< Acts 21 >

1 And it chaunsed that assone as we had launched forth and were departed from them we came with a strayght course vnto Choon and the daye folowinge vnto the Rhodes and from thence vnto Patara.
Tulipokwisha agana nao, tulipanda meli tukaenda moja kwa moja mpaka Kosi. Kesho yake tulifika Rodo, na kutoka huko tulikwenda Patara.
2 And we founde a shippe redy to sayle vnto Phenices and went a borde and set forthe.
Huko, tulikuta meli iliyokuwa inakwenda Foinike, hivyo tulipanda, tukasafiri.
3 Then appered vnto vs Cyprus and we lefte it on the lefte honde and sayled vnto Syria and came vnto Tyre. For there the shyppe vnladed her burthen.
Baada ya kufika mahali ambapo tuliweza kuona Kupro, tulipitia upande wake wa kusini tukaelekea Siria. Tulitia nanga katika mji wa Tiro ambapo ile meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
4 And when we had founde brethren we taryed there. vii. dayes. And they tolde Paul thorowe ye sprete that he shuld not goo vp to Ierusalem.
Tulikuta waumini huko, tukakaa pamoja nao kwa muda wa juma moja. Waumini hao wakawa waongea kwa nguvu ya Roho, wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu.
5 And when the dayes were ended we departed and went oure wayes and they all brought vs on oure waye wt their wyves and chyldren tyll we were come out of the cyte. And we kneled doune in the shore and prayde.
Lakini muda wetu ulipokwisha tuliondoka. Wote pamoja na wanawake na watoto wao walitusindikiza mpaka nje ya mji. Tulipofika pwani, sote tulipiga magoti tukasali.
6 And when we had taken oure leave one of another we toke shyppe and they returned home agayne.
Kisha tuliagana; sisi tukapanda meli nao wakarudi makwao.
7 When we had full ended the course fro Tyre we aryved at Ptolomaida and saluted the brethren and abode with the one daye.
Sisi tuliendelea na safari yetu kutoka Tiro tukafika Tolemai ambapo tuliwasalimu ndugu zetu, tukakaa nao siku moja.
8 The nexte daye we that were of Pauls copany departed and came vnto Cesarea. And we entred into the housse of Philip ye Evagelist which was one of the seve deacones and abode with him.
Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisarea. Huko Kaisarea tulikwenda nyumbani kwa mhubiri Filipo. Yeye alikuwa mmoja wa wale saba waliochaguliwa kule Yerusalemu.
9 The same man had fower doughters virges which dyd prophesy.
Alikuwa na binti watatu ambao walikuwa na kipaji cha unabii.
10 And as we taried there a good many dayes there came a certayne prophete from Iurie named Agabus.
Baada ya kukaa huko siku kadhaa, nabii mmoja aitwaye Agabo alifika kutoka Yudea.
11 When he was come vnto vs he toke Pauls gerdell and bounde his hondes and fete and sayde: thus saith the holy goost: so shall ye Iewes at Ierusalem bynde the man yt oweth this gerdell and shall delyver him into the hondes of the gentyls.
Alitujia, akachukua mkanda wa Paulo, akajifunga mikono na miguu, akasema “Roho Mtakatifu asema hivi: Wayahudi kule Yerusalemu watamfunga namna hii mtu mwenye ukanda na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa.”
12 When we hearde this both we and other of the same place besought him that he wolde not goo vp to Ierusalem.
Tuliposikia hayo, sisi na wale watu wengine waliokuwa hapo tulimsihi Paulo asiende Yerusalemu.
13 Then Paul answered and sayde: what do ye wepynge and breakinge myne hert? I am redy not to be bound only but also to dye at Ierusalem for ye name of ye Lorde Iesu.
Lakini yeye alijibu, “Mnataka kufanya nini? Mnataka kuvunja moyo wangu kwa machozi? Niko tayari siyo tu kutiwa ndani kule Yerusalemu, ila hata kufa kwa ajili ya Bwana Yesu.”
14 When we coulde not turne his mynde we ceased sayinge: the will of ye Lorde be fulfilled.
Tuliposhindwa kumshawishi tulinyamaza, tukasema tu: “Mapenzi ya Bwana yafanyike”
15 After those dayes we made oure selfes redy and went vp to Ierusalem.
Baada ya kukaa pale kwa muda, tulifunga mizigo yetu, tukaendelea na safari kwenda Yerusalemu.
