< 1 Wakorintho 1 >

1 Paulo, aliyeitwa na Kristo Yesu kuwa mtume kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,
Paul, appelé à être apôtre de Jésus-Christ par la volonté de Dieu, et notre frère Sosthène,
2 kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale ambao wamewekwa wakfu katika Yesu Kristo, ambao wameitwa kuwa watu watakatifu. Tunawaandikia pia wale wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo katika mahali pote, Bwana wao na wetu.
à l'assemblée de Dieu qui est à Corinthe, à ceux qui sont sanctifiés en Jésus-Christ, appelés saints, avec tous ceux qui invoquent le nom de notre Seigneur Jésus-Christ, en tout lieu, chez eux et chez nous:
3 Neema na amani iwe kwenu kutoka kwa Mungu baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
Grâce et paix à vous, de la part de Dieu notre Père et du Seigneur Jésus-Christ.
4 Siku zote namshukru Mungu wangu kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu ambayo Kristo Yesu aliwapa.
Je rends toujours grâces à mon Dieu à votre sujet, pour la grâce de Dieu qui vous a été donnée en Jésus-Christ,
5 Amewafanya kuwa matajiri katika kila njia, katika usemi na pamoja maarifa yote.
afin que vous soyez enrichis en tout par lui, en toute parole et en toute connaissance,
6 Amewafanya matajiri, kama ushuhuda kuhusu Kristo ya kwamba amethibitishwa kuwa kweli miongoni mwenu.
comme le témoignage de Christ a été confirmé en vous,
7 Kwa hiyo hampungukiwi karama za kiroho, kama mlivyo na hamu ya kusubiri ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo.
afin que vous ne soyez en retard d'aucun don, dans l'attente de la révélation de notre Seigneur Jésus-Christ,
8 Atawaimarisha ninyi pia hadi mwisho, ili msilaumiwe siku ya Bwana wetu Yesu Kristo.
qui vous confirmera aussi jusqu'à la fin, irréprochables au jour de notre Seigneur Jésus-Christ.
9 Mungu ni mwaminifu ambaye aliwaita ninyi katika ushirika wa mwana wake, Yesu Kristo Bwana wetu.
Dieu est fidèle, celui par qui vous avez été appelés à la communion de son Fils, Jésus-Christ notre Seigneur.
10 Sasa nawasihi kaka na dada zangu, kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba wote mkubali, na kwamba kusiwe na migawanyiko miongoni mwenu. Nawasihi kwamba muungane pamoja katika nia moja na katika kusudi moja.
Or, je vous prie, frères, par le nom de notre Seigneur Jésus-Christ, de parler tous de la même chose, et qu'il n'y ait pas de divisions parmi vous, mais que vous soyez perfectionnés ensemble dans le même esprit et dans le même jugement.
11 Kwani watu wa nyumba ya Kloe wamenitaarifu kuwa kuna mgawanyiko unaoendelea miongoni mwenu.
Car il m'a été rapporté à votre sujet, mes frères, par ceux de la maison de Chloé, qu'il y a des disputes parmi vous.
12 Nina maana hii: Kila mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo,” au “Mimi ni wa Apolo”, au “Mimi ni wa Kefa” au “Mimi ni wa Kristo”.
Or, je veux dire que chacun de vous dit: « Je suis Paul », « Je suis Apollos », « Je suis Céphas », et « Je suis le Christ ».
13 Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulubiwa kwa ajili yenu? Je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Le Christ est-il divisé? Paul a-t-il été crucifié pour vous? Ou bien avez-vous été baptisé au nom de Paul?
14 Namshukuru Mungu kuwa sikumbatiza yeyote, isipokuwa Krispo na Gayo.
Je rends grâces à Dieu de ce que je n'ai baptisé aucun de vous, excepté Crispus et Gaïus,
15 Hii ilikuwa kwamba hakuna yeyote angesema mlibatizwa kwa jina langu.
afin que personne ne puisse dire que je vous ai baptisés en mon propre nom.
16 (Pia niliwabatiza wa nyumba ya Stephania. Zaidi ya hapo, sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote).
(J'ai aussi baptisé la maison de Stéphanas; en dehors d'eux, je ne sais pas si j'en ai baptisé d'autres).
17 Kwa kuwa, Kristo hakunituma kubatiza bali kuhubiri injili. Hakunituma kuhubiri kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili kwamba nguvu ya msalaba wa Kristo isiondolewe.
