< Zaburi 24 >

1 Nchi ni ya Yahwe, na vyote viijazavyo, dunia, na wote wakaao ndani yake.
A Psalm of David. The earth is the LORD'S, and the fulness thereof; the world, and they that dwell therein.
2 Kwa kuwa yeye aliianzisha juu ya bahari na kuiimarisha juu ya mito.
For He hath founded it upon the seas, and established it upon the floods.
3 Ni nani atakaye panda mlima wa Yahwe? Ni nani atakaye simama patakatifu pake?
Who shall ascend into the mountain of the LORD? and who shall stand in His holy place?
4 Yeye ambaye ana mikono misafi na moyo safi; ambaye hajauinua uongo, na haja apa kiapo ili kudanganya.
He that hath clean hands, and a pure heart; who hath not taken My name in vain, and hath not sworn deceitfully.
5 Yeye atapokea baraka kutoka kwa Yahwe na haki kutoka kwa Mungu wa wokovu wake.
He shall receive a blessing from the LORD, and righteousness from the God of his salvation.
6 Kizazi cha wale wamtafutao Mungu ni kama hiki, wale ambao wanautafuta uso wa Mungu wa Yakobo.
Such is the generation of them that seek after Him, that seek Thy face, even Jacob. (Selah)
7 Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
Lift up your heads, O ye gates, and be ye lifted up, ye everlasting doors; that the King of glory may come in.
8 Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe, mwenye nguvu na uweza; Yahwe, mwenye uweza katika vita.
'Who is the King of glory?' 'The LORD strong and mighty, the LORD mighty in battle.'
9 Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
Lift up your heads, O ye gates, yea, lift them up, ye everlasting doors; that the King of glory may come in.
10 Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe wa majeshi, yeye ni Mfalme wa utukufu.
'Who then is the King of glory?' 'The LORD of hosts; He is the King of glory.' (Selah)

< Zaburi 24 >