< Warumi 1 >

1 Paulo, mtumishi wa Yesu Kristo, aliyeitwa kuwa mtume, na kutengwa kwa ajili ya Injili ya Mungu.
Paul, serviteur de Jésus-Christ, appelé à être apôtre, mis à part pour la Bonne Nouvelle de Dieu,
2 Hii ndio ile Injili aliyoiahidi zamani kupitia manabii wake katika maandiko matakatifu.
qu'il a promise auparavant par ses prophètes dans les saintes Écritures,
3 Ni kuhusu Mwana wake, aliyezaliwa kutoka ukoo wa Daudi kwa jinsi ya mwili.
concernant son Fils, né de la postérité de David selon la chair,
4 Yeye alitangazwa kwa Mwana wa Mungu kwa nguvu ya Roho ya utakatifu kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu.
déclaré Fils de Dieu avec puissance selon l'Esprit de sainteté, par la résurrection des morts, Jésus-Christ notre Seigneur,
5 Kupitia yeye tumepokea neema na utume kwa utii wa imani kati ya mataifa yote, kwa ajili ya jina lake.
par lequel nous avons reçu la grâce et l'apostolat pour l'obéissance de la foi parmi toutes les nations, à cause de son nom;
6 Kati ya mataifa haya, ninyi pia mmeitwa kuwa wa Yesu Kristo.
parmi lesquels vous êtes aussi appelés à appartenir à Jésus-Christ;
7 Barua hii ni kwa wote walioko Rumi, wapendwao na Mungu, walioitwa kuwa watu watakatifu. Neema na iwe kwenu, na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
à tous ceux qui sont à Rome, bien-aimés de Dieu, appelés à être saints: Grâce et paix à vous, de la part de Dieu notre Père et du Seigneur Jésus-Christ.
8 Kwanza, namshukuru Mungu wangu katika Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inahubiriwa katika dunia nzima.
D'abord, je rends grâce à mon Dieu par Jésus-Christ pour vous tous, de ce que votre foi est proclamée dans le monde entier.
9 Kwa maana Mungu ni shahidi wangu, ambaye ninamtumikia kwa roho yangu katika injili ya Mwana wake, jinsi ninavyodumu katika kuwataja.
Car Dieu m'est témoin, lui que je sers en esprit dans la Bonne Nouvelle de son Fils, combien sans cesse je fais mention de vous dans mes prières,
10 Daima naomba katika sala zangu kwamba kwa njia yoyote nipate mwishowe kuwa na mafanikio sasa kwa mapenzi ya Mungu katika kuja kwenu.
en demandant si, d'une manière ou d'une autre, la volonté de Dieu me permet enfin d'aller vers vous.
11 Maana natamani kuwaona, ili nipate kuwapa ninyi baadhi ya karama za rohoni, nipate kuwaimarisha.
Car je désire ardemment vous voir, afin de vous communiquer quelque don spirituel, pour que vous soyez affermis;
12 Yaani, natazamia kutiwa moyo pamoja nanyi, kwa njia ya imani ya kila mmoja wetu, yenu na yangu.
c'est-à-dire que je sois encouragé en vous, chacun de nous par la foi de l'autre, la vôtre et la mienne.
13 Sasa ndugu, sitaki mkose kufahamu kwamba, mara nyingi nimekusudia kuja kwenu, lakini nimezuiliwa mpaka sasa. Nilitaka hivi ili kuwa na matunda kwenu kama ilivyo pia miongoni mwa watu wa mataifa.
Or, je ne veux pas que vous ignoriez, frères, que j'ai souvent projeté de venir chez vous (et que j'en ai été empêché jusqu'ici), afin de porter du fruit parmi vous aussi, comme parmi le reste des païens.
14 Nadaiwa na Wayunani na wageni pia, werevu na wajinga.
J'ai une dette envers les Grecs et les étrangers, envers les sages et les insensés.
15 Kwa hiyo, kwa upande wangu, mimi niko tayari kutangaza injili kwenu pia ninyi mlio huko Roma.
Ainsi, autant qu'il est en moi, je suis impatient d'annoncer la Bonne Nouvelle à vous aussi qui êtes à Rome.
16 Kwa maana siionei haya injili, kwa kuwa ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza na kwa Myunani pia.
En effet, je n'ai pas honte de la Bonne Nouvelle du Christ, car elle est la puissance de Dieu pour le salut de quiconque croit, du Juif d'abord, et aussi du Grec.
17 Kwa maana haki ya Mungu imedhihirishwa kutoka imani hata imani, kama ilivyo andikwa, “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
Car en elle est révélée la justice de Dieu, de foi à foi. Comme il est écrit: « Le juste vivra par la foi. »
18 Maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi na uovu wote wa watu, ambao kwa njia ya udhalimu huificha kweli.
