< Warumi 2 >

1 Kwa hiyo hauna udhuru, wewe uhukumuye, kwa maana katika yale uhukumuyo mwingine wajitia hatiani mwenyewe. Kwa maana wewe uhukumuye unafanya mambo yale yale.
C'est pourquoi tu es sans excuse, ô homme, quel que soit celui qui juge. Car dans ce que tu juges un autre, tu te condamnes toi-même. Car toi qui juges, tu pratiques les mêmes choses.
2 Lakini twajua kwamba hukumu ya Mungu ni ya kweli juu yao wafanyao mambo kama hayo.
Nous savons que le jugement de Dieu est conforme à la vérité contre ceux qui pratiquent de telles choses.
3 Lakini wewe tafakari hili, wewe ambaye unahukumu wale wanaotenda mambo hayo ingawa nawe unafanya mambo yayo hayo. Je utaepuka hukumu ya Mungu?
Penses-tu, ô homme qui juge ceux qui pratiquent de telles choses, et qui fais de même, que tu échapperas au jugement de Dieu?
4 Au unafikiri kidogo sana juu ya wingi wa wema wake, kuchelewa kwa adhabu yake, na uvumilivu wake? Je, hujui kwamba wema wake unapaswa kukuelekeza katika toba?
Ou bien méprises-tu les richesses de sa bonté, de sa longanimité et de sa patience, ne sachant pas que la bonté de Dieu vous conduit à la repentance?
5 Bali kwa kadiri ya ugumu wako na kwa moyo wako usio na toba wajiwekea mwenyewe akiba ya ghadhabu kwa siku ile ya ghadhabu, yaani, siku ile ya ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu.
Mais selon votre dureté et votre impénitence, vous vous réservez la colère au jour de la fureur, de la révélation et du juste jugement de Dieu,
6 Yeye atamlipa kila mtu kipimo sawa na matendo yake:
qui « rendra à chacun selon ses œuvres ».
7 kwa wale ambao kwa uthabiti wa matendo mema wametafuta sifa, heshima na kutokuharibika, atawapa uzima wa milele. (aiōnios g166)
à ceux qui, par la persévérance dans la bonne action, recherchent la gloire, l'honneur et l'incorruptibilité, la vie éternelle; (aiōnios g166)
8 Lakini kwa wale ambao ni wabinafsi, wasioitii kweli bali hutii dhuluma, ghadhabu na hasira kali itakuja.
mais à ceux qui se complaisent dans l'égoïsme et n'obéissent pas à la vérité, mais obéissent à l'injustice, il y aura de la colère, de l'indignation,
9 Mungu ataleta dhiki na shida juu ya kila nafsi ya binadamu aliyefanya uovu, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
de l'oppression et de l'angoisse sur toute âme d'homme qui fait le mal, au Juif d'abord, et aussi au Grec.
10 Lakini sifa, heshima na amani itakuja kwa kila mtu atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
Mais la gloire, l'honneur et la paix vont à tout homme qui fait le bien, au Juif d'abord, et aussi au Grec.
11 Kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu.
Car il n'y a pas de partialité chez Dieu.
12 Kwa maana kama vile wengi waliokosa pasipo sheria watapotea pasipo sheria, na kama vile wengi waliokosa kulingana na sheria watahukumiwa kwa sheria.
En effet, tous ceux qui ont péché sans la loi périront aussi sans la loi. Tous ceux qui ont péché sous la loi seront jugés par la loi.
13 Maana si wasikiaji wa sheria walio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale waitendao sheria watakaohesabiwa haki.
Car ce ne sont pas ceux qui écoutent la loi qui sont justes devant Dieu, mais ceux qui la mettent en pratique qui seront justifiés
14 Kwa maana watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanafanya kwa asili mambo ya sheria, wao, wamekuwa sheria kwa nafsi zao, ingawa wao hawana sheria.
