< Zaburi 24 >

1 Nchi ni ya Yahwe, na vyote viijazavyo, dunia, na wote wakaao ndani yake.
Ein Psalm Davids. Die Erde ist des HERRN und was darinnen ist, der Erdboden und was darauf wohnt.
2 Kwa kuwa yeye aliianzisha juu ya bahari na kuiimarisha juu ya mito.
Denn er hat ihn an die Meere gegründet und an den Wassern bereitet.
3 Ni nani atakaye panda mlima wa Yahwe? Ni nani atakaye simama patakatifu pake?
Wer wird auf des HERRN Berg gehen, und wer wird stehen an seiner heiligen Stätte?
4 Yeye ambaye ana mikono misafi na moyo safi; ambaye hajauinua uongo, na haja apa kiapo ili kudanganya.
Der unschuldige Hände hat und reines Herzens ist; der nicht Lust hat zu loser Lehre und schwört nicht fälschlich:
5 Yeye atapokea baraka kutoka kwa Yahwe na haki kutoka kwa Mungu wa wokovu wake.
der wird den Segen vom HERRN empfangen und Gerechtigkeit von dem Gott seines Heils.
6 Kizazi cha wale wamtafutao Mungu ni kama hiki, wale ambao wanautafuta uso wa Mungu wa Yakobo.
Das ist das Geschlecht, das nach ihm fragt, das da sucht dein Antlitz, Gott Jakobs. (Sela)
7 Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
Machet die Tore weit und die Türen in der Welt hoch, daß der König der Ehren einziehe!
8 Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe, mwenye nguvu na uweza; Yahwe, mwenye uweza katika vita.
Wer ist derselbe König der Ehren? Es ist der HERR, stark und mächtig, der HERR, mächtig im Streit.
9 Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
Machet die Tore weit und die Türen in der Welt hoch, daß der König der Ehren einziehe!
10 Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe wa majeshi, yeye ni Mfalme wa utukufu.
Wer ist derselbe König der Ehren? Es ist der HERR Zebaoth; er ist der König der Ehren. (Sela)

< Zaburi 24 >