< James 3 >

1 My brethren, be not many masters, knowing that we shall receiue the greater condemnation.
Ndugu zangu, msiwe walimu wengi, kwa maana mnafahamu kwamba sisi tufundishao tutahukumiwa vikali zaidi.
2 For in many things we sinne all. If any man sinne not in word, he is a perfect man, and able to bridle all the body.
Sisi sote tunajikwaa katika mambo mengi. Ikiwa mtu yeyote hakosei kamwe katika yale anayosema, yeye ni mkamilifu, naye anaweza kuuzuia pia na mwili wake wote.
3 Beholde, we put bittes into the horses mouthes, that they should obey vs, and we turne about all their bodie.
Tunapotia lijamu kwenye vinywa vya farasi ili kuwafanya watutii, tunaweza kuigeuza miili yao yote.
4 Behold also the shippes, which though they be so great, and are driuen of fierce windes, yet are they turned about with a very small rudder, whither soeuer the gouernour listeth.
Au angalia pia meli, ingawa ni kubwa sana, nazo huchukuliwa na upepo mkali, lakini hugeuzwa kwa usukani mdogo sana, kokote anakotaka nahodha.
5 Euen so the tongue is a litle member, and boasteth of great things: beholde, howe great a thing a litle fire kindleth.
Vivyo hivyo ulimi ni kiungo kidogo sana katika mwili, lakini hujivuna majivuno makuu. Fikirini jinsi moto mdogo unavyoweza kuteketeza msitu mkubwa!
6 And the tongue is fire, yea, a worlde of wickednesse: so is the tongue set among our members, that it defileth the whole body, and setteth on fire the course of nature, and it is set on fire of hell. (Geenna g1067)
Ulimi pia ni moto, ndio ulimwengu wa uovu kati ya viungo vya mwili. Ulimi huutia mwili wote wa mtu unajisi na kuuwasha moto mfumo mzima wa maisha yake, nao wenyewe huchomwa moto wa jehanamu. (Geenna g1067)
7 For the whole nature of beasts, and of birds, and of creeping things, and things of the sea is tamed, and hath bene tamed of the nature of man.
Kwa maana kila aina ya wanyama, ndege, wanyama watambaao na viumbe vya baharini vinafugika na vimefugwa na binadamu,
8 But the tongue can no man tame. It is an vnruly euill, full of deadly poyson.
lakini hakuna mtu awezaye kuufuga ulimi. Ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.
9 Therewith blesse we God euen the Father, and therewith curse we men, which are made after the similitude of God.
Kwa ulimi tunamhimidi Bwana, yaani Baba yetu, na kwa huo twawalaani watu walioumbwa kwa mfano wa Mungu.
10 Out of one mouth proceedeth blessing and cursing: my brethren, these things ought not so to be.
Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haistahili kuwa hivyo.
11 Doeth a fountaine send forth at one place sweete water and bitter?
Je, chemchemi yaweza kutoa katika tundu moja maji matamu na maji ya chumvi?
12 Can ye figge tree, my brethren, bring forth oliues, either a vine figges? so can no fountaine make both salt water and sweete.
Je, ndugu zangu, mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Wala chemchemi ya maji ya chumvi haiwezi kutoa maji matamu.
13 Who is a wise man and endued with knowledge among you? let him shew by good conuersation his workes in meekenesse of wisdome.
Ni nani aliye na hekima na ufahamu miongoni mwenu? Basi na aionyeshe hiyo kwa maisha yake mema na kwa matendo yake yaliyotendwa kwa unyenyekevu utokanao na hekima.
14 But if ye haue bitter enuying and strife in your hearts, reioyce not, neither be liars against the trueth.
Lakini ikiwa mna wivu na ni wenye chuki na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu kwa ajili ya hayo wala msiikatae kweli.
15 This wisedome descendeth not from aboue, but is earthly, sensuall, and deuilish.
Hekima ya namna hiyo haishuki kutoka mbinguni, bali ni ya kidunia, isiyo ya kiroho, na ya kishetani.
16 For where enuying and strife is, there is sedition, and all maner of euill workes.
Kwa maana panapokuwa na wivu na ubinafsi, ndipo penye machafuko na uovu wa kila namna.
17 But the wisedome that is from aboue, is first pure, then peaceable, gentle, easie to be intreated, full of mercie and good fruites, without iudging, and without hipocrisie.
Lakini hekima itokayo mbinguni kwanza ni safi, kisha inapenda amani, tena ni ya upole, iliyo tayari kusikiliza wengine kwa unyenyekevu, iliyojaa huruma na matunda mema, isiyopendelea mtu, tena isiyokuwa na unafiki.
18 And the fruite of righteousnesse is sowen in peace, of them that make peace.
Mavuno ya haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani.

< James 3 >