< Luke 12 >

1 In the meane time, there gathered together an innumerable multitude of people, so that they trode one another: and he began to say vnto his disciples first, Take heede to your selues of the leauen of the Pharises, which is hypocrisie.
Wakati huo, umati mkubwa wa watu maelfu, walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu akaanza kuzungumza kwanza na wanafunzi wake, akawaambia: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani, unafiki wao.
2 For there is nothing couered, that shall not bee reueiled: neither hidde, that shall not be knowen.
Hakuna jambo lolote lililositirika ambalo halitafunuliwa, au lililofichwa ambalo halitajulikana.
3 Wherefore whatsoeuer yee haue spoken in darkenesse, it shall be heard in the light: and that which ye haue spoken in the eare, in secret places, shall be preached on the houses.
Kwa hiyo, lolote mlilosema gizani litasikiwa nuruni. Na kile mlichonongʼona masikioni mkiwa kwenye vyumba vya ndani, kitatangazwa juu ya paa.
4 And I say vnto you, my friendes, be not afraide of them that kill the bodie, and after that are not able to doe any more.
“Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, lakini baada ya hilo hawawezi kufanya lolote zaidi.
5 But I wil forewarne you, who ye shall feare: feare him which after hee hath killed, hath power to cast into hell: yea, I say vnto you, him feare. (Geenna g1067)
Lakini nitawaambia nani wa kumwogopa: Mwogopeni yule ambaye baada ya kuua mwili, ana mamlaka ya kuwatupa motoni. Naam, nawaambia, mwogopeni huyo! (Geenna g1067)
6 Are not fiue sparowes bought for two farthings, and yet not one of them is forgotten before God?
Mnajua kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti mbili? Lakini Mungu hamsahau hata mmoja wao.
7 Yea, and all the heares of your head are nombred: feare not therefore: yee are more of value then many sparowes.
Naam, hata nywele za vichwa vyenu zote zimehesabiwa. Hivyo msiogope, kwa maana ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.
8 Also I say vnto you, Whosoeuer shall confesse mee before men, him shall the Sonne of man confesse also before the Angels of God.
“Ninawaambia kwamba yeyote atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri mbele za malaika wa Mungu.
9 But hee that shall denie mee before men, shall be denied before the Angels of God.
Lakini yeye atakayenikana mimi mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkana mbele ya malaika wa Mungu.
10 And whosoeuer shall speake a woorde against the Sonne of man, it shall be forgiuen him: but vnto him, that shall blaspheme ye holy Ghost, it shall not be forgiuen.
Naye kila atakayenena neno baya dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
11 And when they shall bring you vnto the Synagogues, and vnto the rulers and Princes, take no thought howe, or what thing ye shall answere, or what yee shall speake.
“Watakapowapeleka katika masinagogi, na mbele ya watawala na wenye mamlaka, msiwe na wasiwasi kuhusu namna mtakavyojitetea au mtakavyosema.
12 For the holy Ghost shall teache you in the same houre, what yee ought to say.
Kwa maana Roho Mtakatifu atawafundisha wakati huo huo mnachopaswa kusema.”
13 And one of the companie said vnto him, Master, bidde my brother deuide the inheritance with me.
Mtu mmoja katika umati wa watu akamwambia Yesu, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane naye urithi wetu.”
14 And he said vnto him, Man, who made me a iudge, or a deuider ouer you?
Lakini Yesu akamwambia, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi kuwa hakimu wenu au msuluhishi juu yenu?”
15 Wherefore he said vnto them, Take heede, and beware of couetousnesse: for though a man haue abundance, yet his life standeth not in his riches.
Ndipo Yesu akawaambia, “Jihadharini! Jilindeni na aina zote za choyo. Kwa maana maisha ya mtu hayatokani na wingi wa mali alizo nazo.”
16 And he put foorth a parable vnto them, saying, The grounde of a certaine riche man brought foorth fruites plenteously.
Kisha akawaambia mfano huu: “Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana.
17 Therefore he thought with himselfe, saying, What shall I doe, because I haue no roume, where I may lay vp my fruites?
Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Sina mahali pa kuhifadhi mavuno yangu.’
18 And he said, This wil I do, I wil pul downe my barnes, and builde greater, and therein will I gather all my fruites, and my goods.
“Ndipo huyo tajiri akasema, ‘Nitafanya hivi: Nitabomoa ghala zangu za nafaka na kujenga nyingine kubwa zaidi na huko nitayahifadhi mavuno yangu yote na vitu vyangu.
19 And I wil say to my soule, Soule, thou hast much goods laide vp for many yeeres: liue at ease, eate, drinke and take thy pastime.
