< Acts 20 >

1 After the rage was ceased Paul called the disciples vnto him and toke his leave of them and departed for to goo into Macedonia.
Ile ghasia ya Efeso ilipokwisha tulia Paulo aliwaita pamoja wale waumini, akawatia moyo. Kisha akawaaga, akasafiri kwenda Makedonia.
2 And when he had gone over those parties and geven them large exhortacions he came into Grece
Alipitia sehemu za nchi zile akiwatia watu moyo kwa maneno mengi. Halafu akafika Ugiriki.
3 and there abode. iii. monethes. And when the Iewes layde wayte for him as he was about to sayle into Syria he purposed to returne thorowe Macedonia.
ambako alikaa kwa miezi mitatu. Alipokuwa anajitayarisha kwenda Siria, aligundua kwamba Wayahudi walikuwa wanamfanyia mpango mbaya; hivyo aliamua kurudi kwa kupitia Makedonia.
4 Ther acompanied him into Asia Sopater of Berrea and of Thessalonia Aristarcus and Secundus and Gayus of Derba and Timotheus: and out of Asia Tychicus and Trophimos.
Sopatro, mwana wa Pirho kutoka Berea, aliandamana naye; pia Aristarko na Sekundo kutoka Thesalonika, Gayo kutoka Derbe, Timotheo, Tukiko na Trofimo wa mkoa wa Asia.
5 These went before and taryed vs at Troas.
Hao walitutangulia na kutungojea kule Troa.
6 And we sayled awaye fro Philippos after the ester holydayes and came vnto them to Troas in five dayes where we abode seven dayes.
Sisi, baada ya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, tulipanda meli kutoka Filipi na baada ya siku tatu tukawafikia kule Troa. Huko tulikaa kwa muda wa juma moja.
7 And on the morowe after the saboth daye the disciples came to geder for to breake breed and Paul preached vnto them (redy to departe on the morowe) and cotinued the preachynge vnto mydnyght.
Jumamosi jioni, tulikutana ili kumega mkate. Kwa vile Paulo alikuwa amekusudia kuondoka kesho yake, aliwahutubia watu na kuendelea kuongea nao hadi usiku wa manane.
8 And there were many lyghtes in the chamber where thy were gaddered to geder
Katika chumba tulimokuwa, ghorofani, kulikuwa na taa nyingi zinawaka.
9 and there sate in a wyndowe a certayne yonge man named Eutichos fallen into a depe slepe. And as Paul declared he was the moare overcome with slepe and fell doune from the thyrde lofte and was taken vp deed.
Kijana mmoja aitwaye Eutuko alikuwa ameketi dirishani wakati Paulo alipokuwa anaendelea kuhutubu. Eutuko alianza kusinzia kidogokidogo na hatimaye usingizi ukambana, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu. Wakamwokota amekwisha kufa.
10 Paul went doune and fell on him and embrased him and sayde: make nothinge ado for his lyfe is in him.
Lakini Paulo alishuka chini, akainama, akamkumbatia na kusema, “Msiwe na wasiwasi maana kuna uhai bado ndani yake.”
11 When he was come vp agayne he brake breed and tasted and comened a longe whyle even tyll the mornynge and so departed.
Kisha akapanda tena ghorofani, akamega mkate, akala. Aliendelea kuhubiri kwa muda mrefu hadi alfajiri, halafu akaondoka.
12 And they brought the youge man a lyve and were not alytell comforted.
Wale watu walimchukua yule kijana nyumbani akiwa mzima kabisa, wakapata kitulizo kikubwa.
13 And we went a fore to shippe and lowsed vnto Asson there to receave Paul. For so had he apoynted and wolde him selfe goo a fote.
Sisi tulipanda meli tukatangulia kwenda Aso ambako tungemchukua Paulo. Ndivyo alivyopanga; maana alitaka kufika huko kwa kupitia nchi kavu.
14 When he was come to vs vnto Asson we toke him in and came to Mytelenes.
Basi, alitukuta kule Aso, tukampandisha melini, tukaenda Mitulene.
15 And we sayled thence and came the nexte daye over agaynst Chios. And the nexte daye we aryved at Samos and taryed at Trogilion. The nexte daye we came to Myleton:
Kutoka huko tulisafiri tukafika Kio kesho yake. Siku ya pili, tulitia nanga Samo na kesho yake tukafika Mileto.
16 for Paul had determined to leave Ephesus as they sayled because he wolde not spende ye tyme in Asia. For he hasted to be (yf he coulde possible) at Ierusalem at the daye of pentecoste.
Paulo alikuwa amekusudia kuendelea na safari kwa meli bila kupitia Efeso ili asikawie zaidi huko Asia. Alikuwa na haraka ya kufika Yerusalemu kwa sikukuu ya Pentekoste kama ingewezekana.
17 Wherfore from Myleton he sent to Ephesus and called the elders of the cogregacion.
Kutoka Mileto Paulo alituma ujumbe kwa wazee wa Efeso wakutane naye.
18 And when they were come to him he sayde vnto the: Ye knowe fro the fyrst daye yt I came vnto Asia after what maner I have bene wt you at all ceasons
Walipofika kwake aliwaambia, “Mnajua jinsi nilivyotumia wakati wote pamoja nanyi tangu siku ile ya kwanza nilipofika Asia.
19 servynge the lorde with all humblenes of mynde and with many teares and temptacions which happened vnto me by the layinges awayte of the Ieues
Mnajua jinsi nilivyomtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote, kwa machozi na matatizo yaliyonipata kutokana na mipango ya hila ya Wayahudi.
