< Romans 16 >

1 I Commende vnto you Phebe our sister, which is a seruaunt of the Church of Cenchrea:
Napenda kumtambulisha kwenu dada yetu Foibe, mtumishi katika kanisa la Kenkrea.
2 That ye receiue her in the Lord, as it becommeth Saintes, and that ye assist her in whatsoeuer businesse she needeth of your ayde: for she hath giuen hospitalitie vnto many, and to me also.
Naomba mpokeeni katika Bwana ipasavyo watakatifu na kumpa msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, kwa maana yeye amekuwa msaada kwa watu wengi, mimi nikiwa miongoni mwao.
3 Greete Priscilla, and Aquila my fellowe helpers in Christ Iesus,
Wasalimuni Prisila na Akila, watumishi wenzangu katika Kristo Yesu.
4 (Which haue for my life laide downe their owne necke. Vnto whom not I onely giue thankes, but also all the Churches of the Gentiles.)
Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu; wala si mimi tu ninayewashukuru bali pia makanisa yote ya watu wa Mataifa.
5 Likewise greete the Church that is in their house. Salute my beloued Epenetus, which is the first fruites of Achaia in Christ.
Lisalimuni pia kanisa linalokutana nyumbani mwao. Msalimuni rafiki yangu mpendwa Epaineto, aliyekuwa mtu wa kwanza kumwamini Kristo huko Asia.
6 Greete Marie which bestowed much labour on vs.
Msalimuni Maria, aliyefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
7 Salute Andronicus and Iunia my cousins and fellowe prisoners, which are notable among the Apostles, and were in Christ before me.
Wasalimuni Androniko na Yunia, jamaa zangu ambao wamekuwa gerezani pamoja nami. Wao ni maarufu miongoni mwa mitume, nao walikuwa katika Kristo kabla yangu.
8 Greete Amplias my beloued in the Lord.
Msalimuni Ampliato, yeye nimpendaye katika Bwana.
9 Salute Vrbanus our fellow helper in Christ, and Stachys my beloued.
Msalimuni Urbano, mtendakazi mwenzetu katika Kristo, pamoja na rafiki yangu mpendwa Stakisi.
10 Salute Apelles approoued in Christ. Salute them which are of Aristobulus friendes.
Msalimuni Apele aliyejaribiwa na akaithibitisha imani yake katika Kristo. Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Aristobulo.
11 Salute Herodion my kinsman. Greete them which are of the friendes of Narcissus which are in the Lord.
Msalimuni ndugu yangu Herodioni. Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Narkisi walio katika Bwana.
12 Salute Tryphena and Tryphosa, which women labour in the Lord. Salute the beloued Persis, which woman hath laboured much in the Lord.
Wasalimuni Trifaina na Trifosa, wale wanawake wanaofanya kazi kwa bidii katika Bwana. Msalimuni rafiki yangu mpendwa Persisi, mwanamke mwingine aliyefanya kazi kwa bidii katika Bwana.
13 Salute Rufus chosen in the Lord, and his mother and mine.
Msalimuni Rufo, mteule katika Bwana, pamoja na mama yake, ambaye amekuwa mama kwangu pia.
14 Greete Asyncritus, Phlegon, Hermas, Patrobas, Mercurius, and the brethren which are with them.
Wasalimuni Asinkrito, Flegoni, Herme, Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.
15 Salute Philologus and Iulias, Nereas, and his sister, and Olympas, and all the Saintes which are with them.
Wasalimuni Filologo, Yulia, Nerea na dada yake, na Olimpa na watakatifu wote walio pamoja nao.
16 Salute one another with an holy kisse. The Churches of Christ salute you.
Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa busu takatifu. Makanisa yote ya Kristo yanawasalimu.
17 Now I beseech you brethren, marke them diligently which cause diuision and offences, contrary to the doctrine which ye haue learned, and auoide them.
Ndugu zangu, nawasihi mjihadhari na kujiepusha na wale watu waletao matengano na kuweka vikwazo mbele yenu dhidi ya mafundisho mliyojifunza.
18 For they that are such, serue not the Lord Iesus Christ, but their owne bellies, and with faire speach and flattering deceiue the heartes of the simple.
Kwa maana watu kama hao hawamtumikii Bwana Kristo, bali wanatumikia tamaa zao wenyewe. Kwa kutumia maneno laini na ya kubembeleza, hupotosha mioyo ya watu wajinga.
19 For your obedience is come abroade among all: I am glad therefore of you: but yet I woulde haue you wise vnto that which is good, and simple concerning euill.
Kila mtu amesikia juu ya utii wenu, nami nimejawa na furaha tele kwa ajili yenu. Lakini nataka mwe na hekima katika mambo mema na bila hatia katika mambo maovu.
20 The God of peace shall treade Satan vnder your feete shortly. The grace of our Lord Iesus Christ be with you.
Mungu wa amani atamponda Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu iwe nanyi. Amen.
21 Timotheus my helper, and Lucius, and Iason, and Sosipater my kinsemen, salute you.
Timotheo, mtendakazi mwenzangu anawasalimu. Vivyo hivyo Lukio, Yasoni, na Sosipatro, ndugu zangu.
22 I Tertius, which wrote out this Epistle, salute you in the Lord.
Mimi, Tertio, niliye mwandishi wa waraka huu, nawasalimu katika Bwana.
23 Gains mine hoste, and of the whole Church saluteth you. Erastus the steward of the citie saluteth you, and Quartus a brother.
Gayo, ambaye ni mwenyeji wangu na wa kanisa lote, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto ndugu yetu pia wanawasalimu. [
24 The grace of our Lord Iesus Christ be with you all. Amen.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi nyote. Amen.]
25 To him nowe that is of power to establish you according to my Gospel, and preaching of Iesus Christ, by the reuelation of the mysterie, which was kept secrete since the worlde began: (aiōnios g166)
Sasa atukuzwe yeye awezaye kuwafanya ninyi imara kwa Injili yangu na kuhubiriwa kwa Yesu Kristo, kutokana na kufunuliwa siri zilizofichika tangu zamani za kale. (aiōnios g166)
26 (But nowe is opened, and published among all nations by the Scriptures of the Prophetes, at the commandement of the euerlasting God for the obedience of faith) (aiōnios g166)
Lakini sasa siri hiyo imefunuliwa na kujulikana kupitia maandiko ya kinabii kutokana na amri ya Mungu wa milele, ili mataifa yote yaweze kumwamini na kumtii (aiōnios g166)
27 To God, I say, only wise, be praise through Iesus Christ for euer. Amen. ‘Written to the Romans from Corinthus, and sent by Phebe, seruaunt of the Church which is at Cenchrea.’ (aiōn g165)
Mungu aliye pekee, mwenye hekima, ambaye kwa njia ya Yesu Kristo utukufu ni wake milele na milele! Amen. (aiōn g165)

< Romans 16 >