Nami nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, unavyo vitu vingi vizuri ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi. Pumzika; kula, unywe, ufurahi.”’
20 But God said vnto him, O foole, this night wil they fetch away thy soule from thee: then whose shall those things be which thou hast prouided?
“Lakini Mungu akamwambia, ‘Mpumbavu wewe! Usiku huu uhai wako unatakiwa. Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’
21 So is he that gathereth riches to himselfe, and is not riche in God.
“Hivyo ndivyo ilivyo kwa wale wanaojiwekea mali lakini hawajitajirishi kwa Mungu.”
22 And he spake vnto his disciples, Therefore I say vnto you, Take no thought for your life, what yee shall eate: neither for your body, what yee shall put on.
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini.
23 The life is more then meate: and the body more then the raiment.
Maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
24 Consider the rauens: for they neither sowe nor reape: which neither haue storehouse nor barne, and yet God feedeth them: how much more are yee better then foules?
Fikirini ndege! Wao hawapandi wala hawavuni, hawana ghala wala popote pa kuhifadhi nafaka; lakini Mungu huwalisha. Ninyi ni wa thamani zaidi kuliko ndege!
25 And which of you with taking thought, can adde to his stature one cubite?
Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake?
26 If yee then bee not able to doe the least thing, why take yee thought for the remnant?
Kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini basi kuyasumbukia hayo mengine?
27 Consider the lilies howe they growe: they labour not, neither spin they: yet I say vnto you, that Salomon himselfe in all his royaltie was not clothed like one of these.
“Angalieni maua jinsi yameavyo: Hayafanyi kazi wala hayafumi. Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua.
28 If then God so clothe the grasse which is to day in the field, and to morowe is cast into the ouen, howe much more will he clothe you, O yee of litle faith?
Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo, na kesho yanatupwa motoni, si atawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba!
29 Therefore aske not what yee shall eate, or what ye shall drinke, neither hag you in suspense.
Wala msisumbuke mioyoni mwenu mtakula nini au mtakunywa nini. Msiwe na wasiwasi juu ya haya.
30 For all such things the people of the world seeke for: and your Father knoweth that ye haue neede of these things.
Watu wa mataifa ya duniani husumbuka sana kuhusu vitu hivi vyote, lakini Baba yenu anafahamu kuwa mnahitaji haya yote.
31 But rather seeke ye after the kingdome of God, and all these things shalbe cast vpon you.
Bali utafuteni Ufalme wa Mungu, na haya yote atawapa pia.
32 Feare not, litle flocke: for it is your Fathers pleasure, to giue you the kingdome.
“Msiogope enyi kundi dogo, kwa maana Baba yenu ameona vyema kuwapa ninyi Ufalme.
33 Sell that ye haue, and giue almes: make you bagges, which waxe not old, a treasure that can neuer faile in heauen, where no theefe commeth, neither mothe corrupteth.
Uzeni mali zenu mkawape maskini. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, mkajiwekee hazina mbinguni isiyokwisha, mahali ambapo mwizi hakaribii wala nondo haharibu.
34 For where your treasure is, there will your hearts be also.
Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo moyo wako utakapokuwa pia.
35 Let your loynes be gird about and your lights burning,
“Kuweni tayari mkiwa mmevikwa kwa ajili ya huduma na taa zenu zikiwa zinawaka,
36 And ye your selues like vnto men that waite for their master, when he will returne from the wedding, that when he commeth and knocketh, they may open vnto him immediatly.
kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka kwenye karamu ya arusi, ili ajapo na kubisha mlango waweze kumfungulia mara.
37 Blessed are those seruants, whom the Lord when he commeth shall finde waking: verely I say vnto you, he will girde himselfe about, and make them to sit downe at table, and will come forth, and serue them.
Heri wale watumishi ambao bwana wao atakapokuja atawakuta wakiwa wanakesha. Amin, nawaambia, atajifunga mkanda wake na kuwaketisha ili wale, naye atakuja na kuwahudumia.
38 And if he come in the seconde watch, or come in the third watch, and shall finde them so, blessed are those seruants.
Itakuwa heri kwa watumwa hao ikiwa bwana wao atakapokuja atawakuta wamekesha hata kama atakuja mnamo usiku wa manane, au karibu na mapambazuko.
39 Nowe vnderstand this, that if the good man of the house had knowen at what houre the theefe would haue come, he would haue watched, and would not haue suffered his house to be digged through.
Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angalijua saa mwizi atakuja, asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
40 Be ye also prepared therefore: for the Sonne of man will come at an houre when ye thinke not.
Ninyi nanyi hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.”
