alimtoa tena Harani akaja kukaa katika nchi hii mnayokaa sasa.
5 and he gave him none inheritaunce in it no not the bredeth of a fote: but promised yt he wolde geve it to him to possesse and to his seed after him when as yet he had no chylde.
Mungu hakumpa hata sehemu moja ya nchi hii iwe mali yake; hata hivyo, alimwahidia kumpa nchi hii iwe yake na ya wazawa wake, ingawaje wakati huu hakuwa na mtoto.
6 God verely spake on this wyse that his seade shulde be a dweller in a straunge londe and that they shulde kepe them in bondage and entreate them evyll. iiii. C. yeares.
Mungu alimwambia hivi: Wazao wako watapelekwa katika nchi inayotawaliwa na watu wengine, na huko watafanywa watumwa na kutendewa vibaya kwa muda wa miaka mia nne.
7 But the nacion to whom they shalbe in bondage will I iudge sayde God. And after that shall they come forthe and serve me in this place.
Lakini mimi nitalihukumu taifa hilo litakalowafanya watumwa. Kisha nitawatoa katika nchi hiyo ili waje kuniabudu mahali hapa.
8 And he gave him the covenaunt of circumcision. And he begat Isaac and circumcised him the viii. daye and Isaac begat Iacob and Iacob the twelve patriarkes
Halafu Mungu aliifanya tohara iwe ishara ya agano. Hivyo, Abrahamu alimtahiri mtoto wake Isaka, siku ya nane baada ya kuzaliwa. Na Isaka, vivyo hivyo, alimtahiri Yakobo. Naye Yakobo aliwatendea wale mababu kumi na wawili vivyo hivyo.
9 And the patriarkes havinge indignacio solde Ioseph into Egipte. And God was with him
“Wale mababu walimwonea wivu Yosefu, wakamuuza utumwani Misri. Lakini Mungu alikuwa pamoja naye,
10 and delivered him out of all his adversities. And gave him faveour and wisdome in the sight of Pharao kynge of Egipte which made him governer over Egipte and over all his housholde.
akamwokoa katika taabu zake zote. Mungu alimjalia fadhili na hekima mbele ya Farao, mfalme wa Misri, hata Farao akamweka awe mkuu wa ile nchi na nyumba ya kifalme.
11 Then came ther a derth over all the londe of Egipt and Canaan and great affliccion that our fathers founde no sustenauce.
Kisha, kulizuka njaa kubwa katika nchi yote ya Misri na Kanaani, ikasababisha dhiki kubwa. Babu zetu hawakuweza kupata chakula chochote.
12 But when Iacob hearde that ther was corne in Egipte he sent oure fathers fyrst
Basi, Yakobo alipopata habari kwamba huko Misri kulikuwa na nafaka, aliwatuma watoto wake, yaani babu zetu, waende huko Misri mara ya kwanza.
13 and at the seconde tyme Ioseph was knowen of his brethren and Iosephs kynred was made knowne vnto Pharao.
Katika safari yao ya pili, Yosefu alijitambulisha kwa ndugu zake, na Farao akaifahamu jamaa ya Yosefu.
14 Then sent Ioseph and caused his father to be brought and all his kynne thre score and xv. soules.
Yosefu alituma ujumbe kwa baba yake na jamaa yote, jumla watu sabini na tano, waje Misri.
15 And Iacob descended into Egipte and dyed bothe he and oure fathers
Hivyo, Yakobo alikwenda Misri ambako yeye na babu zetu wengine walikufa.
16 and were translated into Sichem ond were put in ye sepulcre that Abraham bought for money of the sonnes of Emor at Sichem.
Miili yao ililetwa mpaka Shekemu, ikazikwa katika kaburi Abrahamu alilonunua kutoka kwa kabila la Hamori kwa kiasi fulani cha fedha.
17 When ye tyme of ye promes drue nye (which God had sworme to Abraham) the people grewe and multiplied in Egipte
“Wakati ulipotimia Mungu aitimize ahadi aliyompa Abrahamu, idadi ya wale watu kule Misri ilikwisha ongezeka na kuwa kubwa zaidi.