16 There went with vs also certayne of his disciples of Cesarea and brought with them one Mnason of Cyprus an olde disciple with whom we shuld lodge.
Wengine kati ya wale wafuasi wa Kaisarea walienda pamoja nasi, wakatupeleka nyumbani kwa Mnasoni ambaye tulikuwa tunakwenda kukaa naye kwa muda. Mnasoni alikuwa mwenyeji wa Kupro na alikuwa amekuwa muumini kwa siku nyingi.
17 And when we were come to Ierusalem the brethren receaved vs gladly.
Tulipofika Yerusalemu, ndugu waumini walitupokea vizuri sana.
18 And on the morowe Paul wet in with vs vnto Iames. And all the elders came to geder.
Kesho yake Paulo alikwenda pamoja nasi kumwamkia Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwako pia.
19 And when he had saluted them he tolde by order all thinges that God had wrought amoge the getyls by his ministracion.
Baada ya kuwasalimu, Paulo aliwapa taarifa kamili kuhusu yote Mungu aliyokuwa ametenda kati ya mataifa kwa njia ya utumishi wake.
20 And when they hearde it they glorified the Lorde and sayde vnto him: thou seist brother how many thousande Iewes ther are which beleve and they are all zelous over ye lawe.
Waliposikia hayo, walimtukuza Mungu. Kisha wakamwambia Paulo, “Ndugu, unaweza kuona kwamba kuna maelfu ya Wayahudi ambao sasa wamekuwa waumini na wote hao wanashika kwa makini Sheria ya Mose.
21 And they are informed of the that thou teachest all the Iewes which are amoge the gentyls to forsake Moses and sayst that they ought not to circumcise their chyldren nether to live after the customes.
Wamepata habari zako kwamba umekuwa ukiwafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa mengine kuwa wasiijali Sheria ya Mose, wasiwatahiri watoto wao na kwamba wasizifuate mila za Wayahudi.
22 What is it therfore? The multitude must nedes come togeder. For they shall heare that thou arte come.
Sasa, mambo yatakuwaje? Ni dhahiri kuwa watapata habari kwamba umekwisha wasili hapa.
23 Do therfore this that we saye to the. We have. iiii. men which have a vowe on them.
Basi, fanya kama tunavyokushauri. Tunao hapa watu wanne ambao wameweka nadhiri.
24 Them take and purifye thy selfe with them and do cost on them that they maye shave their heeddes and all shall knowe yt tho thinges which they have hearde concerninge the are nothinge: but that thou thy selfe also walkest and kepest the lawe.
Jiunge nao katika ibada ya kujitakasa, ukalipe na gharama zinazohusika, kisha wanyolewe nywele zao. Hivyo watu wote watatambua kwamba habari zile walizoambiwa juu yako hazina msingi wowote, na kwamba wewe binafsi bado unaishi kufuatana na maagizo ya Sheria za Mose.
25 For as touchinge the gentyls which beleve we have written and concluded yt they observe no soche thinges: but that they kepe them selves from thinges offred to ydoles from bloud fro strangled and fro fornicacion.
Kuhusu wale watu wa mataifa mengine ambao wamekuwa waumini, tumekwisha wapelekea barua tukiwaambia mambo tuliyoamua: wasile chochote kilichotambikiwa miungu ya uongo, wasinywe damu, wasile nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati.”
26 Then the nexte daye Paul toke the men and purified him selfe with them and entred into the teple declaringe that he observed the dayes of ye purificacio vntyll that an offeringe shuld be offred for every one of them.
