< Zaburi 49 >

1 Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
Oigan esto, pueblos todos, Escuchen todos los habitantes del mundo,
2 wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
Tanto los humildes como los de alto nivel, Ricos y pobres juntamente.
3 Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
Mi boca hablará sabiduría, Y la meditación de mi corazón entendimiento.
4 Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
Inclinaré al proverbio mi oído. Declararé con el arpa mi dicho.
5 Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
¿Por qué tengo que temer en días de adversidad Cuando me rodea la iniquidad de mis adversarios,
6 Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
Que confían en la abundancia de sus posesiones, Y se jactan de sus inmensas riquezas?
7 Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
Ninguno de ellos puede de algún modo redimir al hermano, Ni pagar su rescate a ʼElohim.
8 Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
Porque la redención de su vida es costosa, Y nunca será suficiente,
9 Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
Para que viva eternamente Y jamás pase a corrupción.
10 Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
Porque ve que aun los sabios mueren Igual como perecen el ignorante y el necio, Y dejan a otros sus riquezas.
11 Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
Su íntima aspiración es que sus casas sean eternas, Sus moradas, por todas las generaciones. A sus tierras dan sus nombres.
12 Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
Pero el hombre no permanecerá con honra. Es como las bestias que perecen.
13 Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
Esta es la senda de los necios, Y de aquellos que tras ellos aprueban sus palabras. (Selah)
14 Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol h7585)
Como un rebaño están destinados al Seol, La muerte los pastorea. Los rectos se enseñorearán de ellos por la mañana, Se consumirá su buen parecer, Y el Seol será su morada. (Sheol h7585)
15 Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol h7585)
Pero ʼElohim redimirá mi alma del poder del Seol, Porque me llevará consigo. (Selah) (Sheol h7585)
16 Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
No temas cuando alguno se enriquece, Cuando aumenta el esplendor de su casa.
17 Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
Porque nada llevará al morir, Ni descenderá su esplendor tras él.
18 Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
Aunque se congratule mientras vive, Aunque sea alabado porque prospera,
19 naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
Se irá a la generación de sus antepasados Y nunca jamás verá la luz.
20 Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.
El hombre que vive con honor, Pero no entiende [esto], Es como las bestias que perecen.

< Zaburi 49 >