18 till another kynge arose which knewe not of Ioseph.
Mwishowe, mfalme mmoja ambaye hakumtambua Yosefu alianza kutawala huko Misri.
19 The same dealte suttelly with oure kynred and evyll intreated oure fathers and made them to cast oute their younge chyldren that they shuld not remayne alyve.
Alilifanyia taifa letu ukatili, akawatendea vibaya babu zetu kwa kuwalazimisha waweke nje watoto wao wachanga ili wafe.
20 The same tyme was Moses borne and was a proper childe in ye sight of God which was norisshed vp in his fathers housse thre monethes.
Mose alizaliwa wakati huo. Alikuwa mtoto mzuri sana. Alilelewa nyumbani kwa muda wa miezi mitatu,
21 When he was cast out Pharoes doughter toke him vp and norisshed him vp for her awne sonne.
na alipotolewa nje, binti wa Farao alimchukua, akamlea kama mtoto wake.
22 And Moses was learned in all maner wisdome of the Egipcians and was mighty in dedes and in wordes.
Mose alifundishwa mambo yote ya hekima ya Wamisri akawa mashuhuri kwa maneno na matendo.
23 And when he was full forty yeare olde it came into his hert to visit his brethren the chyldren of Israhel.
“Alipokuwa na umri wa miaka arobaini aliamua kwenda kuwaona ndugu zake Waisraeli.
24 And when he sawe one of them suffre wronge he defended him and avenged his quarell that had the harme done to him and smote the Egypcian.
Huko alimwona mmoja wao akitendewa vibaya, akaenda kumwokoa, na kulipiza kisasi, akamuua yule Mmisri.
25 For he supposed hys brethren wolde have vnderstonde how yt God by his hondes shuld save them But they vnderstode not.
(Alidhani kwamba Waisraeli wenzake wangeelewa kwamba Mungu angemtumia yeye kuwakomboa, lakini hawakuelewa hivyo.)
26 And the next daye he shewed him selfe vnto the as they strove and wolde have set the at one agayne sayinge: Syrs ye are brethren why hurte ye one another?
Kesho yake, aliwaona Waisraeli wawili wakipigana, akajaribu kuwapatanisha, akisema: Ninyi ni ndugu; kwa nini basi, kutendeana vibaya ninyi kwa ninyi?
27 But he that dyd his neghbour wronge thrust him awaye sayinge: who made ye a rular and a iudge amonge vs?
Yule aliyekuwa anampiga mwenzake alimsukuma Mose kando akisema: Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi wa watu?
28 What wilt thou kyll me as thou dyddest the Egyptian yester daye?
Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri jana?
29 Then fleed Moses at that sayenge and was a stranger in the londe of Madian where he begat two sonnes.
Baada ya kusikia hayo Mose alikimbia, akaenda kukaa katika nchi ya Midiani na huko akapata watoto wawili.
30 And when. xl. yeares were expired ther appered to him in the wyldernes of mounte Syna an angell of the Lorde in a flamme of fyre in a busshe.
“Miaka arobaini ilipotimia, malaika wa Bwana alimtokea Mose katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto kule jangwani karibu na mlima Sinai.
31 When Moses sawe it he wondred at the syght. And as he drue neare to beholde the voyce of the Lorde came vnto him:
Mose alistaajabu sana kuona jambo hilo hata akasogea karibu ili achungulie; lakini alisikia sauti ya Bwana:
32 I am ye God of thy fathers the God of Abraham the God of Isaac and the God of Iacob. Moses trembled and durst not beholde.
Mimi ni Mungu wa baba zako, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo! Mose akatetemeka kwa hofu na wala hakuthubutu kutazama zaidi.
33 Then sayde ye Lorde to him: Put of thy showes from thy fete for the place where thou stondest is holy grounde.
Bwana akamwambia: Vua viatu vyako maana hapa unaposimama ni mahali patakatifu.
34 I have perfectly sene the affliccion of my people which is in Egypte and I have hearde their gronynge and am come doune to delyver them. And now come and I will sende the into Egypte.
