< Zaburi 50 >

1 Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
El poderoso ʼEL, ʼElohim, Yavé habló Y convocó a la tierra desde el oriente hasta el occidente.
2 Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
Desde Sion, perfección de hermosura, ʼElohim resplandeció.
3 Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
Que venga nuestro ʼElohim, y no en silencio. Un fuego devorador lo precede, Y alrededor de Él ruge una gran tempestad.
4 Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
Desde lo alto convoca a los cielos Y a la tierra para juzgar a su pueblo:
5 Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
Júntenme a mis santos, Los que hicieron un Pacto conmigo con sacrificio.
6 Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
Los cielos proclamarán su justicia, Porque ʼElohim es el Juez. (Selah)
7 Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
Escucha, pueblo mío, y hablaré. Testificaré contra ti, Israel. Yo soy ʼElohim, el ʼElohim tuyo.
8 Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
No te reprendo por tus sacrificios. Tus ofrendas encendidas están siempre delante de Mí.
9 Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
No aceptaré becerros de tu casa, Ni machos cabríos de tus corrales.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
Porque mía es toda bestia del bosque Y los ganados sobre 1.000 colinas.
11 Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
Conozco todas las aves de las montañas, Y todo lo que se mueve en el campo es mío.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
Si tuviera hambre, No te lo diría a ti, Porque mío es el mundo y todo lo que contiene.
13 Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
¿Yo como carne de becerros? ¿Bebo sangre de machos cabríos?
14 Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
Ofrece a ʼElohim sacrificio de acción de gracias. Paga a ʼElyón tus votos.
15 Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
Invócame en el día de la angustia. Te libraré, Y tú me honrarás.
16 Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
al perverso ʼElohim dice: ¿Qué derecho tienes tú para recitar mis Estatutos, Y tomar mi Pacto en tu boca?
17 wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
Porque tú aborreces la corrección, Y das tu espalda a mis Palabras.
18 Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
Si ves a un ladrón, te complaces con él, Y te asocias con los adúlteros.
19 Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
Permites que tu boca se pierda en lo malo, Y tu lengua trama el engaño.
20 Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
Te sientas, hablas contra tu hermano, Y difamas al hijo de tu propia madre.
21 Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
Estas cosas hiciste, Y Yo callé. Pensaste que Yo soy como tú. Pero te reprenderé y las expondré delante de tus ojos.
22 Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
Entiendan esto, los que se olvidan de ʼEloah, No sea que los quebrante sin que haya quien los libre.
23 Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”
El que ofrece sacrificio de acción de gracias me honra, Y al que ordena rectamente su camino Le mostraré la salvación de ʼElohim.

< Zaburi 50 >