Car ce n'est pas pour baptiser que Christ m'a envoyé, mais pour annoncer la Bonne Nouvelle, sans sagesse de mots, afin que la croix de Christ ne soit pas annulée.
18 Kwa kuwa ujumbe wa msalaba ni upuuzi kwa wale wanaokufa. Lakini kwa wale ambao Mungu anawaokoa, ni nguvu ya Mungu.
Car la parole de la croix est une folie pour ceux qui meurent, mais pour nous qui sommes sauvés, elle est une puissance de Dieu.
19 Kwa kuwa imeandikwa, “Nitaiharibu hekima ya wenye busara. Nitauharibu ufahamu wa wenye akili.”
Car il est écrit, « Je détruirai la sagesse des sages. Je réduirai à néant le discernement de ceux qui savent discerner. »
20 Yuko wapi mtu mwenye busara? Yuko wapi mwenye elimu? Yuko wapi msemaji mshawishi wa dunia hii? Je, Mungu hakuigeuza hekima ya dunia hii kuwa ujinga? (aiōn g165)
Où est le sage? Où est le scribe? Où est le discoureur de ce siècle? Dieu n'a-t-il pas rendu insensée la sagesse de ce monde? (aiōn g165)
21 Tangu dunia imekuwa katika hekima yake haikumjua Mungu, ilimpendeza Mungu katika ujinga wao wa kuhubiri ili kuokoa wale wanaoamini.
En effet, puisque, dans la sagesse de Dieu, le monde n'a pas connu Dieu, Dieu a voulu, par la folie de la prédication, sauver ceux qui croient.
22 Kwa Wayahudi huuliza ishara za miujiza na kwa Wayunani hutafuta hekima.
Car les Juifs demandent des signes, les Grecs cherchent la sagesse,
23 Lakini tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa, aliye kikwazo kwa Wayahudi na ni ujinga kwa Wayunani.
mais nous, nous prêchons Christ crucifié, pierre d'achoppement pour les Juifs et folie pour les Grecs,
24 Lakini kwa wale ambao waliitwa na Mungu, Wayahudi na Wayunani, tunamhubiri Kristo kama nguvu na hekima ya Mungu.
mais pour ceux qui sont appelés, Juifs et Grecs, Christ est la puissance de Dieu et la sagesse de Dieu,
25 Kwa kuwa ujinga wa Mungu una hekima kuliko ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.
car la folie de Dieu est plus sage que les hommes, et la faiblesse de Dieu est plus forte que les hommes.
26 Angalia wito wa Mungu juu yenu, kaka na dada zangu. Si wengi wenu mlikuwa na hekima katika viwango vya kibinadamu. Si wengi wenu mlikuwa na nguvu. Si wengi wenu mlizaliwa katika ukuu.
Car vous voyez votre vocation, frères, qu'il n'y a pas beaucoup de sages selon la chair, ni beaucoup de puissants, ni beaucoup de nobles;
27 Lakini Mungu alichagua vitu vijinga vya dunia ili kuviaibisha vyenye hekima. Mungu alichagua kilicho dhaifu katika dunia kukiaibisha chenye nguvu.
mais Dieu a choisi les choses insensées du monde pour confondre les sages. Dieu a choisi les choses faibles du monde, pour couvrir de honte les choses fortes.
28 Mungu alichagua kile kilicho cha hali ya chini na kilichodharauliwa katika dunia. Alichagua hata vitu ambavyo havikuhesabiwa kuwa kitu, kwa kuvifanya si kitu vitu vilivyo na thamani.
Dieu a choisi les choses humbles du monde, les choses méprisées, les choses qui n'existent pas, afin de réduire à néant les choses qui existent,
29 Alifanya hivi ili asiwepo yeyote aliye na sababu ya kujivuna mbele zake.
pour que nulle chair ne se glorifie devant Dieu.
30 Kwa sababu ya kile Mungu alichofanya, sasa mko ndani ya Kristo Yesu, ambaye amefanyika hekima kwa ajili yetu kutoka kwa Mungu. Alikuwa haki yetu, utakatifu na ukombozi.
C'est à cause de lui que vous êtes en Jésus-Christ, qui a été fait pour nous sagesse de Dieu, justice, sanctification et rédemption,
31 Kama matokeo, kama andiko lisemavyo, “Anayejisifu, ajisifu katika Bwana.”
afin que, selon qu'il est écrit: « Que celui qui se glorifie se glorifie dans le Seigneur. »

< 1 Wakorintho 1 >