Nimeyaona mabaya wanayotendewa watu wangu kule Misri. Nimesikia kilio chao, nami nimekuja kuwaokoa. Basi sasa, nitakutuma Misri.
35 This Moses whom they forsoke sayinge: who made the a ruelar and a iudge: the same God sent bothe a ruler and delyverer by ye hondes of the angell which appered to him in the busshe.
“Huyu Mose ndiye yule watu wa Israeli waliyemkataa waliposema: Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi wetu? Kwa njia ya yule malaika aliyemtokea katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto, Mungu alimtuma Mose huyo awe kiongozi na mkombozi.
36 And the same brought them out shewynge wonders and signes in Egypte and in the reed see and in the wyldernes. xl. yeares.
Ndiye aliyewaongoza wale watu watoke Misri kwa kufanya miujiza na maajabu katika nchi ya Misri, katika bahari ya Shamu na jangwani kwa muda wa miaka arobaini.
37 This is that Moses which sayde vnto the chyldre of Israel: A Prophet shall the Lorde youre God rayse vp vnto you of youre brethren lyke vnto me him shall ye heare.
Mose ndiye aliyewaambia watu wa Israeli: Mungu atawateulieni nabii kama mimi kutoka katika ndugu zenu ninyi wenyewe.
38 This is he that was in ye congregacion in the wyldernes with the angell which spake to him in ye moute Syna and with oure fathers. This man receaved the worde of lyfe to geve vnto vs
Wakati watu wa Israeli walipokutana pamoja kule jangwani, Mose ndiye aliyekuwako huko pamoja nao. Alikuwa huko pamoja na babu zetu na yule malaika aliyeongea naye mlimani Sinai; ndiye aliyekabidhiwa yale maneno yaletayo uzima atupe sisi.
39 to who oure fathers wolde not obeye but cast it from them and in their hertes turned backe agayne into Egypte
“Lakini yeye ndiye babu zetu waliyemkataa kumsikiliza; walimsukuma kando, wakatamani kurudi Misri.
40 sayinge vnto Aaron: Make vs goddes to goo before vs. For this Moses that brought vs out of the londe of Egypte we wote not what is become of him.
Walimwambia Aroni: Tutengenezee miungu itakayotuongoza njiani, maana hatujui yaliyompata Mose huyu aliyetuongoza kutoka Misri!
41 And they made a calfe in those dayes and offered sacrifice vnto the ymage and reioysed in the workes of their awne hondes.
Hapo ndipo walipojitengenezea sanamu ya ndama, wakaitambikia na kukifanyia sherehe kitu ambacho ni kazi ya mikono yao wenyewe.
42 Then God turned him selfe and gave them vp that they shuld worship the starres of the skye as it is written in the boke of the prophetes. O ye of ye housse of Israel gave ye to me sacrefices and meate offerynges by the space of xl. yeares in the wildernes?
Lakini Mungu aliondoka kati yao, akawaacha waabudu nyota za anga, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha manabii: Enyi watu wa Israeli! Si mimi mliyenitolea dhabihu na sadaka kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani!
43 And ye toke vnto you the tabernacle of Moloch and the starre of youre god Remphan figures which ye made to worshippe them. And I will translate you beyonde Babylon.
Ninyi mlikibeba kibanda cha mungu Moloki, na sanamu ya nyota ya mungu wenu Refani. Sanamu mlizozifanya ndizo mlizoabudu. Kwa sababu hiyo nitakupeleka mateka mbali kupita Babuloni!
44 Oure fathers had the tabernacle of witnes in ye wyldernes as he had apoynted the speakynge vnto Moses that he shuld make it acordynge to the fassion that he had sene.
Kule jangwani babu zetu walikuwa na lile hema lililoshuhudia kuweko kwa Mungu. Lilitengenezwa kama Mungu alivyomwambia Mose alifanye; nakala kamili ya kile alichoonyeshwa.