Basi, kesho yake Paulo aliwachukua wale watu akafanya ibada ya kujitakasa pamoja nao. Kisha akaingia Hekaluni kutoa taarifa kuhusu mwisho wa siku za kujitakasa na kuhusu dhabihu itakayotolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
27 And as the seven dayes shuld have bene ended ye Iewes which were of Asia when they sawe him in the teple they moved all the people and layde hondes on him
Wakati siku hizo saba zilipokaribia kuisha, Wayahudi waliokuwa wametoka katika mkoa wa Asia walimwona Paulo Hekaluni. Wakachochea hasira kati ya kundi lote la watu, wakamtia nguvuni
28 cryinge: men of Israel helpe. This is the man that teacheth all men every where agaynst the people and the lawe and this place. Moreover also he hath brought Grekes into the teple and hath polluted this holy place.
wakipiga kelele: “Wananchi wa Israeli, msaada, msaada! Huyu ndiye yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo yanayopinga watu wa Israeli, yanayopinga Sheria ya Mose na mahali hapa patakatifu. Hata sasa amewaingiza watu wa mataifa mengine Hekaluni na kupatia najisi mahali hapa patakatifu.”
29 For they sawe one Trophimus an Ephesian with him in the cyte. Him they supposed Paul had brought into the teple.
Sababu ya kusema hivyo ni kwamba walikuwa wamemwona Trofimo mwenyeji, wa Efeso, akiwa pamoja na Paulo mjini, wakadhani kwamba Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.
30 And all the cyte was moved and the people swarmed to geder. And they toke Paul and drue him out of the teple and forthwith the dores were shut to.
Mji wote ulienea ghasia; watu wakaja kutoka pande zote, wakamkamata Paulo, wakamburuta, wakamtoa nje ya Hekalu na papo hapo milango ya Hekalu ikafungwa.
31 As they went about to kyll him tydinges came vnto the hye captayne of the soudiers that all Ierusalem was moved.
Walikuwa tayari kumuua, lakini habari zilimfikia mkuu wa jeshi la Kiroma kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
32 Which immediatly toke soudiers and vndercaptaynes and ranne doune vnto them. When they sawe ye vpper captayne and the soudiers they lefte smytinge of Paul.
Mara, mkuu wa jeshi akawachukua askari na jemadari, akalikabili lile kundi la watu. Nao walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
33 Then the captayne came neare and toke him and comaunded him to be bounde with two chaynes and demaunded what he was and what he had done.
Mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamtia nguvuni na kuamuru afungwe minyororo miwili. Kisha akauliza, “Ni mtu gani huyu, na amefanya nini?”
34 And one cryed this another that amoge the people. And whe he coulde not knowe the certayntie for ye rage he comaunded him to be caryed into the castle.
Wengine katika lile kundi la watu walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kitu kingine. Kwa sababu ya ghasia hiyo, mkuu wa jeshi hakufaulu kujua kisa kamili. Hivyo, aliamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome.
35 And whe he came vnto a grece it fortuned that he was borne of the soudiers of the violence of the people.
Paulo alipofika kwenye ngazi, askari walilazimika kumbeba kwa sababu ya fujo za watu.
36 For the multitude of the people folowed after cryinge: awaye wt him.
Kwa maana kundi kubwa la watu walimfuata wakipiga kelele, “Muulie mbali!”
37 And as Paul shuld have bene caryed into the castle he sayde vnto the hye Captayne: maye I speake vnto the? Which sayde: canst thou speake Greke?
Walipokuwa wanamwingiza ndani ya ngome, Paulo alimwomba mkuu wa jeshi akisema, “Naweza kukwambia kitu?” Yule mkuu wa jeshi akamjibu, “Je unajua Kigiriki?
38 Arte not thou that Egypcian which before these dayes made an vproure and ledde out into the wildernes. iiii. thousande men that were mortherers?
Kwani wewe si yule Mmisri ambaye hivi majuzi alianzisha uasi na kuwaongoza majahili elfu nne hadi jangwani?”
39 But Paul sayde: I am a ma which am a Iewe of Tharsus a cite in Cicill a Citesyn of no vyle cite I beseche ye soffre me to speake vnto ye people.
Paulo akajibu, “Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia; mimi ni raia wa mji maarufu. Tafadhali, niruhusu niongee na watu.
40 When he had geve him licece Paul stode on ye steppes and beckned with the honde vuto the people and ther was made a greate silence. And he spake vnto the in ye Ebrue tonge sayinge:
Yule mkuu wa jeshi akamruhusu. Hivyo Paulo alisimama juu ya ngazi, akawapungia mkono wale watu na walipokaa kimya, akaanza kuongea nao kwa Kiebrania.

< Acts 21 >