< Zaburi 31 >

1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
For the Leader. A Psalm of David. In thee, O LORD, have I taken refuge; let me never be ashamed; deliver me in Thy righteousness.
2 Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
Incline Thine ear unto me, deliver me speedily; be Thou to me a rock of refuge, even a fortress of defence, to save me.
3 Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
For Thou art my rock and my fortress; therefore for Thy name's sake lead me and guide me.
4 Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
Bring me forth out of the net that they have hidden for me; for Thou art my stronghold.
5 Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
Into Thy hand I commit my spirit; Thou hast redeemed me, O LORD, Thou God of truth.
6 Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
I hate them that regard lying vanities; but I trust in the LORD.
7 Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
I will be glad and rejoice in Thy lovingkindness; for Thou hast seen mine affliction, Thou hast taken cognizance of the troubles of my soul,
8 Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
And Thou hast not given me over into the hand of the enemy; Thou hast set my feet in a broad place.
9 Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
Be gracious unto me, O LORD, for I am in distress; mine eye wasteth away with vexation, yea, my soul and my body.
10 Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
For my life is spent in sorrow, and my years in sighing; my strength faileth because of mine iniquity, and my bones are wasted away.
11 Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
Because of all mine adversaries I am become a reproach, yea, unto my neighbours exceedingly, and a dread to mine acquaintance; they that see me without flee from me.
12 Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
I am forgotten as a dead man out of mind; I am like a useless vessel.
13 Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
For I have heard the whispering of many, terror on every side; while they took counsel together against me, they devised to take away my life.
14 Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
But as for me, I have trusted in Thee, O LORD; I have said: 'Thou art my God.'
15 Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
My times are in Thy hand; deliver me from the hand of mine enemies, and from them that persecute me.
16 Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
Make Thy face to shine upon Thy servant; save me in Thy lovingkindness.
17 Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol h7585)
O LORD, let me not be ashamed, for I have called upon Thee; let the wicked be ashamed, let them be put to silence in the nether-world. (Sheol h7585)
18 Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
Let the lying lips be dumb, which speak arrogantly against the righteous, with pride and contempt.
19 Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
Oh how abundant is Thy goodness, which Thou hast laid up for them that fear Thee; which Thou hast wrought for them that take their refuge in Thee, in the sight of the sons of men!
20 Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
Thou hidest them in the covert of Thy presence from the plottings of man; Thou concealest them in a pavilion from the strife of tongues.
21 Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
Blessed be the LORD; for He hath shown me His wondrous lovingkindness in an entrenched city.
22 Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
As for me, I said in my haste: 'I am cut off from before Thine eyes'; nevertheless Thou heardest the voice of my supplications when I cried unto Thee.
23 Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
O love the LORD, all ye His godly ones; the LORD preserveth the faithful, and plentifully repayeth him that acteth haughtily.
24 Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.
Be strong, and let your heart take courage, all ye that wait for the LORD.

< Zaburi 31 >