Car la colère de Dieu se révèle du ciel contre toute impiété et toute injustice des hommes qui suppriment la vérité dans l'injustice,
19 Hii ni kwa sababu, yote yanayoweza kujulikana juu ya Mungu ni wazi kwao. Maana Mungu amewafahamisha.
parce que ce qui est connu de Dieu est révélé en eux, car Dieu le leur a révélé.
20 Maana mambo yake yasioonekana vizuri yamekuwa wazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Yanaeleweka kupitia vitu vilivyoumbwa. Mambo haya ni uwezo wake wa milele na asili ya uungu. Matokeo yake, watu hawa hawana udhuru. (aïdios g126)
Car les choses invisibles de Dieu, depuis la création du monde, se voient clairement, étant perçues par les choses faites, même sa puissance éternelle et sa divinité, afin qu'ils soient sans excuse. (aïdios g126)
21 Hii ni kwa sababu, ingawa walijua kuhusu Mungu, hawakumtukuza yeye kama Mungu, wala hawakumpa shukrani. Badala yake, wamekuwa wapumbavu katika mawazo yao, na mioyo yao yenye ujinga ilitiwa giza.
Parce que, connaissant Dieu, ils ne l'ont pas glorifié comme Dieu, et n'ont pas rendu grâces, mais ils sont devenus vains dans leurs raisonnements, et leur cœur insensé s'est obscurci.
22 Walijiita kuwa ni werevu, lakini wakawa wajinga.
Se prétendant sages, ils sont devenus fous,
23 Waliubadili utukufu wa Mungu asie na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, ya wanyama wenye miguu minne, na ya viumbe vitambaavyo.
et ils ont échangé la gloire du Dieu incorruptible contre l'image de l'homme corruptible, des oiseaux, des quadrupèdes et des reptiles.
24 Kwa hiyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa za mioyo yao kwa uchafu, kwa miili yao kufedheheshwa baina yao.
C'est pourquoi Dieu les a livrés à l'impureté dans les convoitises de leur cœur, afin que leur corps soit déshonoré au milieu d'eux.
25 Ni wao walioibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, na ambao waliabudu na kutumikia viumbe badala ya Muumbaji, ambaye anasifiwa milele. Amina. (aiōn g165)
Ils ont changé la vérité de Dieu en mensonge, et ils ont adoré et servi la créature plutôt que le Créateur, qui est béni éternellement. Amen. (aiōn g165)
26 Kwa sababu hii, Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, kwa kuwa wanawake wao walibadilisha matumizi yao ya asili kwa kile kilicho kinyume na asili.
C'est pourquoi Dieu les a livrés à des passions infâmes. Car leurs femmes ont changé la fonction naturelle en ce qui est contre nature.
27 Hali kadhalika, wanaume pia wakaacha matumizi yao ya asili kwa wanawake na kuwakwa na tamaa dhidi yao wenyewe. Hawa walikuwa wanaume ambao walifanya na wanaume wenzao yasiyo wapasa, na ambao walipokea adhabu iliyostahili upotovu wao.
De même, les hommes, abandonnant la fonction naturelle de la femme, se sont enflammés dans leur convoitise les uns envers les autres, les hommes faisant ce qui est inconvenant avec les hommes, et recevant en eux-mêmes la peine due à leur erreur.
28 Kwa sababu walikataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wafanye mambo yale yasiyofaa.
De même qu'ils ont refusé d'avoir Dieu dans leur connaissance, Dieu les a livrés à un esprit réprouvé, pour qu'ils fassent ce qui ne convient pas;
29 Wamejawa na udhalimu wote, uovu, tamaa na ubaya. Wamejawa na wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu, na nia mbaya.
étant remplis de toute iniquité, d'immoralité sexuelle, de méchanceté, de cupidité, de malice; pleins d'envie, de meurtres, de querelles, de tromperies, de mauvaises habitudes, calomniateurs en secret,
30 Wao pia ni wasengenyaji, wasingiziaji, na wenye kumchukia Mungu. Wenye vurugu, kiburi, na majivuno. Wao ni watunga mabaya, na wasiotii wazazi wao.
médisants, odieux à Dieu, insolents, arrogants, fanfarons, inventeurs de malheurs, désobéissants à leurs parents,
31 Wao hawana ufahamu; wasioaminika, hawana mapenzi ya asili, na wasio na huruma.
sans intelligence, violateurs d'alliance, sans affection naturelle, impitoyables, sans miséricorde,
32 Wanaelewa kanuni za Mungu, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo wanastahili kifo. Lakini si tu wanafanya mambo hayo, wao pia wanakubaliana na wale wanaofanya mambo hayo.
qui, connaissant le décret de Dieu, selon lequel ceux qui pratiquent de telles choses méritent la mort, non seulement agissent de même, mais encore approuvent ceux qui les pratiquent.

< Warumi 1 >