< Ufunuo 3 >

1 Kwa malaika wa kanisa la Sardi andika: 'Maneno ya yule anayeshikilia zile roho saba za Mungu na nyota saba. “Najua ambacho umefanya. Una sifa ya kuwa hai, lakini u-mfu.
« Et écris à l'ange de l'assemblée de Sardes: « Celui qui a les sept esprits de Dieu et les sept étoiles dit ces choses: « Je connais vos œuvres, que vous avez la réputation d'être vivants, mais que vous êtes morts.
2 Amka na kuimarisha yaliyosalia, lakini yako karibu kufa, kwa sababu sikuyaona matendo yako yamekamilika machoni pa Mungu wangu.
Réveillez-vous et fortifiez ce qui reste, ce que vous alliez jeter, car je n'ai trouvé aucune de vos œuvres parfaite devant mon Dieu.
3 Kwa hiyo, kumbuka, yale uliyoyapokea na kusikia. Yatii na kutubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwivi, na hutajua saa ipi nitakayokuja juu yako.
Rappelez-vous donc comment vous avez reçu et entendu. Gardez-le et repentez-vous. Si donc vous ne veillez pas, je viendrai comme un voleur, et vous ne saurez pas à quelle heure je viendrai sur vous.
4 Lakini kuna majina machache ya watu katika Sardi ambao hawakuchafua nguo zao. Watatembea pamoja nami, wamevaa nguo nyeupe, kwa sababu wanastahili.
Vous avez cependant à Sardes quelques noms qui n'ont pas souillé leurs vêtements. Ils marcheront avec moi en blanc, car ils en sont dignes.
5 Yeye ashindaye atavikwa mavazi meupe, na kamwe sitalifuta jina lake kutoka katika kitabu cha uzima, na nitalitaja jina lake mbele ya Baba yangu, na mbele ya malaika.
Celui qui vaincra sera revêtu de vêtements blancs, et je n'effacerai en aucune façon son nom du livre de vie, et je confesserai son nom devant mon Père et devant ses anges.
6 Ukiwa na sikio, sikiliza Roho ayaambiavyo makanisa.”
Que celui qui a des oreilles entende ce que l'Esprit dit aux assemblées.
7 “Kwa malaika wa kanisa la Philadefia andika: Maneno ya aliye mtakatifu na kweli - aliye na funguo za Daudi, hufungua na hakuna afungaye, hufunga na hakuna awezaye kufungua.
« Écris à l'ange de l'assemblée de Philadelphie: « Celui qui est saint, celui qui est vrai, celui qui a la clé de David, celui qui ouvre et personne ne peut fermer, et qui ferme et personne n'ouvre, dit ces choses:
8 Najua ambacho umetenda. Tazama, nimekuwekea mbele yako mlango uliofunguliwa ambao hakuna awezaye kuufunga. Najua unazo nguvu kidogo, lakini umelitii neno langu na hujalikana jina langu.
« Je connais tes œuvres (voici, j'ai mis devant toi une porte ouverte, que personne ne peut fermer), que tu as un peu de force, et que tu as gardé ma parole, et que tu n'as pas renié mon nom.
9 Angalia! Wote walio wa sinagogi la shetani, wale wasemao wao ni Wayahudi na kumbe siyo, badala yake wanadanganya. Nitawafanya waje na kusujudu mbele ya miguu yako, na watajua ya kuwa nilikupenda.
Voici que je fais venir quelques-uns de la synagogue de Satan, de ceux qui se disent Juifs et qui ne le sont pas, mais qui mentent, je les fais venir se prosterner à tes pieds, et savoir que je t'ai aimé.
10 Kwa kuwa umetunza amri yangu kwa uvumilivu wa uthabiti, nitakulinda pia katika saa yako ya kujaribiwa ambayo inakuja katika ulimwengu wote, kuwajaribu wale wote wanaoishi katika nchi.
Parce que tu as gardé mon commandement de persévérer, je te garderai aussi de l'heure de l'épreuve qui doit venir sur le monde entier, pour éprouver les habitants de la terre.
