< Marko 1 >

1 Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
The beginning of the gospel of Jesus Christ, the Son of God;
2 Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
As it is written in the prophets, Behold, I send my messenger before thy face, who shall prepare thy way before thee.
3 Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
The voice of one crying in the wilderness, Prepare ye the way of the Lord, make his paths straight.
4 Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
John was baptizing in the wilderness, and preaching the baptism of repentance for the remission of sins.
5 Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
And there went out to him all the land of Judaea, and they of Jerusalem, and were all baptized by him in the river Jordan, confessing their sins.
6 Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
And John was clothed with camel’s hair, and with a leather belt around his loins; and he ate locusts and wild honey;
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
And preached, saying, There cometh after me one mightier than I, the latchet of whose shoes I am not worthy to stoop down and loose.
8 Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
I indeed have baptized you in water: but he shall baptize you in the Holy Spirit.
9 Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
And it came to pass in those days, that Jesus came from Nazareth to Galilee, and was baptized by John in Jordan.
10 Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
And immediately coming up out of the water, he saw the heavens opened, and the Spirit like a dove descending upon him:
11 Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
And there came a voice from heaven, saying, Thou art my beloved Son, in whom I am well pleased.
12 Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
And immediately the Spirit driveth him into the wilderness.
13 akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
And he was there in the wilderness forty days, tempted by Satan; and was with the wild beasts; and the angels ministered to him.
14 Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
Now after John was put in prison, Jesus came into Galilee, preaching the gospel of the kingdom of God,
15 “Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
And saying, The time is fulfilled, and the kingdom of God is at hand: repent ye, and believe the gospel.
16 Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
Now as he was walking by the sea of Galilee, he saw Simon and Andrew his brother casting a net into the sea: for they were fishermen.
17 Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
And Jesus said to them, Come ye after me, and I will make you to become fishers of men.
18 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
And immediately they forsook their nets, and followed him.
19 Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
And when he had gone a little further from there, he saw James the son of Zebedee, and John his brother, who also were in the boat mending their nets.
20 Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
And immediately he called them: and they left their father Zebedee in the boat with the hired servants, and went after him.
21 Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
And they went into Capernaum; and immediately on the sabbath he entered into the synagogue, and taught.
22 Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
And they were astonished at his doctrine: for he taught them as one that had authority, and not as the scribes.
23 Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
And there was in their synagogue a man with an unclean spirit; and he cried out,
24 akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
Saying, Let us alone; what have we to do with thee, thou Jesus of Nazareth? art thou come to destroy us? I know thee who thou art, the Holy One of God.
25 Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
And Jesus rebuked him, saying, Hold thy peace, and come out of him.
26 Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
And when the unclean spirit had torn him, and cried with a loud voice, he came out of him.
27 Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
And they were all amazed, so that they questioned among themselves, saying, What thing is this? what new doctrine is this? for with authority he commandeth even the unclean spirits, and they obey him.
28 Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
And immediately his fame spread abroad throughout all the region surrounding Galilee.
29 Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
And immediately, when they had come out of the synagogue, they entered into the house of Simon and Andrew, with James and John.
30 Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
But the mother of Simon’s wife lay sick with a fever, and immediately they tell him of her.
31 Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
And he came and took her by the hand, and lifted her up; and immediately the fever left her, and she ministered to them.
32 Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
And at evening, when the sun had set, they brought to him all that were diseased, and them that were possessed with demons.
33 Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
And all the city was gathered together at the door.
34 Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
And he healed many that were sick with various diseases, and cast out many demons; and permitted not the demons to speak, because they knew him.
35 Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
And in the morning, rising a great while before day, he went out, and departed into a solitary place, and there prayed.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
And Simon and they that were with him followed after him.
37 Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
And when they had found him, they said to him, All men seek for thee.
38 Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
And he said to them, Let us go into the next towns, that I may preach there also: for this purpose have I come.
39 Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
And he preached in their synagogues throughout all Galilee, and cast out demons.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
And there came a leper to him, beseeching him, and kneeling down to him, and saying to him, If thou wilt, thou canst make me clean.
41 Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
And Jesus, moved with compassion, put forth his hand, and touched him, and saith to him, I will; be thou clean.
42 Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
And as soon as he had spoken, immediately the leprosy departed from him, and he was cleansed.
43 Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
And he strictly charged him, and immediately sent him away;
44 “Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
And saith to him, See thou say nothing to any man: but go, show thyself to the priest, and offer for thy cleansing those things which Moses commanded, for a testimony to them.
45 Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.
But he went out, and began to proclaim it freely, and to blaze abroad the matter, so that Jesus could no more openly enter into the city, but was without in desert places: and they came to him from every quarter.

< Marko 1 >