41 Then Peter saide vnto him, Master, tellest thou this parable vnto vs, or euen to all?
Ndipo Petro akamuuliza, “Bwana, mfano huu unatuambia sisi peke yetu au watu wote?”
42 And the Lord saide, Who is a faithfull steward and wise, whom the master shall make ruler ouer his householde, to giue them their portion of meate in season?
Yesu akamjibu, “Ni yupi basi wakili mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamfanya msimamizi juu ya watumishi wake wote, ili awape watumishi wengine chakula chao wakati unaofaa?
43 Blessed is that seruant, whom his master when he commeth, shall finde so doing.
Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
44 Of a trueth I say vnto you, that he wil make him ruler ouer all that he hath.
Amin nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote.
45 But if that seruant say in his heart, My master doeth deferre his comming, and ginne to smite the seruants, and maydens, and to eate, and drinke, and to be drunken,
Lakini kama yule mtumishi atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu anakawia kurudi,’ kisha akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, na kula na kunywa na kulewa.
46 The master of that seruant will come in a day when he thinketh not, and at an houre when he is not ware of, and will cut him off, and giue him his portion with the vnbeleeuers.
Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua. Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wale wasioamini.
47 And that seruant that knewe his masters will, and prepared not himselfe, neither did according to his will, shalbe beaten with many stripes.
“Yule mtumishi anayefahamu vyema mapenzi ya bwana wake na asijiandae wala kufanya kama apendavyo bwana wake, atapigwa kwa mapigo mengi.
48 But he that knewe it not, and yet did commit things worthy of stripes, shall be beaten with fewe stripes: for vnto whomsoeuer much is giuen, of him shalbe much required, and to whom men much commit, the more of him will they aske.
Lakini yeyote ambaye hakujua naye akafanya yale yastahiliyo kupigwa, atapigwa kidogo. Yeyote aliyepewa vitu vingi, atadaiwa vingi; na yeyote aliyekabidhiwa vingi, kwake vitatakiwa vingi.
49 I am come to put fire on the earth, and what is my desire, if it be already kindled?
“Nimekuja kuleta moto duniani; laiti kama ungekuwa tayari umewashwa!
50 Notwithstanding I must be baptized with a baptisme, and how am I grieued, till it be ended?
Lakini ninao ubatizo ambao lazima nibatizwe, nayo dhiki yangu ni kuu mpaka ubatizo huo ukamilike!
51 Thinke ye that I am come to giue peace on earth? I tell you, nay, but rather debate.
Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? La, nawaambia sivyo, nimekuja kuleta mafarakano.
52 For from hencefoorth there shall be fiue in one house deuided, three against two, and two against three.
Kuanzia sasa, kutakuwa na watu watano katika nyumba moja, watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
53 The father shalbe deuided against ye sonne, and the sonne against the father: the mother against the daughter, and the daughter against the mother: the mother in lawe against her daughter in lawe, and the daughter in lawe against her mother in lawe.
Watafarakana baba dhidi ya mwanawe na mwana dhidi ya babaye, mama dhidi ya bintiye na binti dhidi ya mamaye, naye mama mkwe dhidi ya mkwewe na mkwe dhidi ya mama mkwe wake.”
54 Then said he to the people, When ye see a cloude rise out of the West, straightway ye say, A shower commeth: and so it is.
Pia Yesu akauambia ule umati wa watu, “Mwonapo wingu likitokea magharibi, mara mwasema, ‘Mvua itanyesha,’ nayo hunyesha.
55 And when ye see the South winde blowe, ye say, that it wilbe hoate: and it commeth to passe.
Nanyi mwonapo upepo wa kusini ukivuma, ninyi husema, ‘Kutakuwa na joto,’ na huwa hivyo.
56 Hypocrites, ye can discerne the face of the earth, and of the skie: but why discerne ye not this time?
Enyi wanafiki! Mnajua jinsi ya kutambua kuonekana kwa dunia na anga. Inakuwaje basi kwamba mnashindwa kutambua wakati huu wa sasa?
57 Yea, and why iudge ye not of your selues what is right?
“Kwa nini hamwamui wenyewe lililo haki?
58 While thou goest with thine aduersarie to the ruler, as thou art in the way, giue diligence in the way, that thou mayest be deliuered from him, least he drawe thee to the iudge, and the iudge deliuer thee to the iayler, and the iayler cast thee into prison.
Uwapo njiani na mshtaki wako kwenda kwa hakimu, jitahidi kupatana naye mkiwa njiani. La sivyo, atakupeleka kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa afisa, naye afisa atakutupa gerezani.
59 I tell thee, thou shalt not depart thence, till thou hast payed the vtmost mite.
Nakuambia, hautatoka humo hadi uwe umelipa senti ya mwisho.”

< Luke 12 >