< Acts 19 >

1 It fortuned whyll Appollo was at Corinthum that Paul passed thorow the vpper costes and came to Ephesus and foude certayne disciples
Wakati Apolo alipokuwa Korintho, Paulo alisafiri sehemu za bara, akafika Efeso ambako aliwakuta wanafunzi kadhaa.
2 and sayd vnto them: have ye receaved the holy gost sence ye beleved? And they sayde vnto him: no we have not hearde whether ther be eny holy goost or no.
Akauliza, “Je, mlipopata kuwa waumini mlipokea Roho Mtakatifu?” Nao wakamjibu, “La! Hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatujasikia.”
3 And he sayd vnto them: wher wt were ye then baptised? And they sayd: with Iohns baptim
Naye akasema, “Sasa mlipata ubatizo wa namna gani?” Wakamjibu, “Ubatizo wa Yohane.”
4 Then sayde Paul: Iohn verely bapiised with the baptim of repentaunce sayinge vnto the people that they shuld beleve on him which shuld come after him: that is on Christ Iesus.
Naye Paulo akasema, “Ubatizo wa Yohane ulikuwa wa kuonyesha kwamba watu wametubu. Yohane aliwaambia watu wamwamini yule ambaye alikuwa anakuja baada yake, yaani Yesu.”
5 When they hearde that they were baptised in the name of the lorde Iesu.
Baada ya kusikia hayo, walibatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
6 And Paul layde his hondes apon them and the holy gost came on them and they spake with tonges and prophesied
Basi, Paulo akawawekea mikono, na Roho Mtakatifu akawashukia, wakaanza kusema lugha mbalimbali na kutangaza ujumbe wa Mungu.
7 and all the men were aboute. xii.
Wote jumla, walikuwa watu wapatao kumi na wawili.
8 And he went into the synagoge and behaved him selfe boldely for the space of thre monethes disputynge and gevynge them exhortacions of the kyngdome of God.
Kwa muda wa miezi mitatu Paulo alikuwa akienda katika sunagogi, akawa na majadiliano ya kuvutia sana juu ya Ufalme wa Mungu.
9 When dyvers wexed harde herted and beleved not but spake evyll of the waye and that before the multitude: he departed from them and seperated the disciples. And disputed dayly in ye scole of one called Tyranus.
Lakini wengine walikuwa wakaidi, wakakataa kuamini, wakaanza kuongea vibaya hadharani juu ya Njia ya Bwana. Hapo Paulo alivunja uhusiano nao, akawachukua pembeni wale wanafunzi wake, akawa anazungumza nao kila siku katika jumba la masomo la Turano.
10 And this contynued by the space of two yeares: so yt all they which dwelt in Asia hearde the worde of the lorde Iesu bothe Iewes and Grekes.
Aliendelea kufanya hivyo kwa muda wa miaka miwili hata wakazi wote wa Asia, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, wakaweza kusikia neno la Bwana.
11 And god wrought no small miracles by the hondes of Paul:
Mungu alifanya miujiza ya ajabu kwa mikono ya Paulo.
12 so that from his body were brought vnto the sicke napkyns or partlettes and the diseases departed from the and the evyll spretes went out of them.
Watu walikuwa wakichukua leso na nguo nyingine za kazi ambazo Paulo alikuwa amezitumia, wakazipeleka kwa wagonjwa, nao wakaponywa magonjwa yao; na wale waliokuwa na pepo wabaya wakatokwa na pepo hao.
13 Then certayne of the vagabounde Iewes exorcistes toke apon them to call over them which had evyll spretes the name of the lorde Iesus sayinge: We adiure you by Iesu who Paul preacheth.
Wayahudi kadhaa wenye kupunga pepo wabaya, walisafiri huko na huko, wakijaribu kulitumia jina la Bwana Yesu kwa wale waliokuwa wamepagawa na pepo wabaya. Walikuwa wakisema: “Ninawaamuru kwa jina la Yesu ambaye Paulo anamhubiri.”
14 And ther were seven sonnes of one Sceva a Iewe and chefe of the prestes which dyd so.
Watoto saba wa Skewa, Kuhani Mkuu wa Kiyahudi, walikuwa miongoni mwa hao waliokuwa wanafanya hivyo.
