< Luka 12 >

1 Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
In the mean time, when there was gathered together an innumerable multitude of people, so that they trampled one upon another, he began to say to his disciples first of all, Beware ye of the leaven of the Pharisees, which is hypocrisy.
2 Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
For there is nothing covered, that shall not be revealed; neither hid, that shall not be known.
3 Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
Therefore whatever ye have spoken in darkness shall be heard in the light; and that which ye have spoken in the ear in closets shall be proclaimed upon the housetops.
4 “Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
And I say to you my friends, Be not afraid of them that kill the body, and after that have no more that they can do.
5 Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo. (Geenna g1067)
But I will forewarn you whom ye shall fear: Fear him, who after he hath killed hath power to cast into hell; yea, I say to you, Fear him. (Geenna g1067)
6 Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
Are not five sparrows sold for two farthings, and not one of them is forgotten before God?
7 Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
But even the very hairs of your head are all numbered. Fear not therefore: ye are of more value than many sparrows.
8 “Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
Also I say to you, Whoever shall confess me before men, him shall the Son of man also confess before the angels of God:
9 Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
But he that denieth me before men shall be denied before the angels of God.
10 “Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
And whoever shall speak a word against the Son of man, it shall be forgiven him: but to him that blasphemeth against the Holy Spirit it shall not be forgiven.
11 “Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
And when they bring you to the synagogues, and before magistrates, and powers, be not anxious how or what thing ye shall answer, or what ye shall say:
12 Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema.”
For the Holy Spirit shall teach you in the same hour what ye ought to say.
13 Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba.”
And one of the company said to him, Master, speak to my brother, that he divide the inheritance with me.
14 Yesu akamjibu, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?”
And he said to him, Man, who made me a judge or a divider over you?
15 Basi, akawaambia wote, “Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo.”
And he said to them, Take heed, and beware of covetousness: for a man’s life consisteth not in the abundance of the things which he possesseth.
16 Kisha akawaambia mfano: “Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
And he spoke a parable to them, saying, The ground of a certain rich man brought forth plentifully:
17 Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
And he thought within himself, saying, What shall I do, because I have no place where to store my fruits?
18 Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
And he said, This will I do: I will pull down my barns, and build greater; and there will I store all my fruits and my goods.
19 Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
And I will say to my soul, Soul, thou hast many goods laid up for many years; take thy ease, eat, drink, and be merry.
20 Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?”
But God said to him, Thou fool, this night thy soul shall be required of thee: then whose shall those things be, which thou hast provided?
21 Yesu akamaliza kwa kusema “Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu.”
So is he that layeth up treasure for himself, and is not rich toward God.
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
And he said to his disciples, Therefore I say to you, Be not anxious for your life, what ye shall eat; neither for the body, what ye shall put on.
23 Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
The life is more than food, and the body is more than raiment.
24 Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
Consider the ravens: for they neither sow nor reap; which neither have storehouse nor barn; and God feedeth them: how much more are ye better than the fowls?
25 Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
And which of you by being anxious can add to his stature one cubit?
26 Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
If ye then are not able to do that thing which is least, why are ye anxious for the rest?
27 Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
Consider the lilies how they grow: they toil not, they spin not; and yet I say to you, that Solomon in all his glory was not arrayed like one of these.
28 Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
If then God so clothe the grass, which is to day in the field, and to morrow is cast into the oven; how much more will he clothe you, O ye of little faith?
29 “Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
And seek ye not what ye shall eat, or what ye shall drink, neither be ye of doubtful mind.
30 Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
For all these things do the nations of the world seek after: and your Father knoweth that ye have need of these things.
31 Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
But rather seek ye the kingdom of God; and all these things shall be added to you.
32 “Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
Fear not, little flock; for it is your Father’s good pleasure to give you the kingdom.
33 Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
Sell what ye have, and give alms; provide yourselves bags which become not old, a treasure in the heavens that faileth not, where no thief approacheth, neither moth corrupteth.
34 Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
For where your treasure is, there will your heart be also.
35 “Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
Let your loins be girt, and your lamps burning;
36 muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
And ye yourselves like men that wait for their lord, when he will return from the wedding; that when he cometh and knocketh, they may open to him immediately.
37 Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
Blessed are those servants, whom the lord when he cometh shall find watching: verily I say to you, that he shall gird himself, and make them to sit down to eat, and will come forth and serve them.
38 Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
And if he shall come in the second watch, or come in the third watch, and find them so, blessed are those servants.
39 Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
And this know, that if the master of the house had known what hour the thief would come, he would have watched, and not have allowed his house to be broken into.
40 Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
Be ye therefore ready also: for the Son of man cometh at an hour when ye think not.
41 Petro akamwambia, “Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?”
Then Peter said to him, Lord, speakest thou this parable to us, or even to all?
42 Bwana akajibu, “Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
And the Lord said, Who then is that faithful and wise steward, whom his lord shall make ruler over his household, to give them their portion of food in due season?
43 Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
Blessed is that servant, whom his lord when he cometh shall find so doing.
44 Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
Truly I say to you, that he will make him ruler over all that he hath.
45 Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
But if that servant shall say in his heart, My lord delayeth his coming; and shall begin to beat the male and female servants, and to eat and drink, and to be drunk;
46 bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
The lord of that servant will come in a day when he looketh not for him, and at an hour when he is not aware, and will cut him in two, and will appoint him his portion with the unbelievers.
47 Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
And that servant, who knew his lord’s will, and prepared not himself, neither did according to his will, shall be beaten with many stripes.
48 Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
But he that knew not, and committed things worthy of stripes, shall be beaten with few stripes. For to whomever much is given, of him shall much be required: and to whom men have committed much, from him they will ask the more.
49 “Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
I am come to send fire on the earth; and what will I, if it is already kindled?
50 Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
But I have a baptism to be baptized with; and how am I constrained till it shall be accomplished!
51 Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
Suppose ye that I am come to give peace on earth? I tell you, Nay; but rather division:
52 Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
For from henceforth there shall be five in one house divided, three against two, and two against three.
53 Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake.”
The father shall be divided against the son, and the son against the father; the mother against the daughter, and the daughter against the mother; the mother in law against her daughter in law, and the daughter in law against her mother in law.
54 Yesu akayaambia tena makundi ya watu, “Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
And he said also to the people, When ye see a cloud rising in the west, immediately ye say, There cometh a shower; and so it is.
55 Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
And when ye see the south wind blowing, ye say, There will be heat; and it cometh to pass.
56 Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
Ye hypocrites, ye can discern the face of the sky and of the earth; but how is it that ye do not discern this time?
57 “Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
Yea, and why even of yourselves judge ye not what is right?
58 Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
When thou goest with thy adversary to the magistrate, as thou art in the way, give diligence that thou mayest be delivered from him; lest he drag thee before the judge, and the judge deliver thee to the officer, and the officer cast thee into prison.
59 Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho.”
I tell thee, thou shalt not depart from there, till thou hast paid the very last mite.

< Luka 12 >