45 Which tabernacle oure fathers receaved and brought it in with Iosue into the possession of the gentyls which God drave out before the face of oure fathers vnto the tyme of David
Kisha babu zetu walilipokezana wao kwa wao mpaka wakati wa Yoshua, walipoinyakua ile nchi kutoka kwa mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele yao. Hapo lilikaa mpaka nyakati za Daudi.
46 which founde favour before God and desyred that he myght fynde a tabernacle for the God of Iacob.
Daudi alipata upendeleo kwa Mungu, akamwomba Mungu ruhusa ya kumjengea makao yeye aliye Mungu wa Yakobo.
47 But Salomon bylt him an housse.
Lakini Solomoni ndiye aliyemjengea Mungu nyumba.
48 How be it he that is hyest of all dwelleth not in teple made with hondes as saith the Prophete:
“Hata hivyo, Mungu Mkuu haishi katika nyumba zilizojengwa na binadamu; kama nabii asemavyo:
49 Heven is my seate and erth is my fote stole what housse will ye bylde for me sayth the Lorde? or what place is it that I shuld rest in?
Bwana asema: Mbingu ni kiti changu cha enzi na dunia ni kiti changu cha kuwekea miguu.
50 hath not my honde made all these thinges?
Ni nyumba ya namna gani basi mnayoweza kunijengea, na ni mahali gani nitakapopumzika? Vitu hivi vyote ni mimi nimevifanya, au sivyo?
51 Ye stiffenecked and of vncircumcised hertes and eares: ye have all wayes resisted the holy goost: as youre fathers dyd so do ye.
“Enyi wakaidi wakuu! Mioyo na masikio yenu ni kama ya watu wa mataifa. Ninyi ni kama baba zenu. Siku zote mnampinga Roho Mtakatifu.
52 Which of the prophetes have not youre fathers persecuted? And they have slayne them which shewed before of the commynge of that iust whom ye have now betrayed and mordred.
Je, yuko nabii yeyote ambaye baba zenu hawakumtesa? Waliwaua hao Mungu aliowatuma watangaze kuja kwake yule Mwenye Haki. Na sasa, ninyi mmemsaliti, mkamuua.
53 And ye also have receaved a lawe by the ordinaunce of angels and have not kept it.
Ninyi mliipokea ile Sheria iliyoletwa kwenu na Malaika, lakini hamkuitii.”
54 When they hearde these thinges their hertes clave a sunder and they gnasshed on him with their tethe.
Wale wazee wa Baraza waliposikia hayo, walighadhibika sana, wakamsagia meno kwa hasira.
55 But he beynge full of the holy goost loked vp stedfastlye with his eyes into heven and sawe the glorie of God and Iesus stondynge on the ryght honde of God
Lakini Stefano akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akatazama juu mbinguni, akauona utukufu wa Mungu na Yesu amekaa upande wa kulia wa Mungu.
56 and sayde: beholde I se the hevens open and the sonne of man stondynge on the ryght honde of god.
Akasema, “Tazameni! Ninaona mbingu zimefunuliwa na Mwana wa Mtu amesimama upande wa kulia wa Mungu.”
57 Then they gave a shute with a loude voyce and stopped their eares and ranne apon him all at once
Hapo, watu wote katika kile kikao cha Baraza, wakapiga kelele na kuziba masikio yao kwa mikono yao. Kisha wakamrukia wote kwa pamoja,
58 and caste him out of the cite and stoned him. And the witnesses layde doune their clothes at a yonge mannes fete named Saul.
wakamtoa nje ya mji, wakampiga mawe. Wale mashahidi wakayaweka makoti yao chini ya ulinzi wa kijana mmoja jina lake Saulo.
59 And they stoned Steven callynge on and sayinge: Lorde Iesu receave my sprete.
Waliendelea kumpiga mawe Stefano, huku akiwa anasali: “Bwana Yesu, ipokee roho yangu!”
60 And he kneled doune and cryed with a loude voyce: Lorde laye not this synne to their charge. And when he had thus spoken he fell a slepe.
Akapiga magoti, akalia kwa sauti kubwa: “Bwana, usiwalaumu kwa sababu ya dhambi hii.” Baada ya kusema hivyo, akafa.

< Acts 7 >