< 1 Corinthians 1 >

1 Paul called to be an Apostle of Iesus Christ, through the will of God, and our brother Sosthenes,
Paulo, niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mtume wa Kristo Yesu, na Sosthene ndugu yetu.
2 Vnto the Church of God, which is at Corinthus, to them that are sanctified in Christ Iesus, Saintes by calling, with all that call on the Name of our Lord Iesus Christ in euery place, both their Lord, and ours:
Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale waliotakaswa katika Kristo Yesu na walioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia Jina la Kristo Yesu Bwana wetu, aliye Bwana wao na wetu pia:
3 Grace be with you, and peace from God our Father, and from the Lord Iesus Christ.
Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
4 I thanke my God alwayes on your behalfe for the grace of God, which is giuen you in Iesus Christ,
Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Kristo Yesu.
5 That in all things ye are made rich in him, in all kinde of speach, and in all knowledge:
Kwa kuwa katika Kristo mmetajirishwa kwa kila hali, katika kusema kwenu na katika maarifa yenu yote,
6 As the testimonie of Iesus Christ hath bene confirmed in you:
kwa sababu ushuhuda wetu kumhusu Kristo ulithibitishwa ndani yenu.
7 So that ye are not destitute of any gift: wayting for the appearing of our Lord Iesus Christ.
Kwa hiyo hamkupungukiwa na karama yoyote ya kiroho wakati mnangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
8 Who shall also confirme you vnto the ende, that ye may be blamelesse, in the day of our Lord Iesus Christ.
Atawafanya imara mpaka mwisho, ili msiwe na hatia siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9 God is faithfull, by whom ye are called vnto the fellowship of his Sonne Iesus Christ our Lord.
Mungu ambaye mmeitwa naye ili mwe na ushirika na Mwanawe Yesu Kristo, Bwana wetu ni mwaminifu.
10 Nowe I beseeche you, brethren, by the Name of our Lord Iesus Christ, that ye all speake one thing, and that there be no dissensions among you: but be ye knit together in one mind, and in one iudgement.
Nawasihi ndugu zangu, katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi, ili pasiwepo na matengano katikati yenu na kwamba mwe na umoja kikamilifu katika nia na katika kusudi.
11 For it hath bene declared vnto me, my brethren, of you by them that are of the house of Cloe, that there are contentions among you.
Ndugu zangu, nimepata habari kutoka kwa baadhi ya watu wa nyumbani mwa Kloe kwamba kuna magomvi katikati yenu.
12 Nowe this I say, that euery one of you saith, I am Pauls, and I am Apollos, and I am Cephas, and I am Christs.
Maana yangu ni kwamba: Mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo”; mwingine, “Mimi ni wa Apolo”; mwingine, “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine, “Mimi ni wa Kristo.”
13 Is Christ deuided? was Paul crucified for you? either were ye baptized into the name of Paul?
Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye alisulubishwa kwa ajili yenu? Je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14 I thanke God, that I baptized none of you, but Crispus, and Gaius,
Nashukuru kwamba sikumbatiza mtu yeyote isipokuwa Krispo na Gayo.
15 Lest any should say, that I had baptized into mine owne name.
Kwa hiyo hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kwamba alibatizwa kwa jina langu.
16 I baptized also the houshold of Stephanas: furthermore knowe I not, whether I baptized any other.
(Naam, niliwabatiza pia watu wa nyumbani mwa Stefana. Lakini zaidi ya hao sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
17 For CHRIST sent me not to baptize, but to preache the Gospel, not with wisdome of wordes, lest the crosse of Christ should be made of none effect.
Kwa maana Kristo hakunituma ili kubatiza bali kuhubiri Injili; sio kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili msalaba wa Kristo usije ukakosa nguvu yake.
18 For that preaching of the crosse is to them that perish, foolishnesse: but vnto vs, which are saued, it is the power of God.
Kwa maana ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
19 For it is written, I will destroy the wisedome of the wise, and will cast away the vnderstanding of the prudent.
Kwa maana imeandikwa: “Nitaiharibu hekima ya wenye hekima, na kubatilisha akili ya wenye akili.”
20 Where is the wise? where is the Scribe? where is the disputer of this worlde? hath not God made the wisedome of this worlde foolishnesse? (aiōn g165)
Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu? (aiōn g165)
21 For seeing the worlde by wisedome knewe not God in the wisedome of GOD, it pleased God by the foolishnesse of preaching to saue them that beleeue:
Kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kwa hekima yake haukumjua yeye, ilimpendeza Mungu kuwaokoa wale walioamini kwa upuzi wa lile neno lililohubiriwa.
22 Seeing also that the Iewes require a signe, and the Grecians seeke after wisdome.
Wayahudi wanadai ishara za miujiza na Wayunani wanatafuta hekima.
23 But wee preach Christ crucified: vnto the Iewes, euen a stumbling blocke, and vnto the Grecians, foolishnesse:
Lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa: yeye kwa Wayahudi ni kikwazo na kwa Wayunani ni upuzi.
24 But vnto them which are called, both of the Iewes and Grecians, we preach Christ, the power of God, and the wisedome of God.
Lakini kwa wale ambao Mungu amewaita, Wayahudi na pia Wayunani, Kristo ndiye nguvu ya Mungu na pia hekima ya Mungu.
25 For the foolishnesse of God is wiser then men, and the weakenesse of God is stronger then men.
Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi kuliko hekima ya wanadamu, nao udhaifu wa Mungu una nguvu kuliko nguvu ya wanadamu.
26 For brethren, you see your calling, how that not many wise men after the flesh, not many mighty, not many noble are called.
Ndugu zangu, kumbukeni mlivyokuwa mlipoitwa. Kwa kipimo cha kibinadamu, si wengi wenu mliokuwa na hekima. Si wengi mliokuwa na ushawishi, si wengi mliozaliwa katika jamaa zenye vyeo.
27 But God hath chosen the foolish thinges of the world to confound the wise, and God hath chosen the weake thinges of the worlde, to confound the mightie things,
Lakini Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye hekima, Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye nguvu.
28 And vile things of the worlde and thinges which are despised, hath God chosen, and thinges which are not, to bring to nought thinges that are,
Alivichagua vitu vya chini na vinavyodharauliwa vya dunia hii, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko,
29 That no flesh shoulde reioyce in his presence.
ili mtu yeyote asijisifu mbele zake.
30 But ye are of him in Christ Iesus, who of God is made vnto vs wisedome and righteousnesse, and sanctification, and redemption,
Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanyika kwetu hekima itokayo kwa Mungu, yaani haki, na utakatifu na ukombozi.
31 That, according as it is written, Hee that reioyceth, let him reioyce in the Lord.
Hivyo, kama ilivyoandikwa: “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”

< 1 Corinthians 1 >