(car lorsque les païens qui n'ont pas la loi font par nature les choses de la loi, ceux-là, n'ayant pas la loi, sont une loi pour eux-mêmes,
15 Kwa hili wanaonesha kwamba matendo yanayohitajika kwa mujibu wa sheria yameandikwa ndani ya mioyo yao. Dhamiri zao pia zinawashuhudia wao, na mawazo yao wenyewe ama huwashitaki au huwalinda wao wenyewe
en ce qu'ils montrent l'œuvre de la loi écrite dans leur cœur, leur conscience en rendant témoignage avec eux, et leurs pensées entre eux les accusant ou bien les excusant)
16 na pia kwa Mungu. Haya yatatokea katika siku ambayo Mungu atazihukumu siri za watu wote, sawasawa na injili yangu, kwa njia ya Yesu Kristo.
au jour où Dieu jugera les secrets des hommes, selon ma Bonne Nouvelle, par Jésus-Christ.
17 Tuseme kwamba unajiita mwenyewe Myahudi, aliyekaa katika sheria, shangilia kwa kujisifu katika Mungu,
En effet, tu portes le nom de Juif, tu te reposes sur la loi, tu te glorifies en Dieu,
18 yajue mapenzi yake, na kupima mambo ambayo yanatofautiana nayo, baada ya kuagizwa na sheria.
tu connais sa volonté, et tu approuves les choses excellentes, étant instruit par la loi,
19 Na tuseme kwamba una ujasiri kwamba wewe mwenyewe ni kiongozi wa kipofu, mwanga kwa wale walio gizani,
et tu as l'assurance d'être toi-même un guide des aveugles, une lumière pour ceux qui sont dans les ténèbres,
20 msahihishaji wa wajinga, mwalimu wa watoto, na kwamba unayo katika sheria jinsi ya elimu na kweli.
un correcteur des insensés, un éducateur de bébés, ayant dans la loi la forme de la connaissance et de la vérité.
21 Wewe basi, uhubiriye mwingine, je, hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kutokuiba, je wewe huiba?
Toi donc qui enseignes un autre, n'enseignes-tu pas toi-même? Toi qui prêches que l'homme ne doit pas voler, voles-tu?
22 Wewe usemae usizini, je unazini? Wewe uchukiaye sanamu, je unaiba hekaluni?
Vous qui dites que l'homme ne doit pas commettre d'adultère, commettez-vous l'adultère? Vous qui avez en horreur les idoles, pillez-vous les temples?
23 Wewe ujisifuye katika sheria, je haumfedheheshi Mungu katika kuvunja sheria?
Vous qui vous glorifiez de la loi, déshonorez-vous Dieu en désobéissant à la loi?
24 Kwa maana “jina la Mungu linafedheheshwa kati ya watu wa mataifa kwa sababu yenu,” kama ilivyoandikwa.
Car « le nom de Dieu est blasphémé parmi les païens à cause de vous », comme il est écrit.
25 Kwa maana Kutahiriwa kweli kwafaa kama ukitii sheria, lakini kama wewe ni mkiukaji wa sheria, kutahiriwa kwako kunakuwa kutokutahiriwa.
En effet, la circoncision est utile, si tu mets la loi en pratique; mais si tu transgresses la loi, ta circoncision est devenue incirconcision.
26 Basi, ikiwa, mtu asiyetahiriwa anaendelea kushika matakwa ya sheria, je kutokutahiriwa kwake hakutachukuliwa kana kwamba ametahiriwa?
Si donc l'incirconcis observe les ordonnances de la loi, son incirconcision ne sera-t-elle pas considérée comme une circoncision?
27 Na yeye asiyetahiriwa kwa asili hatakuhukumu kama akitimiza sheria? Hii ni kwa sababu una maandiko yaliyoandikwa na tohara pia lakini bado u mkiukaji wa sheria!
Ceux qui sont physiquement incirconcis, mais qui accomplissent la loi, ne te jugeront-ils pas, toi qui, avec la lettre et la circoncision, es un transgresseur de la loi?
28 Kwa maana yeye si Myahudi aliye kwa hali ya nje; wala kutahiriwa si kule ambako ni kwa nje tu katika mwili.
Car n'est pas Juif celui qui l'est extérieurement, ni la circoncision extérieure dans la chair;
29 Lakini yeye ni Myahudi aliye kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko. Sifa ya mtu wa namna hiyo haitokani na watu bali yatoka kwa Mungu.
mais est Juif celui qui l'est intérieurement, et la circoncision est celle du cœur, de l'esprit, non de la lettre, dont la louange ne vient pas des hommes, mais de Dieu.

< Warumi 2 >