< Zaburi 94 >

1 Yahwe, Ee Mungu ulipaye kisasi, Mungu ulipaye kisasi, utuangazie sisi.
¡Oh Yavé, ʼEL vengador! ¡Oh ʼEL vengador, resplandece!
2 Inuka, muhukumu wa nchi, uwape wenye majivuno kile wanachosahili.
¡Levántate, oh Juez de la tierra, Da la recompensa a los soberbios!
3 Mpaka lini waovu, Yahwe, mpaka lini waovu watafurahia?
¿Hasta cuándo los perversos, oh Yavé, Hasta cuándo se gozarán los perversos?
4 Wanamwaga maneno yao ya kiburi; wote watendao uovu wanajivuna.
Parlotean insolencias, hablan arrogancias. Se jactan todos los que cometen perversidad.
5 Wanawaangamiza watu wako, Yahwe; wanalitesa taifa ambao ni milki yako.
A tu pueblo quebrantan, oh Yavé. Oprimen a tu heredad.
6 Wanamuua mjane na mgeni aishiye nchini mwao, na wanamuua yatima.
Asesinan a la viuda y al extranjero, Y matan a los huérfanos.
7 Nao husema, “Yahwe hawezi kuona, Mungu wa Yakobo hayagundui haya.”
Y dicen: El YA no ve, Ni discierne el ʼElohim de Jacob.
8 Tambueni, ninyi watu wajinga! Enyi wapumbavu, mtajifunza lini?
Entiendan ustedes, necios del pueblo. ¿Cuándo entenderán ustedes los fatuos?
9 Yeye aliye liumba sikio, hasikii? Yeye aliye litengeneza jicho, haoni?
El que hizo el oído, ¿no escucha? El que formó el ojo, ¿no mira?
10 Yeye awaadhibuye mataifa, hayuko sahihi? Yeye ndiye ampaye maarifa mwanadamu.
El que amonesta a las naciones, ¿no reprenderá? El que enseña al hombre el saber, ¿no sabrá?
11 Yahwe anayajua mawazo ya wanadamu, kuwa ni mvuke.
Yavé conoce los pensamientos del hombre, Que son vanidad.
12 Amebarikiwa yule ambaye umuongozaye, Yahwe, yule ambaye wewe humfundisha kutoka katika sheria yako.
¡Inmensamente feliz es el varón a quien Tú, oh YA, disciplinas, Y a quien Tú enseñas tu Ley!
13 Wewe humpa pumziko wakati wa shida mpaka shimo litakapokuwa limechimbwa kwa ajili ya waovu.
Para darle descanso en los días de adversidad Mientras se cava una fosa para los perversos.
14 Maana Yahwe hatawaacha watu wake wala kutelekeza warithi wake.
Porque Yavé no abandonará a su pueblo, Ni desamparará a su heredad.
15 Kwa kuwa tena hukumu itakuwa ya haki; na wote walio wanyoofu wa moyo wataifuata.
Porque el juicio volverá a ser justo, Y todos los rectos de corazón lo seguirán.
16 Ni nani atainuka kunitetea dhidi ya watendao uovu? Ni nani atasimama dhidi ya waovu kwa ajili yangu?
¿Quién se levantará por mí contra los malhechores? ¿Quién se mantendrá en pie por mí contra los que practican perversidad?
17 Kama Yahwe asingelikuwa msaada wangu, haraka ningekuwa nimelala mahali pa ukimya.
Si Yavé no me ayuda, Pronto mi alma moraría en el silencio.
18 Niliposema, mguu wangu unateleza,” Uaminifu wa agano lako, Yahwe, uliniinua.
Si yo digo: ¡Mi pie resbala! Tu misericordia, oh Yavé, me sostendrá.
19 Wasiwasi uwapo mwingi ndani yangu, faraja yako hunifurahisha.
Cuando mis inquietudes se multiplican dentro de mí, Tus consolaciones deleitan mi alma.
20 Kiti cha uharibifu chaweza kushirikiana nawe, kitungacho madhara kwa njia ya sheria?
¿Se aliará contigo el trono de iniquidad Que por medio de decretos cometa agravios?
21 Wao kwa pamoja hupanga njama kuwaua wenye haki na kuwahukumu adhabu ya kifo wenye haki.
Conspiran juntos contra la vida del justo Y condenan a muerte al inocente.
22 Lakini Yahwe amekuwa mnara wangu mrefu, na Mungu wangu amekuwa mwamba wa kimbilio langu.
Pero Yavé fue mi Fortaleza, Y mi ʼElohim, la Roca de mi refugio.
23 Yeye atawarudishia uovu wao wenyewe na atawaangamiza katika uovu wao wenyewe. Yahwe Mungu wetu atawaangamiza.
Él devolverá sobre ellos su iniquidad Y los destruirá en su maldad. Yavé nuestro ʼElohim los destruirá.

< Zaburi 94 >