< Zaburi 42 >

1 Kama ayala ayatamanivyo maji ya mto. ndivyo hivyo ninakiu yako, Mungu.
BOOK II For the Leader; Maschil of the sons of Korah. As the hart panteth after the water brooks, so panteth my soul after Thee, O God.
2 Ninakiu yako Mungu, Mungu uliye hai, ni lini nitaonekana mbele zako?
My soul thirsteth for God, for the living God: 'When shall I come and appear before God?'
3 Machozi yangu yamekuwa ni chakula changu mchana na usiku, wakati maadui zangu siku zote wanasema, “Yuko wapi Mungu wako?”
My tears have been my food day and night, while they say unto me all the day: 'Where is Thy God?'
4 Mambo haya niayakumbuka ninapoumimina roho yangu: nilipoenda na umati wa watu na kuwaongoza kwenye nyumba ya Mungu kwa sauti ya shangwe na kusifu, ni wengi tulisherekea.
These things I remember, and pour out my soul within me, how I passed on with the throng, and led them to the house of God, with the voice of joy and praise, a multitude keeping holyday.
5 Roho yangu, kwa nini unainama? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu, Kwa kuwa kwa mara nyingine nitamsifu yeye ambaye ni wokovu wangu.
Why art thou cast down, O my soul? and why moanest thou within me? Hope thou in God; for I shall yet praise Him for the salvation of His countenance.
6 Mungu wangu, roho yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo ninakukumbuka toka nchi ya Yordani, toka kwenye vilele vitatu vya mlima Hermoni, na toka mlima wa Mizari.
O my God, my soul is cast down within me; therefore do I remember Thee from the land of Jordan, and the Hermons, from the hill Mizar.
7 Kina huita kina kwenye kelele za maporomoko ya maji yako; mawimbi na mafuriko yako yote yako juu yangu.
Deep calleth unto deep at the voice of Thy cataracts; all Thy waves and Thy billows are gone over me.
8 Wakati wa mchana Yahwe ataamuru uaminifu wa agano lake; na usiku wimbo wake utakuwa nami, ombi kwa Mungu wa uhai wangu.
By day the LORD will command His lovingkindness, and in the night His song shall be with me, even a prayer unto the God of my life.
9 Nami nitasema kwa Mungu wangu, mwamba wangu, “Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninaenenda katika maombolezo kwa sababu ya ukandamizaji wa adui yangu?”
I will say unto God my Rock: 'Why hast Thou forgotten me? Why go I mourning under the oppression of the enemy?'
10 Kama upanga mifupani pangu, maadui zangu wananikemea, siku zote wakiniambia, “Yuko wapi Mungu wako?”
As with a crushing in my bones, mine adversaries taunt me; while they say unto me all the day: 'Where is Thy God?'
11 Roho yangu, kwa nini umeinama chini? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu kwa kuwa nitamsifu tena yeye aliye wokovu wangu na Mungu wangu.
Why art thou cast down, O my soul? and why moanest thou within me? Hope thou in God; for I shall yet praise Him, the salvation of my countenance, and my God.

< Zaburi 42 >