20 and how I kept backe no thinge that was profitable: but that I have shewed you and taught you openly and at home in youre houses
Mnajua kwamba sikusita hata kidogo kuwahubiria hadharani na nyumbani mwenu na kuwafundisha chochote ambacho kingewasaidieni.
21 witnessinge bothe to the Iewes and also to the Grekes the repentaunce toward God and faith towarde oure Lorde Iesu.
Niliwaonya wote—Wayahudi kadhalika na watu wa mataifa, wamgeukie Mungu na kumwamini Bwana wetu Yesu.
22 And now beholde I goo bounde in the sprete vnto Ierusalem and knowe not what shall come on me there
Sasa, sikilizeni! Mimi, nikiwa ninamtii Roho, nakwenda Yerusalemu bila kufahamu yatakayonipata huko.
23 but that the holy goost witnesseth in every cite sayinge: yt bondes and trouble abyde me.
Ninachojua tu ni kwamba Roho Mtakatifu ananithibitishia katika kila mji kwamba vifungo na mateso ndivyo vinavyoningojea.
24 But none of tho thinges move me: nether is my lyfe dere vnto my selfe that I myght fulfill my course wt ioye and the ministracio which I have receaved of ye Lorde Iesu to testify the gospell of ye grace of god.
Lakini, siuthamini uhai wangu kuwa ni kitu sana kwangu. Nataka tu nikamilishe ule utume wangu na kumaliza ile kazi aliyonipa Bwana Yesu niifanye, yaani nitangaze Habari Njema ya neema ya Mungu.
25 And now beholde I am sure yt hence forth ye all (thorow who I have gone preachinge ye kyngdome of God) shall se my face no moore.
“Nimekuwa nikienda huko na huko kati yenu nikiuhubiri Ufalme wa Mungu. Sasa lakini, najua hakuna hata mmoja wenu atakayeniona tena.
26 Wherfore I take you to recorde this same daye that I am pure fro the bloude of all me.
Hivyo, leo hii ninawathibitishieni rasmi kwamba ikijatokea akapotea mmoja wenu, mimi sina lawama yoyote.
27 For I have kepte nothinge backe: but have shewed you all the counsell of God.
Kwa maana sikusita hata kidogo kuwatangazieni azimio lote la Mungu.
28 Take hede therfore vnto youre selves and to all the flocke wherof the holy goost hath made you oversears to rule the congregacion of God which he hath purchased with his bloud.
Jihadharini wenyewe; lilindeni lile kundi ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi muwe walezi wake. Lichungeni kanisa la Mungu ambalo amejipatia kwa damu ya Mwanae.
29 For I am sure of this that after my departynge shall greveous wolves entre in amonge you which will not spare the flocke.
Nafahamu vizuri sana kwamba baada ya kuondoka kwangu mbwa mwitu wakali watawavamieni, na hawatakuwa na huruma kwa kundi hilo.
30 Moreover of youre awne selves shall men aryse speakinge perverse thinges to drawe disciples after the.
Hata kutoka miongoni mwenu watatokea watu ambao watasema mambo ya uongo ili kuwapotosha watu na kuwafanya wawafuate wao tu.
31 Therfore awake and remember that by the space of. iii. yeares I ceased not to warne every one of you both nyght and daye with teares.
Kwa hiyo, muwe macho mkikumbuka kwamba kwa muda wa miaka mitatu, usiku na mchana, sikuchoka kumwonya kila mmoja wenu kwa machozi.
32 And now brethren I comende you to God and to the worde of his grace which is able to bylde further and to geve you an inheritaunce amoge all them which are sanctified.
“Na sasa basi, ninawaweka ninyi chini ya ulinzi wa Mungu na ujumbe wa neema yake. Yeye anao uwezo wa kuwajenga ninyi na kuwawezesha mzipate zile baraka alizowawekea watu wake.
33 I have desyred no mas silver golde or vesture.
Mimi sikutamani hata mara moja fedha, wala dhahabu, wala nguo za mtu yeyote.
34 Ye knowe well yt these hondes have ministred vnto my necessities and to them that were wt me.
Mnajua ninyi wenyewe kwamba nimefanya kazi kwa mikono yangu mwenyewe, ili kujipatia mahitaji yangu na ya wenzangu.
35 I have shewed you all thinges how that so laborynge ye ought to receave the weake and to remember the wordes of the Lorde Iesu howe that he sayde: It is more blessed to geve then to receave.
Nimekuwa nikiwapeni daima mfano kwamba kwa kufanya kazi mithili hiyo tunapaswa kuwasaidia walio dhaifu, tukikumbuka maneno ya Bwana Yesu mwenyewe: Heri zaidi kutoa kuliko kupokea.”
36 When he had thus spoken he kneled doune and prayed with them all.
Baada ya kusema hayo, Paulo alipiga magoti pamoja nao wote, akasali.
37 And they wept all aboundantly and fell on Pauls necke and kissed him
Wote walikuwa wanalia; wakamwaga kwa kumkumbatia na kumbusu.
38 sorowinge most of all for the wordes which he spake that they shuld se his face no moore. And they acompanyed him vnto the shyppe.
Jambo lililowahuzunisha zaidi lilikuwa neno alilosema kwamba hawangemwona tena. Basi, wakamsindikiza hadi melini.

< Acts 20 >