15 And the evyll sprete answered and sayde: Iesus I knowe and Paul I knowe: but who are ye?
Lakini pepo mbaya aliwajibu, “Ninamfahamu Yesu, ninamjua pia Paulo, lakini ninyi ni nani?”
16 And ye man in who the evyll sprete was ranne on the and overcame the and prevayled agaynst them so that they fledde out of that housse naked and wouded.
Kisha yule mtu aliyepagawa aliwarukia wote kwa kishindo, akawashinda nguvu. Na hao watoto wa Skewa wakakimbia kutoka ile nyumba wakiwa uchi na wamejaa majeraha.
17 And this was knowen to all ye Iewes and Grekes also which dwelt at Ephesus and feare came on them all and they magnified the name of ye lorde Iesus.
Kila mtu huko Efeso, Myahudi na asiye Myahudi, alisikia juu ya tukio hilo. Wote waliingiwa na hofu, wakalitukuza jina la Bwana Yesu.
18 And many yt beleved came and confessed and shewed their workes.
Waumini wengi walijitokeza wakakiri hadharani mambo waliyokuwa wametenda.
19 Many of the which vsed curious craftes brought their bokes and burned the before all men and they counted the price of the and foude it fifty thousande silverlynges.
Wengine waliokuwa wameshughulikia mambo ya uchawi hapo awali, walikusanya vitabu vyao, wakavichoma mbele ya wote. Walikisia gharama ya vitabu hivyo, wakaona yafikia vipande vya fedha elfu hamsini.
20 So myghtely grewe ye worde of god and prevayled.
Kwa namna hiyo, neno la Bwana lilizidi kuenea na kuwa na nguvu zaidi.
21 After these thinges were ended Paul purposed in the sprete to passe over Macedonia and Achaia and to goo to Ierusalem saying: After I have bene there I must also se Rome.
Baada ya mambo hayo, Paulo aliamua kwenda Yerusalemu kwa kupitia Makedonia na Akaya. Alisema, “Baada ya kufika huko, itanilazimu kuona Roma pia.”
22 So sent he into Macedonia two of the that ministred vnto him Timotheus and Erastus: but he him selfe remayned in Asia for a season.
Hivyo, aliwatuma wawili wa wasaidizi wake, Timotheo na Erasto, wamtangulie kwenda Makedonia, naye akabaki kwa muda huko Asia.
23 The same tyme ther arose no lytell a do aboute that waye.
Wakati huo ndipo kulipotokea ghasia kubwa huko Efeso kwa sababu ya hiyo Njia ya Bwana.
24 For a certayne man named Demetrius a silvermyth which made silver schrynes for Diana was not a lytell beneficiall vnto the craftes men.
Kulikuwa na mfua fedha mmoja aitwaye Demetrio, ambaye alikuwa na kazi ya kutengeneza sanamu za nyumba ya mungu wa kike aitwaye Artemi. Shughuli hiyo iliwapatia mafundi faida kubwa.
25 Which he called to geder with the worke men of lyke occupacion and sayd: Syrs ye knowe that by this crafte we have vauntage.
Demetrio aliwakusanya hao wafanyakazi pamoja na wengine waliokuwa na kazi kama hiyo, akawaambia, “Wananchi, mnafahamu kwamba kipato chetu kinatokana na biashara hii.
26 Moreover ye se and heare that not alone at Ephesus but almost thorowe oute all Asia this Paul hath persuaded and turned awaye moche people saying yt they be not goddes which are made wt hondes.
Sasa, mnaweza kusikia na kujionea wenyewe mambo Paulo anayofanya, si tu hapa Efeso, ila pia kote katika Asia. Yeye amewashawishi na kuwageuza watu wakakubali kwamba miungu ile iliyotengenezwa na watu si miungu hata kidogo.
27 So that not only this oure crafte cometh into parell to be set at nought: but also that ye temple of ye greate goddas Diana shuld be despysed and her magnificence shuld be destroyed which all Asia and the worlde worshippeth.
Hivyo iko hatari kwamba biashara yetu itakuwa na jina baya. Si hivyo tu, bali pia jambo hilo linaweza kuifanya nyumba ya mungu Artemi kuwa si kitu cha maana. Hatimaye sifa zake huyo ambaye Asia na dunia yote inamwabudu, zitakwisha.”