11 Naja upesi. Shikilia sana kile ulichonacho ili asiwepo mtu wa kuitwaa taji yako.
Je viens vite! Tenez fermement ce que vous avez, afin que personne ne prenne votre couronne.
12 Nitamfanya yeye ashindaye kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, na hatatoka nje kamwe. Nitaliandika kwake jina la Mungu wangu, jina la mji wa Mungu wangu (Yerusalemu mpya, ushukao chini toka mbinguni kwa Mungu wangu), na jina langu jipya.
Celui qui vaincra, je ferai de lui une colonne dans le temple de mon Dieu, et il n'en sortira plus. J'écrirai sur lui le nom de mon Dieu et le nom de la cité de mon Dieu, la nouvelle Jérusalem, qui descend du ciel d'auprès de mon Dieu, et mon nom nouveau.
13 Yeye aliye na sikio, na asikie ambacho Roho anasema kwa makanisa.'
Que celui qui a des oreilles entende ce que l'Esprit dit aux assemblées.
14 “Kwa malaika wa kanisa la Laodikia andika: 'Maneno yake aliye Amina, wakutegemewa na shahidi mwaminifu, mtawala juu ya uumbaji wa Mungu.
« Écris à l'ange de l'assemblée de Laodicée: « L'Amen, le témoin fidèle et véritable, le commencement de la création de Dieu, dit ces choses:
15 Najua ambacho umefanya, na kwamba wewe si baridi wala moto, natamani kwamba ungekuwa wa baridi au moto!
« Je connais tes œuvres: tu n'es ni froid ni chaud. Je voudrais que tu sois froid ou chaud.
16 Hivyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu, si moto wala baridi, nitakutapika utoke kinywani mwangu.
Ainsi, parce que vous êtes tièdes, et ni chauds ni froids, je vous vomirai de ma bouche.
17 Kwa kuwa unasema, “Mimi ni tajiri, nimekuwa na mali nyingi, na sihitaji chochote.” Lakini hujui kwamba wewe ni duni sana, wakuhuzunikiwa, maskini, kipofu na uchi.
Parce que vous dites: « Je suis riche, j'ai acquis des richesses, et je n'ai besoin de rien », et que vous ne savez pas que vous êtes des malheureux, des misérables, des pauvres, des aveugles et des nus.
18 Sikiliza ushauri kwangu: Nunua kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto ili upate kuwa tajiri, na nguo nyeupe za kumetameta ili ujivike mwenyewe na usioneshe aibu ya uchi wako, na mafuta ya kupaka katika macho yako upate kuona.
Je vous conseille d'acheter de moi de l'or purifié par le feu, afin de vous enrichir, et des vêtements blancs, afin que vous soyez vêtus et que la honte de votre nudité ne paraisse pas, et un collyre pour oindre vos yeux, afin que vous voyiez.
19 Kila nimpendaye, namwelekeza na kuwafundisha namna iwapasavyo kuishi; kwa hiyo, kuwa mkweli na kutubu.
Tous ceux que j'aime, je les reprends et les châtie. Soyez donc zélés, et repentez-vous.
20 Tazama nasimama katika mlango na kubisha. Yeyote asikiaye sauti yangu na kufungua mlango, nitakuja na kuingia nyumbani kwake, na kula chakula naye na yeye pamoja nami.
Voici, je me tiens à la porte et je frappe. Si quelqu'un entend ma voix et ouvre la porte, j'entrerai chez lui, je souperai avec lui, et lui avec moi.
21 Yeye ashindaye, nitampa haki ya kukaa chini pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi nilivyoshinda na kukaa chini pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
Celui qui vaincra, je lui donnerai de s'asseoir avec moi sur mon trône, comme moi aussi j'ai vaincu et me suis assis avec mon Père sur son trône.
22 Yeye aliye na sikio, na asikilize ambacho Roho ayaambia makanisa.”
Que celui qui a des oreilles entende ce que l'Esprit dit aux assemblées. »

< Ufunuo 3 >