< Ufunuo 4 >

1 Baada ya mambo haya nilitazama, nikaona kuwa mlango ulikuwa umefunguliwa mbinguni. Ile sauti ya kwanza, ikizungumza nami kama tarumbeta, ikisema, “Njoo hapa, nitakuonesha yatakayotokea baada ya mambo haya.”
Après cela, je regardai et je vis une porte ouverte dans le ciel; et la première voix que j'entendis, comme une trompette qui me parlait, était une voix qui disait: « Monte ici, et je te montrerai ce qui doit arriver après cela. »
2 Mara moja nilikuwa katika Roho, niliona kulikuwa na kiti cha enzi kimewekwa mbinguni, na mtu amekikalia.
Aussitôt, je fus rempli d'Esprit. Et voici, il y avait un trône placé dans le ciel, et quelqu'un assis sur le trône
3 Mmoja aliyekuwa amekikalia alionekana kama jiwe la yaspi na akiki. Kulikuwa na upinde wa mvua umekizunguka kiti cha enzi. Upinde wa mvua ulionekana kama zumaridi.
qui ressemblait à une pierre de jaspe et à une sardoine. Il y avait un arc-en-ciel autour du trône, comme une émeraude à regarder.
4 Kukizunguka kiti cha enzi kulikuwa na viti vya enzi vingine ishirini na vinne, na waliokaa kwenye viti vya enzi walikuwa wazee ishirini na wanne, wamevikwa mavazi meupe na taji za dhahabu vichwani mwao.
Autour du trône, il y avait vingt-quatre trônes. Sur les trônes étaient assis vingt-quatre anciens, vêtus de vêtements blancs, avec des couronnes d'or sur la tête.
5 Kutoka katika kiti cha enzi kulitoka miale ya radi, muungurumo na radi. Taa saba zilikuwa zikiwaka mbele ya kiti cha enzi, taa ambazo ni roho saba za Mungu.
Du trône partent des éclairs, des sons et des tonnerres. Devant son trône brûlaient sept lampes de feu, qui sont les sept Esprits de Dieu.
6 Tena mbele ya kiti cha enzi kulikuwa na bahari, iliyowazi kama kioo. Wote kuzunguka kiti cha enzi kulikuwa na wenye uhai wanne, waliojaa macho mbele na nyuma.
Devant le trône était quelque chose comme une mer de verre, semblable à du cristal. Au milieu du trône, et autour du trône, il y avait quatre êtres vivants remplis d'yeux devant et derrière.
7 Kiumbe wa kwanza mwenye uhai alikuwa kama simba, kiumbe wa pili mwenye uhai alikuwa kama ndama, kiumbe wa tatu mwenye uhai alikuwa na uso kama wa mwanadamu, na yule mwenye uhai wa nne alikuwa kama tai apaaye.
Le premier être vivant était semblable à un lion, le deuxième être vivant était semblable à un veau, le troisième être vivant avait un visage d'homme, et le quatrième être vivant était semblable à un aigle qui vole.
8 Viumbe wenye uhai wanne kila mmoja alikuwa na mabawa sita, wamejaa macho juu na chini yake. Usiku na mchana hawakomi kusema, “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Bwana Mungu, mtawala juu ya wote, aliyekuwepo, na aliyepo na atakayekuja.”
Les quatre êtres vivants, qui ont chacun six ailes, sont pleins d'yeux autour et au-dedans. Ils n'ont de cesse, jour et nuit, de répéter: « Saint, saint, saint est le Seigneur Dieu, le Tout-Puissant, qui était, qui est et qui vient! »
9 Kila wakati viumbe wenye uhai walipotoa utukufu, heshima, na kushukuru mbele za aliyekuwa ameketi kwenye hicho kiti cha enzi, yeye aishiye milele na daima, (aiōn g165)
Lorsque les êtres vivants rendent gloire, honneur et louange à celui qui est assis sur le trône, à celui qui vit aux siècles des siècles, (aiōn g165)
10 wazee ishirini na wanne walisujudu wenyewe mbele yake aliyekikalia kiti cha enzi. Waliinama chini kwake aishiye milele na daima na kutupa chini taji zao mbele ya kiti cha enzi wakisema, (aiōn g165)
les vingt-quatre anciens se prosternent devant celui qui est assis sur le trône et adorent celui qui vit aux siècles des siècles, et ils jettent leurs couronnes devant le trône, en disant: (aiōn g165)
11 “Wastahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu. Kwa kuwa uliviumba vitu vyote, na kwa mapenzi yako, vilikuwepo na viliumbwa.”
« Tu es digne, Seigneur et Dieu, le Saint, de recevoir la gloire, l'honneur et la puissance, car c'est toi qui as créé toutes choses, et c'est par ta volonté qu'elles existent et qu'elles ont été créées. »

< Ufunuo 4 >