28 When they hearde these sayinges they were full of wrathe and cryed out saying: Greate is Diana of the Ephesians.
Waliposikia hayo, waliwaka hasira, wakaanza kupiga kelele: “Mkuu ni Artemi, wa Efeso!”
29 And all the cite was on a roore and they russhed in to the comen hall with one assent and caught Gayus and Aristarcus men of Macedonia Pauls companios.
Mji wote ukajaa ghasia. Wakawavamia Gayo na Aristarko, wenyeji wa Makedonia, ambao walikuwa wasafiri wenzake Paulo, wakakimbia nao mpaka kwenye ukumbi wa michezo.
30 When Paul wolde have entred in vnto the people ye disciples suffered him not.
Paulo mwenyewe alitaka kuukabili huo umati wa watu, lakini wale waumini walimzuia.
31 Certayne also of ye chefe of Asia which were his frendes sent vnto him desyrynge him that he wolde not preace into the comen hall.
Maofisa wengine wa huo mkoa wa Asia, waliokuwa rafiki zake, walimtumia Paulo ujumbe wakimsihi asijihatarishe kwa kwenda kwenye ukumbi wa michezo.
32 Some cryed one thinge and some another and the congregacion was all out of quiet and ye moare parte knewe not wherfore they were come togeder.
Wakati huo, kila mtu alikuwa anapayuka; wengine hili na wengine lile, mpaka hata ule mkutano ukavurugika. Wengi hawakujua hata sababu ya kukutana kwao.
33 Some of the company drue forth Alexander the Iewes thrustynge him forwardes. Alexander beckened with the honde and wolde have geven ye people an answer.
Kwa vile Wayahudi walimfanya Aleksanda ajitokeze mbele, baadhi ya watu katika ule umati walidhani kuwa ndiye. Basi, Aleksanda aliwaashiria watu kwa mkono akitaka kujitetea mbele ya ule umati wa watu.
34 When they knewe ye he was a Iewe ther arose a shoute almost for the space of two houres of all men cryinge greate is Diana of the Ephesians.
Lakini walipotambua kuwa yeye ni Myahudi, wote kwa sauti moja walipiga kelele: “Mkuu ni Artemi wa Efeso!” Wakaendelea kupayukapayuka hivyo kwa muda wa saa mbili.
35 When the toune clarcke had ceased the people he sayd: ye men of Ephesus what man is it that knoweth not how that the cite of the Ephesians is a worshipper of the great goddas Diana and of ye ymage which came fro heven.
Hatimaye karani wa mji alifaulu kuwanyamazisha, akawaambia, “Wananchi wa Efeso, kila mtu anajua kwamba mji huu wa Efeso ni mlinzi wa nyumba ya mungu Artemi na mlinzi wa ile sanamu iliyoanguka kutoka mbinguni.
36 Seinge then yt no man sayth here agaynst ye ought to be content and to do nothinge rasshly:
Hakuna anayeweza kukana mambo haya. Hivyo basi, tulieni; msifanye chochote bila hadhari.
37 For ye have brought hyther these me whiche are nether robbers of churches nor yet despisers of youre goddes.
Mmewaita watu hawa hapa ingawaje hawakuikufuru nyumba ya mungu wala kumtukana mungu wetu wa kike.
38 Wherfore yf Demetrius and the craftes men which are wt him have eny sayinge to eny man the lawe is open and ther are ruelars let the accuse one another.
Kama, basi Demetrio na wafanyakazi wake wana mashtaka yao kuhusu watu hawa, yapo mahakama na wakuu wa mikoa; wanaweza kushtakiana huko.
39 Yf ye goo about eny other thinge it maye be determined in a lawfull cogregacion
Kama mna matatizo mengine, yapelekeni katika kikao halali.
40 For we are in ieoperdy to be accused of this dayes busines: for as moche as ther is no cause wherby we maye geve a rekenynge of this concourse of people.
Kwa maana tungaliweza kushtakiwa kwa kusababisha ghasia kutokana na vituko vya leo. Ghasia hii haina msingi halali na hatungeweza kutoa sababu za kuridhisha za ghasia hiyo.”
41 And when he had thus spoken he let the congregacion departe.
Baada ya kusema hayo aliuvunja mkutano.

< Acts 19 >